• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC MAYEKA “ASANTE NMB KWA KUMUUNGA MKONO RAIS WA JAMHURI YA MMUNGANO WA TANZANIA”

Imewekwa: October 17th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe. Mayeka S.Mayeka  amesema Banki ya NMB inaunga mkono Juhudu za serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa namna wanavyotoa huduma zao kwa wananchi na kwa michango yao mbalimbali wanayoitoa kuhakikisha jamii inakuwa bora wakati wote


Kauli hiyo ameitoa leo 17/10/2023 kwenye viwanja vya Hospitali ya wilaya ya Chunya  wakati  akipokea vifaa mbalimbali vyenye thamani ya shilingi milioni tisa (9,000,000/=) vilivyotolewa na Banki ya NMB  ili visaidie kupunguza changamoto kwenye sekta ya Afya na Elimu ikiwa ni sera ya banki hiyo kurudisha faida kwa wananchi ambao ndio wateja wa Banki hiyo.


“Nawashukuru sana banki ya NMB kwa huduma na   mchango mkubwa  ambao benki ya NMB inatoa kwaajili ya kusaidia jamii katika sekta ya afya na elimu   Lakini pia  kwa kwendelea kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuhuri ya Muuungano wa Tanzania  kwani mchango huo utasaidia kupunguza changamoto  katika vituo vya afya vitakavyo nufaika na vifaa hivyo ambavyo ni kituo cha Afya cha  Makongolosi pamoja na kituo cha Afya Kalangali pamoja na wanafunzi wenye ulemavu katika shule ya Msingi Lupa”


Kaimu meneja wa kanda nyanda za juu  wa banki ya National Bank of Commarce (NMB)  ndugu Frank Rutakwa  amesema kuwa suala la afya ni moja ya vipaumbele vyao kama Benki  ili kuhakikisha afya za watanzania wanao wahudumia zinakuwa bora   pamoja na kuunga mkono juhudi za serikali  katika sekta ya afya


 “Sisi kama Benki ya NMB  afya ni kipaumbele chetu  na ndio mana katika sekta ambazo tumejikita kusaidia serikali ni pamoja  na sekta ya afya  , lakini pia tunaunga mkono  juhudi za Mheshimiwa Rais katika sekta ya afya kama ambavyo  Raisi wetu   anaipa kipaumbele sekta ya afya’’alisema Rutakwa.


Naye Mkurugenzi mtendaji  wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Tamim Kambona ameishukuru benki ya NMB  kwa mchango mkubwa ilioutoa ikiwa ni sehemu ya kile ambacho wanakipata  na kuahidi  kwamba wao kama Halmashauri wateendelea kutoa ushirikiano  kwa Banki hiyo kama ambavyo wamekuwa wakishirikiana maeneo mbalimbali katika kulijenga Taifa.

 Kwaniaba ya idara ya Afya wilaya ya Chunya, Mganga mkuu wa mkoa wa Mbeya Daktari Elizabeth  Nyema  ameishukuru benki ya NMB  kwa kuendelea kuunga mkono sekta ya afya  kwa kuwapatia vifaa mbalimbali ambavyo wamevitoa  ili kuhakikisha  wanaendelea kuwahudumia wananchi ipasavyo kwani afya ndio msingi wa uzalishaji mali si kwa mwananchi wa Chunya tu bali pia jamii   ya watanzania wote.


Vifaa vilivyokabidhiwa ni  pamoja na  vitanda 10 vya kulazia wagonjwa, vitanda  2 vya kujifungulia wakinamama wajawazito  pamoja na viti mwendo 7 kwaajili ya  wanafunzi wenye ulemavu na vifaa hivyo vimepatikana ikiwa ni kutimiza lengo la Benki hiyo ya kurudisha fadhila kwa wateja wake ambapo kila mwaka shughuli mbalimbali za kijamii hufanyika.

Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe Mayeka S.Mayeka (Kulia na aliyevaa miwani) akimkabidhi kitanda cha kulazia wagonjwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Tamim Kambona (Kushoto) baada ya kupokea vifaa hivyo kutoka kwa kaimu meneja wa Banki ya NMB nyanda za juu kusini

Kaimu meneja wa Benki ya NMB ndugu Frank Rutakwa (Mwenye suti ya blue), Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka S. Mayeka (katikati aliyevaa miwani), Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Tamimu Kambona (anayetazama simu), anayefuata ni Mganga mkuu wa mkoa wa Mbeya Daktari Elizabeth  Nyema na anayemalizia upande wa kushoto ni Dr Darison Andrew mganga mkuu wa wilaya ya Chunya (Mwenye Shati la Blue)

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.