• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC BATENGA AMALIZANA NA WANANCHI WA SIMBALIVU

Imewekwa: October 18th, 2024

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mbaraka Alhaji Batenga amewataka wananchi wakitongoji cha Simbalivu na  Kijiji cha Itumba kuendelea kujiandikisha kwenye Daftari la Mkazi la Kitongoji ili waweze kupiga kura kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika tarehe Novemba 27, 2024 huku akiridhia ombi lao la kitongoji cha Simbalivu la kuendelea kubaki kijiji cha Itumba kilichopo kata ya Chalangwa

Akizungumza wakati wa Mkutano wake na wananchi wa kitongoji cha Simbalivu kilichopo kijiji cha Itumba kata ya Chalangwa mapema leo tarehe 18/10/2024 amesema Lengo la Serikali ni kuwaletea wananchi maendeleo hivyo amesema wananchi hao waendelee kujiandikisha kwenye daftari la mkazi la kitongoji na waendelee kuonekana kwenye kijiji cha Itumba kilichopo Kata ya Chalangwa tofauti na Ilivyokuwa hapo awali.

“Tunafahamu mbele yetu kuna zoezi la upigaji kura lakini kuna hatua za kujiandikisha lakini watu wote hawa hawajajiandikisha Je Mko tayari kujiandikisha leo? Hata sasa hivi uko tayari kujiandikisha? (Ndioooo) Nilikuja hapa tukafanya mkutano, mkaeleza mnahitaji nini (umeme, maji na mengine) na wataalamu wakafafanua kwamba kitongoji hiki kinapata umeme awamu hii na mtaalamu wa Maji alisema hapa tunakuja kuchimba maji bajeti ya 2024/2025, Sasa ili maendeleo hayo yafanyike lazima mjiandikishe ili tushirikiane na viongozi hao kuwaletea maendeleo. Tulichokubaliana ni kwamba mkajiandikishe na mtajiandikisha chini ya viongozi wa kitongoji cha simbalivu wakishirikiana na viongozi wa kijiji cha Itumba pamoja na viongozi wa Kata ya Chalangwa” Amesema Mhe Batenga

Kikao hicho cha Mkuu wa wilaya na wananchi kimekuja ikiwa ni siku moja baada ya wananchi kuzungumza na vyombo vya habari kugomea kitongoji hicho kuwekwa kata ya Sangambi Jambo ambalo limepelea kamati ya usalama kuitisha kikao cha Pande mbili yaani kata ya Sangambi na kata ya Chalangwa hatimaye kufikia maamuzi ya kuruhusu wananchi kujiandikisha na kusomeka kata ya Chalangwa

Ikumbukwe tarehe 16/09/2024 Serikali ilitangaza majina na mipaka ya vijiji na vitongoji, katika Tangazo hilo Kitongoji cha Simbalivu kilionekana kuwa sehemu ya Kijiji cha Sangambi jambo ambalo wananchi wa Kitongoji hawakubaliani nalo. Kamati ya usalama ikiongozwa na Mkuu wa wilaya imeridhia ombi lao na kuruhusu wajiandikishe kwenye kijiji cha Itumba, kata ya Chalangwa na Mpaka mchana wa saa tisa Kitongoji cha Simbalivu kimesajiri wakazi Zaidi ya 40 huku taarifa ya kijiji cha Itumba kwa ujumla itakujia baada ya Majumuisho saa kumi na mbili jioni baada ya vituo kufungwa.

Wananchi wa Kitongoji cha Simbalivu wakiwa kwenye mstari kuelekea kujiandikisha baada ya Kumalizana na Mkuu wa wilaya ya Chunya kuhusu Kitongoji hicho kusomeka Kijiji cha Itumba kilichopo kata ya Chalangwa, Tofauti na ilivyokuwa awali ambapo Kitongoji hicho kilisomeka kijiji cha Sangambi na kata ya Sangambi

Baadhi ya wananchi wakishangilia maamuzi ya Mkuu wa wilaya ya Chunya na wakiwa kwenye Mstari wakisubiria kujiandikisha kwenye Daftari la makazi la kitongoji

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Batenga akiongoza kikao cha viongozi wa Kata mbili yaani kata ya Sangambi na kata ya Chalangwa ili kufikia suluhu juu ya wapi hasa kitongoji cha Simbalivu kinapaswa kuwepo

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.