• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC CHUNYA “KILA MWANANCHI AWE MLINZI WA MWENZIYE”

Imewekwa: September 8th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka S Mayeka amewataka wananchi wa wilaya ya Chunya kila mmoja kushiriki katika kutunza, kulinda na kuendeleza vyanzo vya maji vilivyopo wilayani humo kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vizazi vijavyo


 Ametoa kauli hiyo leo 8/9/2023 wakati akizungumza na wananchi waliojitokeza kushuhudia mitambo ya kuchimba visima ikiendelea na zoezi la uchimbaji wa kisima cha maji katika kata ya Upendo ikiwa ni mwendelezo wa azma ya serikali kuchimba visima 26 vya maji katika halmashauri ya wilaya ya Chunya na kata ya Upendo ni miongopni mwaka kata zitakazonufaika na mradi huo


“Kila mwananchi awe mlinzi wa mwenziye si kwa kipindi hiki cha maandalizi ya mbio za Mwenge wa uhuru tu bali kwa kipindi chote, Lakini pia wako watu watafungwa msishangae maana sheria zipo zinazokataza watu kuharibu mazingira hivyo lindeni maeneo ya vyanzo vya maji ili maji yaendelee kuwepo hata kwaajili ya vizazi vijavyo”


Aidha Mhe. Mayeka amewataka wananchi wa kata ya Upendo kuhakikisha eneo hilo halitumiki kama sehemu ya malisho au sehemu ya kufyatua tofali kwani kufanya hivyo mtakuwa mtakuwa mnaharibu chanzo hiki cha maji jambo linaloweza kupelekea maji kupungua na hatimaye kukosekana kabisa hivyo tunzeni kisima hiki vizuri


“Tafadhali sana linden kwa pamoja  kisima hiki na eneo lote la chanzo cha Maji na kwa kufanya hivyo mtakuwa mmemuunga mkona Mama yetu Mpendwa Mhe Samia Suluhu Hassan  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwani ndiye aliyenunua mitambo hii mnayoiona ili wanachunya na watanzania kwa ujumla wapate maji”


Naye Diwani wa kata ya Upendo Mhe.Richard N. Itelekelo kwa niaba ya wananchi wa kata ya Upendo ameishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwanza kupata mitambo ya maji lakini pia Kata ya Upendo kuwa miongozi mwa wanufaika wa moja kwa moja wa mitambo hiyo ya Uchimbaji wa maji na ameahidi kuendelea kulinda kisima hicho pamoja na vyanzo vya maji vilivyopo katika kata ya Upendo


Mradi wa Uchimbaji wa visma wilayani Chunya unataraji kuchimba visima 26 na utagharimu fedha kiasi cha shilingi milioni mia tisa na kumi (910) mpaka kukamilika kwake na kisima hicho kinachochimbwa kata ya upendo kitawakilisha visima vingingine vyote vinavyochimbwa wilayani Chunya kwa kupitiwa na mwenge wa uhuru mwaka 2023 ambapo kwa wilaya ya Chunya utakimbizwa tarehe 13/09/2023.

Diwani wa kata ya Upendo Mh. Richard N. Itelekelo akitoa salamu za wananchi wa kata ya Upendo kwa Mkuu wa wilaya ya Chunya alipotembelea kuona namna kazi inavyoendelea katika kata hiyo

Baadhi ya wananchi wa kata ya Upendo waliojitokeza kushuhudia utekelezaji wa ahadi za serikali ya awamu ya sita katika sekta ya maji kwa wananchi muda huo wakimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Chunya alipotembelea kuona maendeleo ya kazi ya kuchimba kisima katika kata ya Upendo

Mtambo wa kuchimba visima vya maji chini ya wahandisi wa maji ukiendelea na kazi ya kuchimba kisima katika kata ya upendo, Mbele ya picha hiyo kunaonekana baadhi ya wananchi waliojitokeza kushuhudia namna zoezi la kuchimba maji likiendelea


Wahandisi wa maji wakiendelea na kazi ya kuchimba kisima cha cha Maji katika kata ya Upendo na Pembeni kidogo wananchi wakimsikiliza Mkuu wa wilaya alipotembelea kuona zoezi la uchimbaji wa maji linavyoendelea katika kata ya Upendo

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.