• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

CHUNYA YAJIPANGA KUSHIRIKISHA JAMII KUIBUA NA KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO

Imewekwa: September 29th, 2023

Halmashauri ya wilaya ya Chunya imejipanga kushirikisha jamii kuibua na miradi ya maendeleo yenye maslahi mapana kwa jamii jambo litakalo hakikishia ulinzi na usalama wa miradi hiyo kwani jamii yenyewe ndio itakayohusika kuanzisha miradi hiyo, kutekeleza mpaka ukamilishaji wake pamoja na kuilinda.


 Akizungumza leo 29/09/2023 kwa niaba ya Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya wakati akifunga mafunzo ya mfumo wa fursa na vikwazo kwa maendeleo ulioboreshwa (Opportunities and Obstacles for Development (O & OD)) ndugu Nebart Gavu amewataka washiriki kwenda kupeleka Elimu waliyoipata kwa wananchi ili wananchi moja kwa moja washiriki zoezi la kuibua miradi ya maendeleo yenye maslahi kwao na kuwashirikisha katika utelekezaji wa miradi hiyo huku akihimiza uwajibikaji na uwazi wa taarifa kwa kila hatua za utekelezaji wa miradi hiyo.


“Ndugu washiriki serikali imewaamini ninyi kuwa wawezeshaji wa mpango wa fursa na vikwazo kwa jamii na ni matumaini yetu mafunzo mliyoyapata yatawafikia wanajamii na yataleta mapinduzi chanya katika Maendeleo ya wanajamii. Pia Mafunzo haya yamewapa mwongozo ninyi wa namna sahihi ya kutekeleza majukumu yenu na namna sahihi ya kuishirikisha jamii katika miradi yote inayoibuliwa na kutekelezwa katika jamii na jambo muhimu ni ukweli na uwazi na uwajibikaji kwa kila hatua za mradi” alisema Ndugu Gavu


Aidha Ndugu Gavu amewataka washiriki wa mafunzo hayo kuendelea kutekeleza mkataba wa lishe kwakuwa suala la Lishe sasa ni jambo la kitaifa na amesema ili jamii iweze kushiriki kikamilifu katika uibuaji wa miradi pamoja na utekelezaji wa miradi hiyo ni lazima jamii hiyo iwe na afya njema hivyo lishe ina nafasi kubwa kwa jamii kushiriki kikamilifu katika suala la maendeleo.


“Suala la Lishe linaendelea na ni wimbo wa Taifa kwasasa hivyo endeleeni kutazama hilo na kutekeleza mkataka wa lishe na tunategemea mapinduzi makubwa katika maeneo mbalimbali mnayoyasimamia ikiwepo suala la Lishe”

Kwa niaba ya washiriki wote mtendaji wa kata ya Sangambi ndugu Mtundu Chapa ameshukuru serikali kuwapatia mafunzo hayo ambayo yana nafasi kubwa kusaidia utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku na ameahidi kwa niaba ya washiriki wenzake kwamba watayatendelea kazi mafunzo hayo ili kuhakikisha wananchi wanafaidika kwa uwepo wao katika vijiji na kata wanazotoka. Aliongeza Ndugu Gavu


Mafunzo hayo yaliyoshirikisha watendaji wa vijiji na kata, maafisa ugani na maafisa maendeleo ya jamii ambao jumla yao ni 92 yamehitimishwa rasmi leo tarehe 29/09/2023 kwa maafisa kutoka tarafa ya kiwanja kuhudhuri mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya (Sapanjo)

Paul Lugodisha (Aliyesimama Mbele kushoto) akiendelea na uwezeshaji wakati wa mafunzo ya Mfumo wa fursa na vikwazo ulioboresha katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya (Sapanjo), waliokaa ni washiriki wa mafunzo kutoka Tarafa ya kiwanja

Washiriki wa mafunzo wakiwa katika makundi ili kupima uelewa wa kile walichojifunza wakati wa mafunzo, baadhi ya waliosimama ni wakufunzi wa mafunzo hayo wakipitia kundi moja baada ya kundi lingine ili kuona washiriki wanavyoonesha uwezo wao juu ya kile walichojifunza

Mtendaji wa kata ya Makongolosi Ndugu Egithol Bilal (Aliyenyoosha Mkono kuielekea karatasi iliyoshikwa kikamilifu na washiriki wawili wa nafunzo) akielezea namna kundi lake lilivyotengeneza mpango kazi wa maendeleo kuzingatia ushirikishwaji wa jamii ikiwa ni kupima uelewa wa mafunzo waliyopatiwa mapema leo

Baadhi ya washiriki wa Mafunzo wakiendelea kufuatilia mafunzo kwa ukaribu na alyesimama nyuma yao ni moja kati ya wawezeshaji wakiendelea kuhakikisha washiriki wanapata kile kilichokusudiwa kwa uafasaha


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.