• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

CHUNYA IMEUHESHIMISHA MKOA WA MBEYA SHIMISEMITA DODOMA

Imewekwa: October 28th, 2023

Halmashauri ya wilaya ya Chunya  timu ya wanaume kuvuta kamba imetinga FAINALI baada ya kuwapiga nje ndani wapinzani wote waliokutana nao kwenye Mashindano ya SHIMISEMITA yanayoendelea jiji Dododma ambapo moja ya vibonde wa Chunya ni timu kutoka Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaama maarufu kama Dar city council nao wamepigwa nje ndani.


 Safari bya Timu hiyo tangua hatua za awali imekutana na timu kutoka Halmashauri Mbalimbali na kuzichalaza bila Huruma kwa ushindi wa Mbili bila kwa kila timu waliyokutana nayo jambo linalofanya Chunya kuendelea kuwa na uhalali wa kuendelea kutetea Ubingwa huo kwa mashindano ya SHIMISEMITA mwaka 2023 ambayo yataraji kutamatika hivi punde.


Hebu fuatilia safari ya Chunya DC timu ya wanaume kuvuta Kamba mpaka kutinga Fainali.

Hatua ya Makundi    Mshindi CHUNYA DC alivuka hatua hiyo kwa kuwa mshindi wa kwanza kwenye kundi lake.

Hatua ya Kumi na sita Bora (Mtoano)   Moshi Dc Vs Chunya Dc   Mshindi CHUNYA DC

Hatua ya Robo Fainali        DAR CC    VS  Chunya DC             Mshindi CHUNYA DC

Hatua ya Nusu Fainali     Chunya DC vs muleba                      Mshindi CHUNYA DC

Sasa Fainali ni kesho           CHUNYA DC vs BARIADI DC  Je ni Chunya DC BINGWA? Tukutane kesho Jumapili tarehe 29/10/2023


Haya ni maneno ya kepteni timu ya kuvuta kamba wanaume Ridhiwani Mshighati  “Kabla ya mchezo wa leo tumekaa vikao kwaajili ya mikakati na tumekubaliana leo tunashinda na ni kweli tumeshinda, na  tunahakikisha tupumzika vya kutosha huku yeyote anayetoka kambini  ni kwa ruhusa maalumu na tukimaliza mchezo wa kesho ndipo watu waendelee na mambo mengine.

Mchezo Mgumu kuliko michezo yote ilikuwa ni kati yetu Chunya DC vs Dar CC, baada ya mchezo nimefuatilia takwimu kuna wakati raundi ya kwanza kamba ilisimama haiendi kwao wala kwetu kwa sekunde 48 jambo ambalo nafikiri halijawahi kutokea katika mashindano haya, tuliporejea raundi ya pili ndani ya sekunde kumi tu tulikuwa tumeshawashinda wapinzani wetu.

Lakini nashukuru sapoti kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya kupitia kwa afisa michezo wa mkoa kwani mara Mara amekuwa akitupigia simu, amekuwa akiuliza matokezo mbalimbali na amekuwa akituhamasisha na kutupa mbinu mbalimbali katika michezo mbali maana yeye pia ni mzoefu katika mambo ya michezo na ametuahidi kama tukifanya vizuri tunataraji kupokelewa na ofisi ya Mkuu wa Mkoa na kwetu sisi hii tunaona ni hamasa kubwa” Alisema Mshighati.


Kwa niaba ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Afisa Michezo wa Mkoa wa Mbeya Bwana Robert Mfugale amesema jambo walilolifanya Halmashauri ya wilaya ya Chunya kupitia uongozi wake kwa ujumla ni jambo la kuigwa huku akisema wametimiza wajibu wao vizuri maana kitendo cha Kusafirisha timu ya watu 35 kwenda Dododma kushirki Michezo inapswa kuigwa na Halmashauri zote zinazounda Mkoa wa Mbeya.


“Mimi kwanza nisema kwa maana ya Mkoa wa Mbeya tunaipongeza Halmashauri ya wilaya ya Chunya kwa maana ya uongozi wote wa Halmashauri kwa kuona umuhimu wa mashindano haya hatimaye kuruhusu timu ya watu 35 kusafiri kwenda kushiriki mashindano haya na kwa taarifa nilizonazo kati ya timu zilizosafiri kitajiri ni hii ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya kwani wamelipwa stahiki zao zote, na wamesafiri kwa Basi lao toka Chunya na basi hilo wanalo Dodoma linaendelea kuwazungusha viwanja vya mazoezi na kuwarudisha kambini yaani niseme Chunya wameuheshimisha Mkoa wa Mbeya huko Dododma.


Sisi kama Mkoa tunawapongeza sana viongozi wa Chunya kwa Kutimiza wajibu wao lakini pia tunawapongeza watumishi waliokwenda kushindana wametimiza pia wajibu wao. Na kwa taarifa nilizo nazo tayari tuna washindi wa tatu kwa timu ya wanawake kuvuta kamba, mshindi wa tatu kurusha tufe na tayari timu ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya imeingia Fainali kuvuta kamba wanaume. Sisi kama mkoa tukiona inafaa na ratiba ikaruhusu pande zote mbili basi tutawaalika wanaporudi wapitie hapa ili viongozi wawapongeze ndipo waendelee na safari ya kurejea Chunya”. Alisema Robert Mfugale.


Mwana Chunya, Mwana Mbeya Timu ya Halmashauri ya Chunya hata kama sio moja kwa moja,  inawakilisha Mkoa wa Mbeya kwenye Mashindano yanayoendelea Dodoma, Maandalizi yote yamekamilika lakini maombi yako wewe mwenye Mapenzi mema na Chunya na mwenye Mapenzi mema na Mkoa wa Mbeya iombee timu ya Chunya ichukue ubingwa tena.


Mpaka sasa Halmashauri ya wilaya ya Chunya imeshinda Mshindi wa tatu wanawake kuvuta kamba, nafasi ya Tatu Kurusha Tufe, Mdhindi wa kwanza kurusha tufe ametoka Mbeya (Rungwe) na sasa Chunya tuko Nusu Fainali mchezo wa Draft na Mvhezo wa Vukuta Kamba wanaume tutacheza Fainali kesho tarehe 29/10/2023 saa kumi na Mbili asubuhi.

Timu ya wanaume kuvuta kamba ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya ikiwa katika katika maandalizi ya kuwabuluza wapinzani wao huko SHIMISEMITA DODOMA

Timu ya wanawake kuvuta kamba ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya chini ya kepteni wake Devotha Mwasaga (Wa pili kutoka kushoto) wakisiliza maelekezo katika moja ya michezo yao huko Dodoma


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.