• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC MAYEKA APONGEZA JUHUDI ZINAZOFANYWA NA WCS CHUNYA

Imewekwa: November 4th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe. Mayeka S. Mayeka  amewashukuru na kupongeza  juhudi mbalimbali  zinazofanywa na  Shirika lisilokuwa la kiserikali la Wildlife Conservation Society (WCS)  kwa kazi kubwa wanazozifanya katika kuisaidia serikali na jamii kwa ujumla wilayani Chunya.


Ametoa pongezi hizo leo 4/11/2023 kwenye kikao kilichofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya na kuhudhuriwa na Afisa uhifadhi wanyamapori wa Hamashauri ya wilaya ya Chunya, kamati ya usalama ya wilaya ya Chunya , kaimu katibu tawala na viongozi wengine wakiwepo viongozi mbalimbali wa shirika hilo kuanzia ngazi ya Taifa, Mkoa,  Mratibu wa mradi na wafanyakazi wengine  wa shirika hilo.


“Niwashukuru na kuwapongeza kwa  kazi kubwa  ambazo mnazifanya  Chunya  kwa kufanya shughuli mbalimbali ambazo mnaisaidia serikali na mmeweka alama katika halmashauri ya Wilaya ya Chunya  tunaona juhudi zenu  na niseme tu kwakila kitu mnachohitaji  milango iko wazi tunawakaribisha sana na tutawapatia ushirikiano wa kutosha”  alisema Mhe. Mayeka


Aidha Mhe Mayeka  amewaomba WCS  wanapokutana na wafadhili wao kuendelea kuangalia namna ambavyo wataendelea kuwasaidia wananchi  waliokubali  maeneo yao kuhifadhiwa kwaajili ya mapitio ya Wanyama kwani katika maeneo hayo wananchi  walikuwa wakiyategemea kwa shughuli mbalimbali  za kiuchumi kama kilimo , malisho mawindo pamoja na uvunaji wa asali  kwaajili ya kujipatia kipato.


“Kama tunataka uendelevu wa mradi kwa maeneo hayo ya hifadhi  ni vizuri kuiangalia jamii husika ya maeneo hayo na kuzisaidia   juu ya  shughuli ndogo ndogo ambazo  wanaweza wakazifanya kwaajili ya kujipatia kipato ikiwa ni pamoja na kuwatengea maeneo ya malisho kwaajili ya mifungo yao  kuwapandia nyasi kwaajili ya chakula cha mifugo lakini pia masoko kwaajili ya bidhaa zao kama vile asali. Aliongeza Mhe Mayeka


Awali akiongea katika kikao hicho Mkurugenzi wa WCS Mkoa wa Mbeya Dr Luthando Dziba akiwawakilisha viongozi wa taasisi hiyo  amemshukuru Mkuu wa wilaya kwa ushirikiano ambao wameendelea kuupata kwa kipindi chote  kupitia mradi wa Kuhifadhi mapitio ya Wanyama  yani Ruaha –katavi  unaotekelezwa katika maeneo ya Sipa, Kambikatoto , Bitimanyanga na Mafyeko kwa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya.


‘’Tunashukuru kwa ushirikiano mkubwa ambao tunaupata kutoka kwako na Viongozi wengine , tumekuwa na  ushirikiano na mahusiano mazuri pia hata kwa jamii ambayo imetoa maeneo yao na tutakuwa na amani kama tutaacha alama kwa jamii ambako mradi huu unatekelezwa kwa kuangalia namna ambavyo na wao watanufaika’’ alisema  Dziba


Shirika la WCS linatekeleza miradi yake katika nchi za Afrika Mashariki ikiwemo Tanzania   ambako wanatekeleza mradi wa kuhifadhi mapitio ya wanyama poli   yani Ruaha –Katavi  katika maeneo tofauti tofauti na  Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ikiwa miongoni mwa maeneo hayo yanayonufaika na WCS.

 

Mkurugenzi wa WCS Mkoa wa Mbeya Dr Luthando Dziba akizungumza jambo wakati wa kikao cha shirika hilo na Mkuu wa wilaya ya Chunya kilichofanyika katika ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Chunya leo tarehe 4/11/2023

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka akizungumza kwa kushukuru mbele ya Uongozi wa WCS walipokuja ofisini kwake mapema leo tarehe 4/11/2023

Wajumbe wa kikao cha  Mkuu wa wilaya ya Chunya na WCS  Kilichoketi Mapema leo kilichofanyika ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Chunya

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.