• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC MAYEKA “MUWAELIMISHE WAKULIMA NA WAFUGAJI KUTUNZA CHAKULA”

Imewekwa: February 28th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe. Mayeka Simon Mayeka amewataka maafisa ugani na kilimo wilayani chunya kuwaelimisha wananchi kutunza Chakula ili kuepuka changamoto za kukosekana kwa chakula mwaka ujao jambo linaloweza kupelekea kushuka kwa uzalishaji na Nguvukazi kwa ujumla.

Mhe. Mayeka amesema hayo leo wakati akikabidhi pikipiki kwa maafisa ugani na kilimo wilayani chunya ikiwa ni mwendelezo wa zoaezi la ugawaji wa pikipiki kwa maafisa ugani, maafisa kilimo pamoja na watnedaji wa kata nchi, ambapo pikipiki 33 zimegawiwa kwa maafisa ugani na maafisa kilimo wilayani chunya

Mhe. Mayeka amewataka maafisa ugani na maafisa kilimo wilayani humo kuhakikisha wanatumia vitendea kazi hivyo kuwafikia wakulima kutatua changamoto zianzowakabili na baadaye kuleta tija katika familia na Taifa kwa ujumla

“Inawezekana tukavuna vizuri sana mwaka huu kutokana na mwenendo wa mvua lakini muhimu sana wakulima wasisitizwe kutunza chakula kwani maeneo mengine nchini na nje ya nchi hali sio nzuri, hivyo kupitia vitendea kazi hivi nendeni mkatusaidie kuhimiza wakulima kutunza chakula kwaajili ya matumizi yao hapo baadaye”

Aidha Mhe. Mayeka amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa namna ambavyo anasaidia kurahisisha utekelezaji wa majukumu ya kila siku kwa watumishi wake, sisi kazi yetu ni kumlipa kwa kutekeleza majukumu yetu kwa ufanisi

“Nimshukuru sana Mhe. Rais kwa namna anavyotusaidia kutekeleza majukumu yetu kwa kutupatia vifaa hivi, Hivyo Rais ametiza wajibu wake, wizara imetimiza wajibu wake, eneo lililobaki ni lako wewe. Hatutegemei uzembe wowote utajitokeza kwako, hivyo tunakutarajia wewe kuhakikisha wakulima na wafugaji wananufaika na hatimaye Taifa kwa ujumla wake”

Awali wakati akimkaribisha Mkuu wa wilaya ya Chunya, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mhe. Ramadhan Shumbi ambaye ni Diwani wa kata ya Mamba amewataka maafisa ugani na maafisa kilimo hao kuhakikisha tija ya kupewa vifaa hivyo inaonekana kupitia kazi

“Mmepewa vitendea kazi hivi ambavyo mkuu wa wilaya atakabidhi muda mchache ujao, nawaomba kazi ikafanyike kwani wako wakulima wanalima eneo kubwa na mapato ni kidogo hivyo kupitia vitendea kazi hivi mzunguke kutoa elimu ya kilimo ili wapate tija mfanye hivyo na kwa wafugaji pia” amesema Mhe Shumbi

Kwaniaba ya Maafisa ugani na Maafisa kilimo walipokea pikipiki hizo, Afisa kilimo Felis Mendrad kutoka kata ya Mamba na Msafiri Sufiani Magasa afisa ugani kata ya Mbugani kwa pamoja wameishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa vifaa hivyo na pia wamemshukuru Mkuu wa wilaya ya Chunya  kwa kuwakabidhi vifaa hivyo na wameahidi kuvitumia kama maelekezo yanavyoeleza na lengo kubwa ikiwa ni kuleta tija kwa wakulima na wafugaji katika maeneo yao ya kazi

Jumla ya pikipiki 33 zimegawiwa leo ambapo pikipiki 27 zimegaiwa kwa maafisa kilimo na maafisa ugani wakati pikipiki 6 zimegawiwa kwa maafisa watendaji wa kata.

 


Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe. Mayeka S. Mayeka akimkabidhi pikipiki Bi. Felis Mendrad Afisa Ugani wa kata ya Mamba


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.