• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

CHUNYA KUPOKEA FEDHA NYINGI KULIKO HALMASHAURI ZINGINE MKOA WA MBEYA KUTEKELEZA MIRADI YA WASH.

Imewekwa: June 8th, 2024

MKuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe.Juma Zuberi Homera amesema  Halmashauri ya Wilaya ya Chunya  ni Halmashauri pekee inayotaraji kupokea fedha nyingi zaidi za utekelezaji wa miradi ya WASH ukilinganisha na Halmashauri zingine za Mkoa wa Mbeya ambapo  itapokea zaidi ya shilling billion 1.3 ikiwa  ni  kutokana na usimamizi mzuri wa fedha za ujenzi wa miradi hiyo zilizotolewa awali.

Hayo ameyasema  tarehe 07/06/2024 wakati   akizungumza na Wananchi  kwenye Mkutano wa hadhara  baada ya kukagua Mradi wa ujenzi wa  miundombinu ya maji na vyoo bora (WASH)  Zahanati  ya Mbugani  iliyopo katika kijiji cha Mbugani.

“Mkoa wetu umepokea fedha nyingi sana zaidi ya bilioni 3 .3 kwaajili ya miradi hii ya WASH na Halmashauri ya Wilaya ya Chunya itapokea fedha nyingi zaidi ukilinganisha na Halmashauri zingine ambapo zaidi ya shilingi billion 1.3 zitapokelewa Chunya  kwahiyo niombe tu fedha hizo zisimamiwe vizuri kama mlivyosimamia hapa. Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kwakweli wametutoa kimasomaso wao wamefanya vizuri na mambo yanakwenda vizuri”alisema Homera

Aidha  ametoa rai kwa kila Halmashauri kuhakikisha inasimamia usafi wa mazingira  unaofanyika kila mwezi na kutaka kila kaya kufanya usafi katika maeneo yao ili kuweka mazingira safi na salama  ikiwa ni pamoja na kuhakikisha taka ngumu zinakusanywa pembezoni mwa barabara na maeneo yaliyotengwa kwaajili ya kuweka mazingira safi na kujikinga dhidi ya Magonjwa ya mlipuko.

“Taka ngumu zote ziwekwe pembezoni mwa barabara na maeneo yaliyoainishwa ili ziweze kuondolewa na timu ambazo zimeandaliwa kwaajili ya kutoa taka maeneo mbalimbali, Mji wa chunya ni mji ambao unavutia hivyo mtengeneze Mazingira wekeni vifaa vya kuwekea taka (dust bin) kwaajili ya kuweka takataka maeneo mbalimbali ili mtu akija anakuta mji wa Chunya uko safi, tuwe wa mfano kama tulivyokuwa wa mfano katika masuala ya Afya”.alisema Homera

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ambaye pia ni Diwani wa kata ya  Mhe.Bosco Mwanginde amemshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano waTanzania kwa namna anavyowajali wananchi kwa kuendelea kuleta fedha kwaajili ya kuboresha miundombinu mbalimbali ikiwepo  miundombinu ya Afya ambapo Zahanati ya Mbugani imeweza kuboreshewa miundombinu yake na kuwa Zahanati ya kisasa.

Mganga Mkuu wa Hospital ya Wilaya Dkt Darison Andrew akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa miundombinu ya maji na vyoo bora kwenye vituo vya Afya (WASH) amesema kuwa fedha zilizopokelwa ni  shilingi Million 63,233,000/=  na nguvu za wananchi zenye thamani ya shilingi Million 3,000,000/=  zimesaidia  ujenzi wa vyoo vya watoa huduma na wateja, ujenzi wa muindombinu ya maji  ujenzi wa tanki la  chini la kuhifadhi maji ( underground concrete tank) lenye uwezo wa kuhifadhi lita 30,000 ujenzi wa kichomea taka pamoja na Chumba cha kujifungulia.

Ziara ya kazi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Halmashauri ya Wilaya ya Chunya imekagua ujenzi wa Miundombinu ya maji, vyooo na miundombinu mingine katika zahanati ya kijiji cha Mbugani   pamoja na kuzungumza na wanachi kwenye Mkutano wa Hadhara katika Zahanati hiyo imeenda sambamba na   na kikao cha baraza la hoja za Mkaguzi kilichoketi katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Zuberi Homera (wa katikati aliye vaa suti nyeusi) wakati akikagua ujenzi wa mradi wa miundombinu ya maji na vyoo bora katika Zahanati ya kijiji cha Mbugani pomoja na wataalam mbalimbali kutoka ngazi ya Mkoa na Halmashauri ya Wilaya ya Chunya.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe.Juma Zuberi Homera akinawa mikono katika  moja ya miundombinu ya maji liyojengwa katika zahanati ya Mbugani kupitia mradi wa WASH wakati wa kukagua mrradi wa ujenzi wa miundombinu ya maji na vyoo bora Zahanati hapo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ambaye pia ni Diwani wa kata ya Mbugani Mhe. Bosco Mwanginde akitoa shukrani zake kwa Mhe.Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwajengea miundombinu ya maji na vyoo bora katika Zahanati ya kijiji cha Mbugani.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe.Juma Zuberi Homera akikagua tanki la  chini la kuhifadhia maji (underground concrete tank)lenye uwezo wa kuhifadhi lita 30,000 lililojengwa kupitia mradi wa WASH katika zahanati ya kijiji cha Mbugani


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.