• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

CHUNYA IMEJIPANGA KUPAMBANA NA POLIO

Imewekwa: September 15th, 2023

Afisa utumishi na Rasimali watu wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu John Maholeni amewataka wajumbe wa kikao cha ya Afya Msingi wilani Chunya kutoa ushirikiano wa kutosha kwa wataalamu wa Afya katika mapambano ya Polio Jambo litrakalo leta ufanisi katika mapamano hayo


Ametoa kauli hiyo leo tarehe 15/09/2023 alipomuwakilisha Mkurugenzi mtendaji katika kikao cha ya Afya Msingi kilichoketi katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya uliopo jingo jipya la utawala la wilaya ya hiyo na kuhusisha wajumbe mbalimbali wakiwepo watendaji wa kata, viongozi wa dini, wataalamu wa Afya na wadau wengine


Naye Mganga mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Dr Darison Andrew amewataka wananchi wa wilaya ya Chunya kushirki kwa ukamilifu katika zoezi la Chanjo ya Polio inayotaraji kufanyika kuanzia tarehe 21-24 septemba 2023 ambapo vituo vyote 31 vya kutolea Chanjo vitahusika


 “Tunalo jukumu kwa pamoja kuhakikisha watoto chini ya miaka 8 wanapatiwa Chanjo kwani nao wako katika  hatari kubwa ya kupata Ugonjwa huo na Lengo letu ni kuhakikisha elimu kuhusu Ugonjwa wa polio na chanjo  inawafikia wananchi kikamilifu kwani ugonjwa huu hauna tiba bali unaweza kuzuilika kwa kupitia Chanjo na athari zake  kubwa kama vile kupooza, ulemavu wa kudumu na hata kufa”


Aidha Mganga Mkuu wa wilaya ya Chunya amewataka watendaji wa kata, viongozi wa dini pamoja na watoa huduma za afya kupambana na ugonjwa wa polio kwa Pamoja ili kuepuka athari zinazoweza kujitokeza kwa jamii yetu lakini amewataka watoa huduma za afya kuhakikisha Chanjo zote zinazotakiwa kwa mujibu wa Miongozo zinapatikana maeneo ya vituo vyao.


“Ni kazi yenu wataalamu wa Afya kuhakikisha chanjo zinazotakiwa kuwepo eneo la kituo chako zinakuwepo lakini pia kupitia kamati za afya ngazi za kata mpaka vijiji washirikishwe nao wasaidie kuhakikisha wananchi wanafika kupata huduma ya Chanjo”


Wajumbe wa kikao hicho wamejitokeza kuchangia ili kuboresha maeneo mbalimbali ili kuhakikisha zoezi linakuwa la mafanikio na linafikia lengo ambalo Serikali ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania linafikiwa na hatimaye wananchi wanakuwa salama kiafya na waendelee na uzalishaji mali


Kikao hicho kimehudhuriwa na kamati ya ulinzi na usalama, watendaji wa kata zote za wilaya ya Chunya, viongozi wa Dini zote yaani dini ya Kikristo na Dini Kiislamu, wahudumu wa Afya toka vituo vya kutolea huduma za afya na wajumbe mbalimbali wakiwepo Afisa usafirishaji, na wengine wengi

Mganga Mkuu wa wilaya ya Chuna Dr, Darison Andrew akifafanua jambo alipokuwa akifafanua umuhimu wa chanjo ya polia na namna ambavyo wilaya ya Chunya inatamani wajumbe wa kikao hicho wakashiriki katika mapambanoya polia wakati wa kikao 

Winfrida Mwakabonga Muuguzi msaidizi Zahanati ya Mazimbo akichangia mada wakati wa kikao 

Mratibu wa Huduma za Chanjo halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Blasio N. Kabwebwe akijibu baadhi ya hoja zilizotolewa wakati wa kikao mapema leo

Wajumbe wa kikao cha Afya ya Msingi wakifuatilia kwa makini wakatiMganga Mkuu wa wilayta ya akitoa ufafanuzi wa umuhimu wa kushiriki na kushirikisha watu wengine Chanjo ya Polia inayotaraji kufanyika tarehe 21-24/09/2023

Wajumbe wa kamati ya afya ya msini wakigawiwa vipeperushi na mabango yanayohimiza wananchi kila mmoja kwa nafasi yake kushiriki katika mapambanao ya Polia ambapo serikali inataraji kuratibu zoei la Chanjo kuanzia 21-24 september 2023

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.