• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC MAYEKA “MKAVITUNZE VIZURI VITAMBULISHO HIVI MAANA NDIO UTAMBULISHO WA URAIA WAKO”

Imewekwa: December 8th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka S Mayeka amewataka wananchi wa wilaya ya Chunya kutunza vitambulisho vya Taifa walivyovipata kwani vina umuhimu mkubwa kwao ikiwa ni pamoja na utambulisho wa Utaifa wao

Ametoa Kauli hiyo Mapema leo tarehe 8/12/2023 katika viwanja vya stendi ya Mabasi Chunya wakati akizindua rasmi zoezi la ugawaji wa vitambulisho vya Taifa ambapo wilaya ya Chunya imepata zaidi ya vitambulisho elfu sabini na saba

“Wanachunya naomba tuvitunze vizuri vitambulisho hivi kwani ni utambulisho wa uraia wako lakini pia hutumika maeneo mbalimbali ili kukutambua na kukupatia huduma, lakini pia vitambulisho hivyo msipovitunza vikaangukia  kwenye mikono ya watu wabaya basi vinaweza kutumika kukutia hatiani au kukuhusisha na matukio mabaya”

Awali akitoa taarifa kwa Mkuu wa wilaya ya Chunya katika Hafla hiyo, Afisa usajili wilaya ya Chunya Bi Emma  Ndunguru ameishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuhakikisha wananchi wa Chunya wanapata vitambulisho vya Taifa na kwa awamu hii wilaya hiyo imepata vitambulisho Elfu sabini na saba na mia mbili arobaini na tatu (77,243)

“Tunaishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuhakikisha wananchi wa wilaya ya Chunya wanapata vitambulisho kwani mpaka sasa Chunya tumepokea vitambulisho 92315 ambapo awamu ya kwanza tulipokea vitambulisho 15072 na awamu hii tumepokea vitambulisho 77,243” alisema Bi Emma    

Akitoa salamu za wananchi wa kijiji cha Kibaoni mbele ya Mkuu wa wilaya ya Chunya Mwenyekiti wa kijiji hicho Bwana Joshua Mlambalala amemshukuru mkuu wa wilaya ya Chunya kuiteua kata ya Chokaa na hasa kijiji cha Kibaoni ili kuwakilisha vijiji vingine vya wilaya ya Chunya katika uzinduzi wa Zoezi hilo la ugawaji wa vitambulisho vya Taifa

“Nakushukuru sana Mhe Mkuu wa wilaya ya Chunya kwa kutupatia nafasi hii ya kuwakilisha maeneo mengine ya wilaya ya Chunya kuzindua zoezi hili muhimu la ugawaji wa vitambulisho vya Taifa, tunatambua yapo maeneo mengi katika wilaya hii lakini ukasema zoezi hili lifanyike kijiji cha Kibaoni, Sisi wana kibaoni tunakushukuru”

Zoezi la uzinduzi wa ugawaji wa vitambulisho vya Taifa limefanyika kata ya Chokaa kwenye kijiji cha Kibaoni eneo la stendi ya mabasi ambapo Mkuu wa wilaya ya Chunya amezindua zoezi hilo kwa kugawa vitambulisho kumi kwa wananchi, na zoezi la ugawaji wa vitambulisho hivyo litaendelea kwenye ofisi za vijiji na kata ambapo wananchi wanapaswa kufika ofisi za kata kuona majina yao na hatimaye kuchukua vitambulisho hivyo, Kumbuka kitambulisho hicho ni haki yako na ni bure kabisaa

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka S Mayeka akizungumza na wananchi waliojitokeza wakati wa hafla ya uzinduzi wa ugawaji wa vitambulisho vya Taifa Mapema leo katika viwanja wa Stendi ya Mabasi Chunya

Katibu tawala wilaya ya Chunya Bw Anakleth Michombero akizungumza kabla ya kumkaribisha Mkuu wa wilaya ya Chunya wakati wa Hafla ya uzinduzi wa ugawaji wa vitambulisho mapema leo

Mkuu wa wilaya ya Chunya (Aliyeavaa suti) akikata utepe ili kuzindua zoezi la ugawaji wa Vitambulisho, mwenye tisheri ya Blue bahari ni mtendaji wa kata ya Chokaa na mwenye tisherti nyekundu ni mwenyekiti wa kijiji cha Kibaoni

Mkuu wa wilaya ya Chunya akikabidhi kitambulisho cha Taifa kuashiria uzinduzi rasmi wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho hivyo wilayani Chunya

Afisa msajiliwa NIDA wilaya ya Chunya Bi Emma Ndunguru akisoma taarifa mbela ya Mkuu wa wilaya ya Chunya wakati wa uzinduzi wa zoezi la Ugawaji wa vitambulisho vya Taifa mapema leo

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.