• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

CHILD SUPPORT TANZANIA YATOA MSAADA WA VITI MWENDO KWA WATOTO WENYEULEMAVU SHULE YA MSINGI KIBAONI.

Imewekwa: September 20th, 2022

SHIRIKA lisilo la kiserikali la Child Support Tanzania kwa kushirikiana na shirika la Christian Blind Mission wamekabidhi msaada wa baiskeli {Viti Mwendo} 5 za walemavu katika shule ya msingi Kibaoni halmashauri ya wilaya ya Chunya.

Msaada huo umelenga kuwawezesha wototo wenye ulemavu kuweza kukabiliana na changamoto zinazo wasababisha wasipate Elimu kwa ufasaha.

Akikabidhi msaada huo leo wenye thamani ya milioni 2.2 Mkurugenzi mtendaji wa Child support Tanzania Bi. Noelah Msuya amesema wao kama shirika wamejikita kuhakikisha watoto wenye ulemavu wanapata elimu katika mfumo wa Elimu jumuishi.

Amesema nia yao kubwa ni kuhakikisha wanaondoa vikwazo vinavyo wasababisha waototo wenye ulemavu wasipate elimu kwa ufasaha

“Nia yetu kubwa ni kuhakikisha kuwa watoto wetu wanapata elimu katika mazingira salama na yenye ubora” alisema Bi Noelah Msuya Mkurugenzi mtendaji wa CST.

Vile vile shirika la Child support Tanzania limekuwa likitoa elimu kwa makundi mbalimbali kuhusu ulinzi na  haki za watoto

Bi Noelah Msuya amewataka wazazi wanaopata elimu kuhusu haki za watoto kuhakisha wanaeple elimu hiyo kwa jamii ili kuhakikisha watoto wanakuwa katika mazingira salama .

Kwaupande wa Bw. Richard Dallu Program officer wa Christian blind mission Tanzania amesema wao lengo ni kuhakikisha jamii inakuwa jumuishi.

Tumekuwa tunafanya kazi na wadau mbalimbali wakiwamo CST kupitia hao wadau wanaenda kugusa maisha ya watoto hasa wenye  ulemavu

Pia ametumia fursa hiyo kuwahasa wazazi wa watoto waliopewa msaada wa viti mwendo kuhakikisha wana vitunza vizuri na kuendelea kuwasaidia watoto wao.

“Viti mwendo ambavyo tunawapatia tunaomba sana muweze kuvitunza ili viweze kuendelea kuwahudumia watoto vizuri” amesema Bw. Richard Dallu

Naye Afisa Elimu Maalum wa halmashauri ya wilaya ya Chunya Bi. Hawa Mtonyole amewashukuru shirika la Child support Tanzania kwa kushirikiana na Christian Blind Mission kwa msaada wa viti mwendo walivyotoa kwa watoto wenye ulemavu katika shule ya msingi kibaoni

Aidha ameyaomba mashirika hayo kuendelea kutoa misaada hiyo kwakuwa wahitaji bado ni wengi sana ndani ya  chunya na uhitaji wa viti mwendo ni mkubwa sana.

Sambamba na hayo Bi. Mtonyole ameiomba Serikali,wadau na taasisi mbalimbali zinazo wazunguka kuweze kusaidia kuboresha miundombinu ya shule ya msingi kibaoni ili iweze kuendana na kukidhi mahitaji ya Elimu Jumuishi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Child Support Tanzania Bi. Noelah Msuya akizungumza wakati wa utoaji wa msaada wa viti mwendo kwa wanafunzi wenye ulemavu shule ya msingi Kibaoni

  Afisa Elimu Maalumu wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Bi. Hawa G Mtonyole akizungumza wakati wa halfa ya utoaji wa msaada wa viti mwendo kwa wanafunzi wenye Ulemavu katika shule ya msingi kibaoni

Wawakilishi wa Child Support Tanzania, wawakilishi kutoka Christian Blind Mission wakiwa katika picha ya pamoja na Wanafunzi wenye ulemavu mara baada yakupewa msaada wa viti mwendo 

Ndugu Richard Dallu Program Officer wa shirika la Christian Blind Mission Tanzania akizungumza katika halfa ya utoaji wa msaada wa viti mwendo kwa wanafunzi wenye ulemavu katika shule ya msingi kibaoni

Ndugu Yusuph Libaba Mwenyekiti wa kamati ya shule ya Msingi Kibaoni akitoa neno la Shukrani kwa shirika la CST kwa msaada waliotoa wa viti mwendo kwa wanafunzi wenye ulemavu katika shule hiyo

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.