• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

CHUNYA IMEVUKA LENGO KATIKA ZOEZI LA CHANJO YA SURUA RUBELLA

Imewekwa: February 18th, 2024

Halmashauri ya wilaya ya Chunya imetoa chanjo ya Surua Rubella kwa watoto 44,942 sawa na asilimia 116.37 wakati lengo lilikuwa kuwafikia watoto 38,619 na kwa takwimu hiyo Halmashauri ya wilaya ya Chunya imekuwa ni Halmashauri iliyochanja watoto wengi kuliko wilaya nyingine yoyote ya Mkoa wa Mbeya ukilinganisha na malengo yaliyokuwa yamewekwa awali

Akitoa taarifa ya zoezi la chanjo mratibu wa Huduma za Chanjo Halmashauri ya wilaya ya Chunya Blasio Kabwebwe amesema Halmashauri ya wilaya ya Chunya ni kati ya wilaya Ngumu kuwafikia wananchi katika maeneo yao kwani kutoka eneo moja kwenda eneo lingine kuna umbali mrefu lakini juhudi, kujituma na hata moyo wa uzalendo wa maafisa wanaohusika na zoezi la Chanjo ndiyo msingi wa kufikia lengo na hata kuvuka kiwango kama takwimu zinazoeleza

“Kuwafikia wananchi wa Chunya kwa kiwango hicho sio kazi ndogo maana wilaya ya Chunya inajulikana wazi kwa jiografia yake lakini lazima nipongeze kazi kubwa iliyofanywa na wataalamu ambao wamehusika katika zoezi la Chanjo, wamejituma sana na kwa moyo wa uzalendo na matokeo yake ndo hayo katika mkoa tumefanya vizuri kuliko wilaya nyingine” Amsema Kabwebwe

Aidha Kabwebwe ameshukuru uongozi mzuri na bora kutoka kwa Mganga Mkuu wa wilaya ya Chunya, Mkurugnezi mtendaji wa Halmashauri na viongozi wote ambao wameshiriki kwa namna moja ama nyingine kuhakikisha zoezi la Chanjo linafanikiwa kwa kiwango kikubwa kiasi cha wilaya ya Chunya karibu mara kadhaa sasa huwa tunaongoza mkoa wa Mbeya

“Lazima nitambue uongozi mahiri wa Mganga Mkuu wa wilaya ya Chunya Dr Drison Andrew katika zoezi hili, nitambue pia usimamizi wa Mkurugenzi mtendaji wilaya ya Chunya Ndugu Tamim kambona nna viongozi wengine wote kuanzia ngazi ya wilaya, kata, vijiji pamoja na wananchi kwa ujumla naweza kusema bila watu hao niliowataja na wengine ambao sijawataja ndio wamefanikisha zoezi hili kwa ukubwa huo” Aliongeza Kabwewe

Samweli Macha aliyekuwa kituo cha Mafyeko na Tumain Mbaba aliyekuwa kituo cha Mkola kwaniaba ya wataalamu wote waliohusika kwenye zoezi la Chanjo ya Surua Rubella wamesema zoezi limefanyika vizuri chini ya usimamizi mzuri wa viongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya, viongozi wa kata na Vijiji, huku wakisema wananchi wametoa ushirikiano mzuri ambao umepelekea kuvuka lengo lililokusudiwa

Zoezi la Chanjo ya Surua Rubella zimeendeshwa nchi nzima ambapo lilianza rasmi tarehe 15/2/2024 na kuhitimishwa leo tarehe 18/2/2024 na walengwa walikuwa watoto wenye umri wa miezi tisa 9 mpaka miezi 59 ambapo vituo vya kutolea huduma za afya na maeneo yaliyokubalika yalitumika kutoa chanjo huku wilaya ya Chunya Ikifanikiwa kufanya vizuri kwenye zoezi hilo kwa kuvuka lengo ambapo imewafikia watoto 44,942 kati ya watoto 38619 waliokusudiwa.

Tumain Mbaba (Afisa anayemchoma sindano mtoto) akiwa anaendelea kutekeleza jukumu lake leo tarehe 18/2/2024 katika kata ya Mkola wakati wa zaoezi la Chanjo ya Surua Rubella

Samwel Macha (Anaye mchoma mtoto Sindano) akiendelea kutekeleza jukumu la Chanjo ya Surua Rubella ikiwa ni siku ya mwisho leo tarehe 18/2/2024 katika kituo cha Mafyeko

Wanaume wilayani Chunya wamekuwa na mwamko katika kushiriki Chanjo mbalimbali ili kuhakikisha Familia wanazoziongoza zinakuwa salama, Picha hapo juu ni kati ya picha mbalimbali zinazoonesha namna ambavyo wanaume wamekuwa mstari wa mbele kupeleka watoto katika kupata chanjo

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.