• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC MAYEKA AWATAKA BODABODA WAWE NA MCHANGO CHANYA KWA TAIFA

Imewekwa: October 30th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka S. Mayeka amewataka madereva bodaboda na madereva bajaji kubadirika ili kubadiri mitazamo hasi ya watu wengine dhidi yao akisema kwa kufanya hivyo watatoa mchango chanya kwa jamii yao na Taifa lao la Tanzania tofauti na ilivyo sasa


Ametoa kauli hiyo mwishoni mwa juma wakati alipofanya mazungumzo na maafisa usafirishaji (Madereva bodaboda na madereva bajaji) wanaofanya shughuli zao ndani ya wilaya ya Chunya hasa maeneo ya Chunya Mjini kikao kilichofanyika ukumbi wa Mikutano Sapanja, huku akisema vikao hivyo vitakuwa na mwendelezo mpaka kuwafikia maafisa usafirishaji wote wanaofanya kazi zao ndani ya wilaya ya Chunya kwa ujumla wake.


“Wako watu wanabeza kazi yenu na kudharau kazi hii lakini mimi najua ninyi mumejenga, mnasomesha kupitia kazi hii na pia familia zenu zinawategemeeni sana badirikeni muanze sasa kuheshimu sheria za usalama barabarani kwa usalama wenu ninyi na usalama wa watumiaji wengine wa barabara”


Aidha Mkuu wa wilaya ya Chunya amewataka madereva Boda boda kuwa wazalendo kwa Chunya yao na Nchi yao kwa ujumla ili kuona uwezekana wa kusaidia taifa lao kupitia kazi yao kwa kufichua njama na siri nyingine ambazo zina manufaa makubwa kwa Chunya na Taifa kwani wao wanajua siri nyingi sana kupitia kazi yao ya usafirishaji wa abiria na mizigo kutoka eneo moja kwenda eneo lingine.


“Madereva bajaji na madereva bodaboda mna siri nyingi sana kwanza kuhusu familia zetu na hata siri za watoroshaji wa madini na hata siri nyingine ambazo mkishirikiana nasi mtasaidia sio wilaya ya Chunya tu bali Taifa zima hivyo niwaombe kuwa wazalendo kwa nchi yenu ili tushirikiane kuhakikisha Chunya inasonga Mbele na hamiye Taifa kwa ujumla wake”.


Awali akitoa salamu kwa mkuu wa wilaya kwa niaba ya madereva bodaboda wenzake Mwenyekiti wa umoja wa waendesha bodaboda wilaya ya Chunya ndugu Samson Mwanswa alipeleka ombi lao la kupatiwa ofisi ili waweze kushiriki ipasavyo kusimamia taratibu na miongozo waliyojiwekea na hatimaye kutoa ushirikiano unaofaa kwa jeshi la polisi ukianzia kikosi cha usalama barabarani na baadaye jeshi la polisi kwa ujumla.


“Ombi letu ni moja tu kwako Mhe Mkuu wa wilaya, Tunaomba tupate ofisi na ombi hili tuliwahi kulileta katika ofisi yako na tuliambiwa kwakuwa ofisi nyingi zitahamia jengo jipya ambapo mpaka sasa ofisi zimeshahamia huko lakini ombi letu halijashughulikiwa hivyo tunaomba sana tupate ofisi ili kurahisha utendaji kazi wetu kwa ujumla wake”.


Kikao hicho cha Mkuu wa wilaya ya Chunya na maafisa usafirishaji yaani waendesha bajaji na waendesha bodaboda kimekuja ikiwa ni juhudi yake ya kuendelea kushirikisha wananchi katika kuleta maendeleo kupitia makundi mbalimbali kila mmoja kwa nafasi yake kuhakikisha wilaya ya Chunya inakuwa salama wakati wote na wananchi wanafanya majuku yao ya kawaida kwa amani na utulivu

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka akizungumza na maafisa usafirishaji (Madereva boda boda na bajaji) katika ukumbi wa Mikutano Sapanjo

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.