• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC Mayeka afanya ziara kitongoji cha Mpembe kutatua kero za wananchi.

Imewekwa: June 13th, 2022

MKUU wa Wilaya ya Chunya Mhe. Mayeka S. Mayeka akiambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya pamoja na Wataalam toka Halmashauri ya Wilaya ya chunya wamefanya mkutano wa hadhara katika kitongoji cha Mpembe kwa ajili ya kusikiliza kero za wananchi na kuzipatia ufumbuzi.

Akizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano huo, Mkuu huyo wa Wilaya alianza kwa kuwataka wananchi wa kitongoji hicho kueleza matatizo yanayowakabili,

“Kikao chetu kipo wazi kabisa uwe huru kueleza kero yoyote na mimi nitaichukua kama nina uwezo wa kuitatua hapa hapa na wenzangu tutafanya hivyo lakini Kama ni lazima niende nikaifanyie kazi nitafanya hivyo pia.” Alisema Mhe. Mayeka.

Pia DC Mayeka aliwataka wananchi hao kuwa wawazi katika kueleza changamoto zao hata kwa mambo ambayo hawayafahamu vizuri waulize ili wapatiwe ufafanuzi mzuri kutoka kwa wataalam alioambatana nao.

Wananchi wa kitongoji cha Mpembe wengi wao walionekana kuwa na changamoto ya uelewa juu ya Shamba la Korosho, Huduma ya Afya, miundombinu ya barabara sambamba na kero ya shule kuwa mbali na maeneo wanapoishi.

Akieleza kero yake kwa Mkuu wa Wilaya, Ndugu Joseph Gamba alisema, matatizo yamekuwa yakiibuka mara kwa mara, kitu kinachowasababisha kushindwa kufanya mandeleo katika kitongoji chao.

“Hapo kipindi cha nyuma tuliambiwa tuhame huku kuna TANAPA, limetoka hilo limekuja suala la korosho, tunaambiwa tuhame humu ni eneo la shamba la korosho tunashindwa hata kufanya maendeleo”

Akijibu kero za wananchi hao kuhusu shamba la korosho, Mayeka amesema, wananchi wamepotoshwa sana kwa jinsi wanavyolizungumzia suala la korosho ambapo inaonekana wamepewa taarifa tofauti na suala lenyewe lilivyo.

“Sasa hivi baada ya kuligusa eneo la shamba la korosho imeonekana miundombinu yote ipo kule, kana kwamba hakuna maeneo mengine huku kwamba ukigusa eneo la korosho hamtajenga shule na kufanya maendeleo, sio kweli taarifa mlizopewa.” Aisema Mayeka.

“Hili shamba ni shamba ambalo Serikali inaligharamia lenyewe, hao wanaotoa visiki ni hatua za mwanzo zitakuja mashine kutengeneza vizuri na kuligawa, hilo litafanyika, hayo hayawezi kufanyika kama hakuna barabara nzuri itakayotufikisha Chunya.” Aliongezea Mayeka.

Aliendelea kusema serikali inatekeleza ujenzi wa daraja eneo la mbanga ili kuweza kutengeneza miundombinu ya barabara kuja katika mradi wa shamba la korosho utakaotekelezwa katika kitongoji cha Mpembe.

Kwa upande wa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, Ndg Curthbert Mwinuka amesema, Shamba la Korosho Lualaje limekuja baada ya uongozi wa Kijiji cha Lualaje kupendekeza mradi huo kufanyika katika kijiji chao eneo la Gibiso

“Tuliandika barua kwenye Serikali za Vijiji zote, lakini kijiji cha kwanza kujibu kwamba tuje ni kijiji cha Lualaje, lakini tuliwaandikia barua ile sio kunyang’anya mashamba ya wananchi, tuliwaambia tunataka kulima korosho kwenye misitu ya kijiji ambayo tunayovuna mkaa.” Alisema Mwinuka.

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.