• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

CHUNYA WAITAKA NAFASI YA KWANZA KITAIFA UTEKELEZAJI MKATABA WA LISHE

Imewekwa: October 24th, 2023

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Dkt Darison Andrew kwa niaba ya Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya wilaya ya Chunya amesema lengo la Halmashauri ya wilaya ya Chunya ni kushika nafasi ya Kwanza kitaifa katika utekelezaji wa Mkataba wa Lishe ili kuendelea kuwahakikishia wananchi wa Chunya usalama wa afya ili waendelee kujihusisha na uzalishaji mali bila shaka yoyote.


Ametoa kauli hiyo leo tarehe 24/10/2023 wakati alipoongoza kikao cha Lishe kwa robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2023/2024 kilichoketi ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya uliopo jengo jipya la utawala kwa niaba ya Mkurugenzi mtendaji ambapo amewataka idara mbalimbali zilizo chini ya ofisi ya Mkurugenzi mtendaji kujipanga kwa namna zote ili kufanikisha azma hiyo.


“Matamanio yetu Halmashauri ya wilaya ya Chunya ni kushika nafasi ya kwanza Kitaifa katika utekelezaji wa mktaba wa Lishe hivyo lazima tujipange kuhakikisha  tunatimiza azma hiyo na ili tutumize azma hiyo lazima tushirikiane kwa pamoja kuanzia sisi mpaka mtu wa mwisho kabisa katika Mnyororo wa Lishe ambaye ni mwananchi”.


Aidha Dkt Andrew amewataka mafiasa Elimu Msingi na Sekondari kusimamia suala la Chakula shuleni kwani utoaji wa Chakula Shuleni ni agizo la Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mtu anayekaidi kuleta chakula shule ili watoto wapate chakula wawapo shuleni maana yake anakiuka maelekezo ya Rais hivyo achukuliwe hatua kali kwa mujibu wa Sheria.


Akitoa taarifa mbele ya Kikao hicho Afisa Lishe Halmashauri ya wilaya ya Chunya Bi Rehema Hiluka amemshukuru Mkurugenzi mtendaji kwa namna ambavyo amehakikisha fedha zote zilizopangwa kwaajili ya utekelezaji na usimamizi wa wa lishe zinatolewa kama bajeti inavyoelekeza na pesa hizo zinatolewa kwa wakati.


“Pamoja na kutoa taarifa za kikao cha tathimini ya mkataba wa lishe Kitaifa ambapo wilaya ya Chunya ilishika nafasi ya tatau kitaifa lakini naomba kipekee nikushukuru Mkurugenzi kwa namna ambavyo unahakikisha fedha zilizopangwa kwaajili ya kutekeleza mkataba wa Lishe zinatolewa na pia zinatolewa kwa wakati sahihi. Na kwa robo hii ya kwanza ya mwaka wa fedha 2023/2024 tumepokea fedha zaidi ya lengo ambapo tumepokea asilimia 126 ya fedha zilizotakiwa kwutekelezaji wa mkataba wa lishe kwa Robo hii ya kwanza ya mwaka”.


Kikao cha Lishe kimeketi leo tarehe 24/10/2023 ikiwa ni kikao cha Lishe kwa Robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2023/2024 na huwa kinakaa kila robo ya mwaka wa fedha kutamatika lengo ikiwa ni kutathimini mwenendo wa lishe kwa robo husika, kama kuna changamoto za utakelezaji wa mkataba wa lishe hutafutiwa suluhu katika vikao hivyo

Afisa Lishe wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Bi Rehema Hiluka akitoa taarifa wakati wa kikao cha Lishe kwa Robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2023/2024 kilichoketi leo ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya uliopo jengo jipya la utawala

Bi Komba akimuwakilisha Afisa Elimu sekondari akichangia namna ambavyo idara ya Elimu sekondari itakavyofanikisha suala la lishe kwa wanafunzi wa sekondari kwa Robo ya pili ya mwaka wa fedha 2023/2024 ili kufikia nafasi ya kwanza kitaifa kama ilivyo azma ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya

Dkt Benedict Matogo akichangia hoja kwenye kikao cha Lishe mapema leo namna ambavyo Divisheni ya kilimo itakavyoshiriki kuhakikisha wilaya ya Chunya inapata nafasi ya kwanza katika utekelezaji wa Mkata wa Lishe kitaifa

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.