• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC CHUNYA “VIFAA VINUNULIWE KWA BEI YA SOKONI”.

Imewekwa: June 2nd, 2023

Kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Chunya ikiongozwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe Mayeka S Mayeka Mkuu wa wilaya ya Chunya Wameziagiza kamati zote za Ujenzi kuhakikisha vifaa vya ujenzi wa miradi ya BOOST vinanunuliwa kwa bei iliyoko dukani huku wakiwataka wajumbe wote wa kamati za ujenzi kuwepo eneo la mradi wakiwa na Nyaraka zote zinazohusu ujenzi huo ili kujibu hoja zinazotolewa na viongozi mbalimbali wanapokuja kukagua mradi husika

Mhe. Mayeka ametoa maelekezo hayo wakati alipoiongoza Kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya kwenye ziara ya kukagua na kutembelea miradi ya Boost inayotekelezwa na Halmashauri, ziara hiyo imedumu kwa siku mbili kuanzia tarehe 31/5/2023 hadi tarehe 1/5/2023 ambapo miradi yenye thamani ya zaidi ya bilioni 1.4 imetembelewa na kukaguliwa

Kamati hiyo imeshauri mambo mbalimbali ili utekelezaji wa miradi hiyo uwe wenye tija, Mambo hayo ni pamoja  na;

Kwanza kuhakikisha kamati zote za ujenzi zinakuwepo eneo la mradi wakati wote ili kuhakikisha ufanisi wa utekelezaji wa mradi huo unakuwa wenye ubora

Pili, Kuhakikisha Nyaraka zote zinazohusiana na mradi huo zinapatikana katika eneo la mradi kila viongozi na kamati mabalimbali zinapotembelea miradi hiyo, Na nyaraka hizo ziwe zenye ukamilifu na zenye ukweli ili kuepuka usumbufu unaweza kujitokeza hapo baadaye

Tatu, Kamati imemwagiza mhandisi wa Halmashauri ya wilaya kuwepo eneo la mradi ili kuhakikisha ushauri wowote wa kitaalamu kwa mafundi wanaojenga mradi wanaupata kwa wakati ili kuepusha ucheleweshaji wa mradi huo

Nnne, Wamezielekeza kamati zote zinazosimamia mradi wa ujenzi wa Madarasa mawili katika Shule shikizi ya Mkange kwenda kuzungumza na Mzabuni anayewauzia vifaa vya ujenzi kupunguza bei ya saruji kutoka elfu kumi na nane (18000) na kuwa  elfu kumi na saba na miatano (17500) kama ilivyo kwenye miradi mingine

“Kwanini mnunue saruji kwa bei kubwa kuliko miradi mingine yote wilayani Chunya? Kule Kanoge shule ya Msingi wananua saruji kutoka Chunya ambako ni mbali kuliko mnako nunua ninyi lakini wananunua kwa 17500/= ila ninyi 18000, hivyo tunawataka mzungumze na mzabuni wenu kupunguza bei hiyo” Alihoji Mwenyekiti wa kamati Mhe Mayeka

Vile vile kamati kupitia mwenyekiti wake imewataka wananchi kushiriki ipasavyo kwa namna mbalimbali ikiwa ni kusogeza fursa,zinazopatikana katika maeneo yao, kufika eneo la mradi na kuona maendeleo yake lakini kulinda mradi huo ili miradi hiyo ilete tija iliyokusudiwa maana lengo la miradi inayojengwa na serikali ni kuwasaidia wananchi.

Halmashauri ya wilaya ya Chunya ilipokea fedha kiasi cha shilingi bilioni moja na milioni mia nne themanini na mbili na laki moja (1,482,100,000) kupitia mradi wa kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji kwa shue za awali na Msingi (BOOST) ili kujenga shule mpya Mbili pamoja na kujenga madarasa mawili na ofisi moja kwa shule nane zilizoteuliwa. Shule Mpya moja inajengwa kata ya Makongolosi na Nyingine inajenwa kata ya Mafyeko ambapo kila moja imetengewa milioni mia tano thelasini na nane na laki tano (538.500.000/=)


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.