• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC BATENGA “MKURUGENZI HAKIKISHA KLABU ZOTE MASHULENI ZINAKUWA NA WALIMU WALEZI.

Imewekwa: February 24th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji Mhe. Mubarak Alhaji Batenga amemwagiza Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ndugu Tamim Kambona kuhakikisha Klabu zote zilizopo Mashuleni zinakuwa na walimu walezi pamoja na kuhakikisha wanajengewa uwezo ili waweze kuzisimamia vyema klabu hizo  ili klabu zitekeleze lengo lake ipasavyo.

Maagizo hayo ameyatoa  Februari 24/2023 Wakati wa Maadhimisho ya siku ya mwazilishi wa Skauti duniani ambapo Halmashauri ya wilaya ya Chunya yaliyofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari Kipoka kata ya Bwawani na Mkuu wa wilaya ya Chunya alikuwa Mgeni rasmi katika Maadhimisho hayo

“Natoa maelekezo kwa Mkurugenzi Mtendaji  kuhakikisha kwamba haya maeneo yote  yani klabu ya Skauti , klabu ya kupinga rushwa, klabu ya mali hai ,klabu ya lishe na Ukimwi klabu zote hizi zipate walimu walezi na ziwe na wanachama kuanzia Shule za Msingi hadi Sekondari  kwasababu huko  ndiko tunakoaanza kuwaandaa  na kuwajenga hawa vijana kuwa wazalendo kwaa Taifa lao “alisema Mhe.Batenga

Aidha Batenga aliongeza kuwa ni vizuri wanafunzi kujitafutia sifa za ziada wanapokuwa shule kwa kujiunga na klabu mbalimbali   ambazo zitawawezesha kujifunza mambo mengi yenye manufaa kwao na taifa kwa ujumla ikiwa ni pamoja na kuwajenga kuwa  wazalendo na  taifa lao ,watunzaji wa mazingira , wapinga rushwa  pamoja na mambo mengine lakini pia klabu zitawasaidia  katika maisha yao ya baadae kwenye soko la ajira.

“Sifa za ziada na  misingi ya  uzalendo  itajengwa  kupitia Skauti ,  kilabu za kupinga rusha , Lishe ,Ukimwi  na klabu  za  mali hai tunasema hawa ni wazalendo  kupitia matendo kwani uzalendo ni vitendo tukakupima uzalendo kupitia viashiria vya uzalendo  ambavyo tunaviangalia huku huku kwanye klabu zetu “alisema Mhe. Batenga

Wakiongea kwanyakati tofauti Afisa elimu Msingi mwalim John Gwimile na Afisa elimu Sekondari mwalim Hamis Mapoto wamewapongeza Skauti kwa kazi nzuri wanazozifanya ikiwa ni pamoja na kutunza mazingira kwa kupanda miti katika maeneo mbalimbali  ya Shule na kuwataka waitunze miti hiyo vizuri kwa kuhakikisha wanaimwagilia maji wakati wa kiangazi  ili miti hiyo iweze kustawi vizuri .

Akisoma risala kwa Mgeni rasmi kamishina wa Skauti Wilaya ya Chunya ndugu Joseph Kansato amesema kuwa katika  klabu yao ya skauti  wao kama wanachama wamekuwa wakifanya mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuandaa mafunzo kwa vijana katika makambi,kufanya usafi katika maeneo ya jamii, upandaji wa miti pamoja na kushiriki matukio mbalimbali ya kitaifa  kama vile Kukimbiza Mwenge na matukio mengine .

Kwa niaba ya wanachama wengine wa Skauti Crispa Obeth  kutoka Kipoka sekondari  kidato cha (II)na Gradness Mwakyembe darasa la (V) kutoka Shule ya Msingi Bwawani  wamesema kupitia Skauti wamejifunza mazoezi ya kujenga afya zao lakini pia wamejifunza kuwa wazalendo kwa Taifa lao jambo hilo huwasaidia kujua histoia ya Taifa lao na uzalengo wa viongozi waliotangulia

Maadhimisho ya mwazilishi wa Skauti duniani huazimishwa kila mwaka ifikapo 22 Februari  ambapo kitaifa kilele cha maadhimisho hayo  kimefanyika  tarehe 24 Februari  2024   ambapo Wilayani Chunya  wameadhimishwa kwa kupanda miti 300 katika maeneo ya Shule ya Sekondari Kipoka na kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni “Skauti mmoja mti mmoja”  

Mkuu wa Wilaya ya Chunya mhe.Alhaji Batenga katikati akiwa ameambatana na  Kaim Kamishina wa Skauti aliesimama upade wa kulia ndugi Ambakisye Mwambije wakielekea viwanja vya Shule ya Sekondari Kipoka

pamoja na wanachama waskauiti

Mhe.Batenga akizungumza na wanachama wa Skauti pamoja na maafisa mbalimbali wakati wa maadhimisho ya siku ya mwazilishi wa Skauti yalitoazimishwa ki Wilaya katika viwanja vya Shule ya Sekondari Kipoka.


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.