• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC MAYEKA “TUNATAKA NAFASI YA KWANZA, YA TATU TUMEIZOEA”

Imewekwa: October 31st, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe. Mayeka S.Mayeka  amesema kuwa wazazi na walezi wanajukum kubwa la kuhakikisha wanashiriki vyema katika malezi  kwa kufuata na  kuzingatia  masuala mbalimbali  ya lishe  yanayotolewa na wataalam  ili kuiwezesha halmashauri kushika nafasi ya kwanza kwani imekuwa ikishika nafasi ya tatu mfululizo.


Kauli hiyo ameitoa leo tarehe 31/10/2023 wakati wa maadhimisho ya siku ya lishe kitaifa ambapo kiwilaya yameadhimishwa katika viwanja vya shule ya Msingi Mlimanjiwa iliyopo kata ya Mbugani wilayani Chunya.


‘’Nafasi ya tatu tumeizoea sasa tunataka nafasi ya kwanza niwaombe wazai, walezi na watoto mwendelee kusikliza na kufuata maelekezo ya wataalamu tulishika nafasi ya tatu kwasababu mlisikiliza na kufuata maelekezo ya wataalamu hivyo hata kushika nafasi ya kwanza itawezekana kama mtasikiliza na kufuatilia maelekezo yote mnayopewa na wataalamu.’’alisema Mhe. Mayeka.


Aidha amempongeza Mkurugenzi mtendaji , idara ya afya pamoja na idara zote  zinazohusika na masuala ya lishe kwa juhudi kubwa ambazo wamekuwa wakizifanya ikiwa ni pamoja na kutenga bajeti kubwa kwaajili ya kufanikisha masuala ya lishe  lakini pia  kuhakikisha watoto wanapata chakula wanapokuwa mashuleni.


Akitoa salam katika maadhimisho hayo Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Wilya ya Chunya ndugu Tamim Kambona amemuhakikishia mkuu wa Wilaya ya chunya kuwa uwezekano  wa kushika nafazi ya kwanza  upo kwani idara mbambali za halmashauri  zimepewa majukumu ya kutekeleza katika  masuala ya lishe ikiwepo idara ya kilimo  kwa kutengewa bajeti ili kuhakikisha mazao mbalimbali ya lishe yanalimwa na kutumiwa na wananchi ili kuboresha afya zao .


"lengo letu kama halmashauri ni kutoka kwenye nafasi ya tatu, ya pili na kushika nafasi ya kwanza kwani uwezo wa kufanya hivyo Mhe. Mkuu wa Wilaya tunao ni sisi kuamua na kujipanga kuhakkikisha yale yote yaliyoko kwenye bajeti zetu yanatekelezeka na hatimaye tuweza kufikia lengo la kushika nafasi ya kwanza katika masuala ya lishe” alisema Mkurugenzi.


Akimwakilisha Mgaga Mkuu wa Wilaya Daktari Edward Tengulaga  Mfamasia wa wilaya ya Chunya amesema kuwa lengo la kampeni ya lishe kwa Vijana rika balehe ni  kunusuru vijana rika balehe kwa kutoa elimu ya lishe kutokana na tafiti mbalimbali  zilizofanyika ambazozinaonyesha kuwa  hali duni ya lishe inaanzia mashuleni na kizaki kinachoathirika sana na lishe duni  ni kizazi rika balehe.


‘’Halmashauri ya Wilaya ya Chunya imefanya kampeni ya lishe kwa vijana rika balehe katika Shule za Sekondari Isenyela , Kiwanja na  Itewe Sekondari ambapo jumla ya vijana rika balehe  945 walipimwa hali ya lishae, wanafunzi wa kike 588 wanafunzi wa kiume  365 na kubaini wanafuzi 87 walikuwa na uzito uliozidi na wanafunzi 13 walionekana kuwa na ukondefu’’alisema  Tengulaga


Maadhimisho ya siku ya lishe kitaifa huadhimishwa kila mwaka mwezi Oktoba, kwa mwaka 2023/2024 maadhimisho haya yameadhimishwa leo 31/10/2023 yakioongozwa na kauli mbiu ‘’Lishe bora kwa Vijana Balehe, Chachu ya Mafanikio yao” ambapo wilaya ya Chunya imetumia viwanja vya shule ya msingi Mlimanjiwa kuadhimisha siku la Lishe Kitaifa ambapo yamekuhudhuriwa na Mkuu wa wilaya ya Chunya, Viongozi wa Chama cha Mapinduzi, Mkurugenzi mtendaji na  wataalam mbalimbali kutoka halmashauri , wananchi pamoja na wanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari.

Mkurugenzi Mtendaji wilaya ya Chunya Ndugu Tamimu Kambona akitoa salamu Mbele ya Mkuu wa wilaya ya Chunya wakati wa Maadhimisho ya siku ya Lishe yaliyofanyika viwanja vya shule ya msingi Mlimanjiwa

Kaimu Mganga Mkuu wa wilaya ya Chunya Dkt Edward Tengulaga akitoa salamu na mwenendo wa Lishe wilaya ya Chunya wakati wa Maadhimisho ya siku ya Lishe mwaka 2023 katika viwanja vya shule ya msingi Mlimanjiwa

Mkuu wa wilaya ya Chunya akimkabidhi cheti cha kufanya vizuri katika mkataba wa Lishe Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mlima Njiwa mw. Asajile Juma Ndiga wakati wa Maadhimisho ya siku ya Lishe

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Isenyela wakishiriki Mchezo wa Kuvuta kamba kati ya Timu yenye Lishe bora na Timu yenye lishe Duni wakati wa maadhimisho ya siku ya lishe


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.