• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

CHUNYA IMEDHAMILIA KUFANYA VIZURI NYANJA ZOTE, IKIWEPO MICHEZO

Imewekwa: April 5th, 2024

Halmashauri ya wilaya ya Chunya ikiwakilisha Mkoa wa Mbeya kwenye Mashindano ya Riadha yanayotambulika kwa jina la Twende Olympic yaliyofanyika mkoani Singida imeshika nafasi ya pili kwenye Mbio za Mita 1500, mita 400 na mita 100 ambapo wanafunzi washiriki kutoka ya Sekondari Sangambi waliwakilisha wanafunzi wengine katika Mashindano hayo

Mashindano hayo yamefanyika Mkoani Singida, viwanja vya Shule ya Sekondari Mwenge iliyopo manispaa ya Singida, na yamedumu kwa siku mbili kuanzia tarehe 4-5/4/2024 ambapo Mwanafunzi Joel Samwel amekuwa Mshindi wa pili kwenye mbio za mita 1500, Peter Joseph ameshika nafasi ya pili kwenye mbio za mita 400 wakati Salum Adam akishika nafasi ya pili kwenye mbio za mita 100 wanafunzi wote ni kutoka Shule ya Sekondari Sangambi iliyopo kata ya Sangambi katika Halmashauri ya wilaya ya Chunya.

Akitoa taarifa za mashindano hayo Kaimu afisa utamaduni na michezo wa wilaya ya Chunya Bi Hawa Mtonyole amesema vijana kutoka wilaya ya Chunya wamepambana sana kuhakikisha wanafanya kile walichoelekezwa na walimu wao wakati wa maandalizi ili kuhakikisha azma ya uongozi wa wilaya ya Chunya ya kufanya vizuri katika maeneo yote inatimia hata katika uga wa michezo

“Mashindano yalikuwa magumu sana ukizingatia mikoa ya Singida ni maarufu kwa riadha na katika mbio zote tulizoshiriki washindi wa kwanza wametoka mkoa wa Singida lakini kwa mazingira yetu kupata medali tatu na fedha shilingi laki mbili kwa kila mshindi sio haba hivyo lazima tuwapongeze vijana wetu wamefanya vizuri”. Alisema Mtonyole

Aidha kaimu afisa utamaduni na michezo wilaya ya Chunya ameshukuru uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya kwa namna ambavyo wanasimamia mambo mbalimbali jambo linalopelekea wao watumishi kujituma katika kutekeleza kila jambo linalowakabili ili kuhakikisha linakuwa na ufanisi mkubwa.

Naye afisa michezo Mkoa wa Mbeya Mwalimu Robert Mfugale amesema wilaya ya Chunya imechagiza medali tisa ambazo mkoa wa Mbeya umezipata kwani medali tatu kati ya medali tisa ambazo mkoa umepata zimetoka wilayani Chunya huku akisema kama Halmashauri bado kuna jukumu la kufanya kuhakikisha vipaji vya watoto vinalelewa vyema kutoka shule za msingi na Hatimaye shule za sekondari.

“Uwakilishi wa Chunya umechangia kuupaisha mkoa wa Mbeya kwani medali tatu toka Chunya imechangia katika medali tisa za mkoa wa mbeya, Kwenye sekondari lazima tuongeze usimamizi wa michezo kwani Shule za msingi wanafunzi wanafanya vizuri sana kwenye michezo ikiwepo riadha lakini wakifika sekondari wanapotea hivyo bado tuna kazi ya kufanya kuhakikisha tunaendelea kuwalea watoto ili waendelee kufanya vizuri wakifika sekondari. Pia kupitia michezo hii iwe fundisho kwetu ili kuandaa timu zetu kuelekea mashindano ya UMISETA” Amesema Mfugale

Msafara wa watu tisa (9) wanafunzi saba kutoka Shule ya Sekondari Sangambi, Mwalimu wa Michezo na Afisa Michezo wa wilaya wataungana na timu nzima kutoka mkoa wa Mbeya na kuanza safari ya kurudi mkoani Mbeya Kesho Jumamosi, na kwa mujibu wa afisa michezo wilaya Bi MtonyoleTimu hiyo itafikia Shule ya Sekondari Iyunga na Baadaye Jumapili itarejea wilayani Chunya wakiwa vifua Mbele vikipendezeshwa na medali za ushindi pamoja na kitita cha Fedha tasilimu Shilingi Laki mbili (200,000/=) kwa kila mshindi.

Ikumbukwe Chunya inafanya vizuri Maeneo mbalimbali ya utekelezaji wa majukumu yake ya kawaida, Ni lengo la Uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya kuhakikisha inaendelea kufanya vizuri maeneo mbalimbali bila kujali changamoto zinazojotokeza wakati wa utekelezaji wa jukumu lengo ikiwa ni kufikia ufanisi stahiki

Timu ya wanafunzi saba na Walimu wao kutoka Halmashauri ya wilaya ya Chunya wakiwa kwenye viwanja vya Michezo Mkoani Singida. (Kutoka Kushoto waliokaa Bi Hawa Mtonhole Kaimu Afisa Michezo na Utamaduni (Mwenye tisheti nyekundu), Mwalimu wa Michezo kutoka Shule ya Sekondari Sangambi Mwalim Philimon J Lulimo)

Mwanafunzi Joel Samwel (Mwenye Bukta ya Njano) akielekea kuhitimisha safari ya mbio ya Mita 1500 ambapo yeye alikuwa Mshindi wa Pili akiwakilisha Mkoa wa Mbeya

Timu ya Riadha kutoka Chunya ikiwa kwenye picha ya Pamoja baada ya kupokea medali tatu kutoka katika mbio za aina umbali tofauti ikiwepo mita 1500, mita 400 na mita 100

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.