• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC BATENGA “NINA IMANI NA WADAU HAWAJAWAHI KUTUANGUSHA”.

Imewekwa: May 25th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe.Alhaj Mbaraka batenga amesema kuwa anaimani na wadau katika kuchangia shughuli mbalimbali za Maendeleo katika halmashauri ya Wilaya ya Chunya kwani wamekuwa wa kijitoa sana kwa hali na mali katika Sekta mbalimbali ikiwemo Michezo ambapo wadau hao walianza kushiriki tangu  ujenzi wa Uwanja wa Michezo ulipoanza  mwaka 2013

Kauli hiyo ameitoa tarehe 24/05/2024 wakati wa Harambee ya kuchangia Ujenzi wa Uwanja wa Mpira Wilaya ya Chunya iliyofanyika katika Ukumbi wa Omary City uliopo kata ya Itewe

“Mimi nina Imani sana na wadau hawa hawajawahi kutuangusha  katika shughuli mbalimbali za Maendeleo katika Wilaya yetu , tunatamani ifikapo mwezi wa nane Uwanja uwe umekamilika ili timu ziweze kuja  kucheza chunya  kwani tunataka kuileta Tanzania Chunya na Chunya tuipeleke Tanzania.alisema “Mhe. Batenga

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Zuberi Homera mgeni rasmi wa Hafla hiyo amesemakuwa   kunafaida nyingi timu zinapokuja kushiriki ligi katika viwanja vya Chunya kwani Wafanyabiashara  mbalimbali wa hotel , Mamalishe na wasafirishaji itakuwa ni fursa kwao kufanya biashara na kujipatia kipato  kwaajili ya kukuza uchumi wao pamoja na Halmashauri kujipatia mapato na hatimaye kukuza uchumi wa Chunya

“Uwepo wa timu kushiriki ligi kuu hapa watu wenye  magari mtafanya biashara  sana, watu wenye Hotel watu watalala hapa, Hotel zote zitajaaa lakini pia mama lishe nao watafanya biashara kwani  kunapokuwa na mechi watu wengi sana wanasafiri na timu  jambo ambalo litapelekea kukuza uchumi wa Chunya  na Halmashauri itajipatia mapato Chunya”alisema Mhe.Homera

Aidha Mhe Homera ameongeza kuwa  Timu mbalimbali zinapokuja kucheza ligi katika uwanja wa Chunya  itakuwa ni moja ya fursa ya kukuza uwekezaji pamoja na  kukuza utalii kutokana na ujio wa watu kutoka seheme tofauti tofauti hali ambayo itapelekea Wilaya ya Chunya  kuendelea kufanya vizuri katika kutekeleza ilani ya Chama cha mapinduzi kwa asilimia mia  katika maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na Michezo.

Akitoa Salama katika harambee ya kuchangia Ujenzi wa Uwanja wa Michezo Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi ndugu Noel Chiwanga ametoa rai kwa wadau kwendelea kuwa wazalendo kwa kumuunga Mkono Mkurugenzi wa Timu ya Kengold  ndugu Keneth Mwakyusa ili kwendeleza Michezo katika Wilaya ya Chunya kwani kwa kufanya hivyo italeta hamasa kwa wadau wengine kuunga Mkono  sekta ya Michezo.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ndugu Athumani Bamba amewashukuru Wadau kwa kwendelea kushirikiana na halmashauri katika shughuli mbalimbali za maendelao  katika shughuli mbalimbali za Maendeleo na kuwaomba  kuunga mkono jambo la Ujenzi wa Uwanja wa Michezo ili uwanja uweze kukamilika  na kutumika kwaajili ya michezo mbalimbali.


Harambee ya kuchangia Ujenzi wa Uwanja wa Michezo Wilaya ya Chunya imeongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Zuberi Homera ambapo michanho mbalimbali imeweza kutolewa na wadau  ikiwa ni pamoja na Mifuko ya Saruji 400, Mchanga roli 10, fedha taslimu Milioni 3,240,000/=  ahadi milioni 61,669,000/= pamoja na Kokoto zenye thamani ya shilingi milioni kumi (10,000,000/=) lengo ikiwa ni ukamilishaji wa Uwanja wa Michezo unaomilikiwa na Halmashauri ya wilaya ya Chunya

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe.Juma Zuberi Homera akizungumza na Wadau wa Soka pamoja na Wadau wa Maendeleo wakati wa Harambee ya Kuchangia Ujenzi wa Uwanja wa Michezo Wilaya ya Chunya  iliyofanyika katika Ukumbi wa Omary City uliopo kata ya Itewe.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi ndugu Noel Chiwanga akitoa Salam za Chama wakati wa harambee ya kuchangia Ujenzi wa Uwanja wa Michezo Wilaya ya Chunya  iliyofanyika katika Ukumbi wa Omary City .

Kaim Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ndugu Athumani Bamba akiwashukuru Wadau wa Maendeleo kwa kwendelea kujitoa kwa hali na mali katika shughuli mbalimbali za Maendeleo  hayo ameyasema wakati wa harambee ya kuchangia Ujenzi wa Uwanja wa Michezo.

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.