• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC BATENGA: “WEKENI VIZURI KUMBUKUMBU ZA UMILIKI WA MAENEO AMBAPO MIRADI INATEKELEZWA”

Imewekwa: May 28th, 2024

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mbarak Alhaji Batenga amewataka viongozi wa vijiji na kata kuhakikisha wanaweka vizuri Nyaraka za kumbukumbu za umiliki wa maeneo ambapo miradi mbalimbali ya Maendeleo inajengwa ili kuepuka migogoro ya ardhi mbele pindi kizazi hiki kitakapokuwa kimepita

Ametoa kauli hiyo leo tarehe 28/05/2024 wakati akiongoza kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Chunya wakiambata na wataalamu kutoka taasisi mbalimbali za Serikali katika wilaya ya Chunya ili kukagua utekelezaji wa mradi wa maji unaojengwa na shirika la Catholic Relief Services (CRS) kwa gharama ya shilingi milioni mia tatu hamsini na tano

Akitoa Taarifa ya utekelezaji wa mradi huo mbele ya Kamati ya Ulinzi na Usalama, Meneja wa mradi huo kutoka Shirika na CRS Bi Bertha Mkepela amesema utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia themanini huku akisema mwishoni mwa mwezi juni mradi huo utakuwa umekamilika

Diwani wa kata ya Kasanga Mhe Mh. Benson B. Msomba amewashukuru wadau kutoka shirika la CRS kwa namna ambavyo wanatekeleza ujenzi wa mradi wa maji katika kata ya Kasanga kwani kupitia mradi huo utapunguza uhitaji wa Maji kwenye kata ya Kasanga maana Kijiji cha Soweto kikipata maji maana yake uhitaji wa maji utabaki kwenye kijiji cha Mawelo

“Shukrani kubwa ni kwa Ziara yako wewe Mkuu wa wilaya ya Chunya na Uongozi ulio ongozana nao pamoja na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuweza kutubarikia mradi huu katika kijiji cha Soweto. Mradi huu utapunguza changamoto ya maji kwenye kijiji cha Soweto na najua baada ya kutatua hili kijiji cha Mawelo kitafuata. Mhe Mkuu wa wilaya tupelekee salamu zetu kwa Mhe Rais kwamba Wananchi wa Kata ya Kasanga wanakushukuru sana kumtua Mama Ndoo Kichwani”. Amesema Mhe Msomba

Kamati ya Ulinzi na usalama wakiambatana na viongozi kutoka Taasisi Mbalimbali wameanza rasmi ziara ya siku tatu kukagua miradi ya maji inayotekelezwa wilayani Chunya. Ziara hii kwa siku ya kwanza imehusisha kata ya Matundasi, Kata ya Kasanga na kata ya Chalangwa na ziara hiyo itaendelea tena kesho tarehe 29/05/2024 kuendelea kukagua utekelezaji wa Miradi ya maji wilayani Chunya

Diani wa kata ya Kasanga Mhe Benson Msomba akifafanua jambo mbele ya Kamati ya Usalama ya wilaya ya Chunya ilipotembelea mradi wa maji unaotekelezwa na CRS kwenye kijiji cha Soweto kata ya Kasanga


Meneja wa RUWASA wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya (Aliyevaa shati Nyeupe na ameshika karatasi Mkononi) akifafanua jambo mbele ya Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Batenga (Aliyavaa shati la drafti) wakati alipoongozana na kamati ya usalama ya wilaya kukagua mradi wa Maji Soweto

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Batenga (Aliyevaa shati la Drafti) akiwa sambamba na Mhe Diwani wa kata ya Kasanga Mhe Msomba mapema leo wakitembea kutoka eneo la mradi wa kisima cha Maji kilichochimbwa na CRS kwa lengo la kutatua Changamoto ya Maji katika kijiji cha Soweto kata ya Kasanga

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.