• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

CHUNYA WANAUME WAANZA KUJITOKEZA KUPELEKA WATOTO KUPATA CHANJO

Imewekwa: November 2nd, 2023

Kutokana na elimu, maelekezo na ushauri unaotolewa na wataalamu wa Afya wilayani Chunya, Wananchi wameendelea kujitokeza kwa wingi kupoata Chanjo ya polio awamu ya pili na hata ushiriki wao kwenye chanjo nyinginezo pamoja na mambo mengine ya afya yanayotekelezwa wilayani Chunya kupitia Wataalamu wa Afya wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya.


Chanjo ya Polio awamu ya pili inaendelea katika Mikoa ya nyanda za juu kusini kwa watoto walio chini ya miaka 8 ili kuwakinga na athari zinazoweza kujitokeza endapo ugonjwa wa polio utaikumba familia ambapo nje ya ulemavu kwa mtoto, madhara mengine yanweza kuwa ni kifo.


Ili lengo la serikali la kuwahudumia wananchi wake litimie lazima wananchi wa Chunya tuendelee kuhimizana sisi kwa sisi kwa mambo tunayoelekezwa na wataalamu wetu jambo litakalopelekea jamii kuwa salama na hatimaye kuendelea na shughuli za kila siku za uzalishaji mali.


Chanjo ya Polio awamu yapili inayolenga watoto wenye umri chini ya miaka nane (8) limeanza leo tarehe 2-5/11/2023 hivyo mwananchi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya hakikisha mtoto wako na hata mtoto wa jirani anapata chanjo hii maana ukimkinga mwanao tu na mtoto wa jirani ukamwacha bila kupata kinga bado mwanao yuko kwenye hatari ya kupata Ugonjwa huo kupitia kwa mtoto wa jirani ambaye atakuwa hajapata Chanjo ya Polio.


Kinga ni bora kuliko Tiba, wazazi tuendelee kutoa ushirikiano kwa wataalamu wanaopita kutoa chanjo hizo na pia tukumbushane kwamba Chanjo hizo ni bure na ni kwa usalama wa watoto wetu na jamii kwa ujumla.


Kauli mbiu inayoongoza zoezi la Chanjo ya Polio awamu ya Pili inasisitiza usalama wa watoto wetu “kila tone la Chanjo Humkinga Mtoto dhidi ya Ulemavu na Kifo, Mpeleke mtoto apate Chanjo”.


Tujifunze kidogo kuhusu Ugonjwa wa Polio

Polio ni Ugonjwa unaosababishwa na kirusi cha Polio, ambacho huenezwa kwa kula chakula na kunywa maji yaliyochafuliwa na kinyesi cha mtu mwenye maambukizi ya ugonjwa huo.


Ugonjwa huu unaweza kumpata mtu kwa kutozingatia kanuni za usafi na endapo mtoto mmoja atapata maambukizi, watoto wote watakuwa kwenye hatari ya kuambikizwa ugonjwa wa Polio.


Ugonjwa wa Polio hushambulia mishipa ya fahamu, na kusababisha kupooza kwa misuli hasa miguu, mikono au yote kwa pamoja na kwa wakati mwingine misuli ya kifua inayosaidia kupumua na kusababisha kifo.


Dalili za ugonjwa wa Polio ni pamoja na mgonjwa kuwa na homa kali, mafua, maumivu ya mwili, maumivu ya kichwa na shingo, ulemavu wa ghafla wa viungo.


Ifahamike kuwa, watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano, wapo kwenye hatari kubwa ya kuambukizwa ugonjwa wa Polio, ingawa unaweza kuwapata watu wa rika zote.


Ugonjwa wa Polio unaweza kuzuiwa kwa kupata chanjo ya kukinga ya Polio pamoja na kuzingatia usafi wa mikono, usafi wa mazingira ikiwemo matumizi sahihi ya choo bora.


Nchini Tanzania chanjo dhidi ya ugonjwa wa Polio hutolewa mara 4 kwa mtoto kwa nyakati zifuatazo, mara tuu mtoto anapozaliwa, afikishapo wiki 6, 10 na 14 na wakati wa kampeni maalum zitakapohitajika.


Ni muhimu mtoto kupata chanjo wakati wa Kampeni za chanjo za Kitaifa hata kama amekamilisha ratiba ya chanjo kwa utaratibu wa kliniki.

Hivi ndivo zoezi la Chanjo ya Polio awamu ya Pili likiendela Halmashauri ya wilaya ya Chunya, wazazi wanaendelea kushirkiana na wataalamu wa Afya kuhakikisha watoto chini ya Miaka nane (8) wanapata Chanjo kwa usalama wa watoto wenyewe na jamii kwa ujumla

Mtaalamu wa Afya akiendelea na zoezi la Chanjo katika Halmashauri ya wilaya ya Chunya lengo ikiwa ni kufikia watoto wote wenye umri tarajiwa (Chini ya miaka nane) bila kujali eneo la kijiografia na hata umbali wa eneo hilo kutoka makao makuu ya wilaya. kata ama kijiji, lazima watoto wote wafikiwe

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.