• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

CHUNYA KUONGEZA NGUVU MAPAMBANO VVU

Imewekwa: December 1st, 2025

Afisa tawala wa wilaya ya Chunya Bi Semwano Mlawa kwaniaba ya Mkuu wa wilaya ya Chunya amewataka wananchi wa wilaya ya Chunya kuendelea kujitokeza kuchunguza maambukizi ya Virusi vya Ukimwi huku akisisitiza kutumia dawa za kufubaza virusi hivyo kwa wale wenye maambukizi kwani kupata virusi sio mwisho wa Maisha

Akizungumza wakati wa maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani ambayo huadhimishwa kila tarehe mosi ya mwezi Desemba ambapo kwa Halmashauri ya wilaya ya Chunya maadhimisho hayo yamefanyika viwanja vya Zahanati ya zamani iliyoko kata ya Makongolosi, Mamlaka ya mji mdogo

“Kwa karne ya sasa Virusi vya Ukimwi sio jambo jipya, kwani kila mmoja wetu anafahamu, hivyo nipo hapa kuwaomba wananchi wa Chunya wote kwanza tuendelee kujitokeza kupima ili kujua maambukizi ya virusi hivyo lakini pia ikiwa umepata maambukizi basi tumia dawa kwani kupata virusi vya Ukimwi sio mwisho wa Maisha” alisema Bi Semwano

Aidha Bi Mlawa amewataka Maafisa wote na jamii nzima kuongeza juhudi kuhakikisha elimu ya VVU inawafikia wananchi wote Pamoja na wanafunzi kupitia klabu zao zilizopo mashuleni kwani kwa kufanya hivyo inaongeza ufanisi wa mapambano ya Ugonjwa huu

Kaimu Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii wilaya ya Chunya Ndugu Anton Denga amesema Halmashauri inatumia njia mbalimbali kuelimisha jamii kuhusu VVU na Ukimwi ili jamii iweze kuwa na uelewa mkubwa na hatimaye kuungana katika mapambano ya maambukizi ya Virusi vya Ukimwi na Ukimwi kwa ujumla wake.

Denga amesema wananchi wa Chunya wanafikiwa na Elimu kwa njia za makundi rika, Klabu mbalimbali zilizoko Shule za Msingi na Sekondari, Mikutano mbalimbali ya hadhara Pamoja na makongamano mbalimbali yanayoandaliwa mahusui kwaajili ya kutoa elimu

Afisa Elimu Kata wa kata ya Makongolosi Chunya Bi Rebecca Mkisi amewashukuru wananchi wote Pamoja na viongozi kwanza kuhudhuria kwenye maadhimisho hayo lakini pia kuwa mabalozi wazuri wa yale yaliyozungumzwa kwa wengine ambao hawajafika katika hafla hiyo maadhimisho ya siku ya Ukimwi

Maadhimisho ya siku ya Ukimwi Duniani hufanyika kila Desemba mosi ambapo Halmashauri ya wilaya ya Chunya maadhimisho hayo yamefanyika viwanja vya zahanati ya zamani iliyopo kata ya Makongolosi mamlaka ya mji mdogo, ambapo Pamoja na mambo mengine wananchi waliohudhuria wamepatiwa Elimu ya lishe pia

Baadhi ya wananchi waliojitokeza kushiriki kwenye maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani katika Halmashauri ya wilaya ya Chunya, Viwanja vya zahanati ya zamani kata ya Makongolosi

Matangazo

  • KUPIGA KURA YA RAIS KITUO AMBACHO HAUKUJIANDIKISHA September 15, 2025
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • CHUNYA KUONGEZA NGUVU MAPAMBANO VVU

    December 01, 2025
  • HAKIKISHENI MASHAMBA YOTE YA SHULE YANALIMWA MSIMU HUU WA MVUA.

    November 27, 2025
  • MILLION 789.500,000 ZA KABIDHIWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU CHUNYA.

    November 21, 2025
  • WAJUMBE WA BARAZA LA BIASHARA CHUNYA WAMETOA YA MAYONI

    November 20, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.