• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

CCM WILAYA YA CHUNYA YAPONGEZA UJENZI WA KITUO CHA AFYA SANGAMBI

Imewekwa: February 24th, 2023

Kituo cha afya Sangambi kilichojengwa kwa fedha za mapato ya Ndani kitafunguliwa rasmi tarehe 1/4/2023 ili kuendelea kumrahisishia mwananchi wa Sangambi kupata huduma ya Afya kama ilivyo azma ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan.

Akitoa taarifa Mbele ya Kamati ya siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Chunya Afisa Elimu Kata ya Sangambi Mwalimu JOSEPH KIHWELE akimuwakilisha Afisa mtendeji kata hiyo ndugu Ntundu Chapa amesema kwasasa wako hatua za mwisho za kukamilisha matengenezo madogo madogo ambapo kufikia tarehe 1/4/2023 kituo kitaanza kufanya kazi

Mwalimu KIHWELE amesema wanaishukuru sana serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Dkt SAMIA SULUHU HASSAN kwa kuruhusu halmashauri kupitia makusanyo ya ndani kujenga vituo vya afya ambapo Kata ya Sangambi inakuwa ni kati ya kata za kwanza Tanzania kupata Faida hiyo lakini pia tunashukuru uongozi wa Halmashauri ya wilaya kutoa fedha hizo

“Tunashukuru serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM) inayoongozwa na Mhe. SAMIA SULUHU HASSAN Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uongozi bora pamoja na utoaji wa fedha kwaajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendelo katika halmashauri yetu. Pia tunaishukuru Halmashauri ya wilaya kwa kutoa fedha za ujenzi wa kituo hiki cha Afya kata ya Sangambi kwa Mwaka wa fedha 2022/2023”

Wajumbe wa kamati ya siasa ya Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Chunya iliyoongozwa na katibu wa chama hicho ndugu Charles Jokery kwanza wamepongeza serikali kuruhusu halmashauri kutumia fedha za mapato ya Ndani kujenga vituo vya afya na pia wamepongeza ofisi ya Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Tamimu Kambona aliyewakilishwa na Afisa Mipango Godfey Africa Mwakibinga kwa usimamizi mzuri wa mradi huo

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi akijumuisha maoni ya wajumbe wa kamati ya siasa amesema mradi huo umetekelezwa kwa viwango vikubwa na unastahili pongezi nyingi kwani katika kila eneo walilokagua wameridhishwa sana

“Kama kamati ya siasa tumepitia vituo vya afya karibu vinne na miradi mingine mingi lakini hakuna mradi uliofanywa vizuri kama mradi huu wa kituo cha Afya Sangambi, Hivyo nikupongeze mkurugenzi na timu yako kwa ujumla kwa kazi hii nzuri na njema”

Aidha katibu wa chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Chunya alimtaka Mkurugenzi kuhakikisha kituo kinaanza kutoa huduma kama ilivyokusudiwa ili kuwarahisishia wananchi upatikanaji wa huduma za afya ambapo kwasasa wananchi zaidi ya elfu kumi (10,000) wanaitgemea zahanati moja wakati huduma nyingine kubwa mpaka kituo cha Afya Chalangwa au Hospitali ya wilaya Chunya ambapo ni umbali wa zaidi ya Kilomita thelasini (30) kufikia vituo hivyo

Mradi huo unakadiliwa kugharimu fedha shilingi milioni mia sita (600,000,000/=) kati ya fedha hiyo milioni mia tano (500,000,000=) ni fedha za mapato ya ndani kutoka halmashauri ya wilaya ya Chunya wakati shilingi milioni mia moja (100,000,000/=) ni nguvu za wananchi.

Mpaka sasa mradi umegharimu shilingi milioni mia nne sabini (470,000,000/=) ambapo shilingi milioni mia nne ishirini na tatu (423,000,000/=) ni fedha kutoa mapato ya ndani ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya wakati Nguvu za wananchi zikigharimu milioni arobaini na saba (47,000,000)

Kamati ya siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Chunya iko katika ziara ya kawaida ya kukagua maendeleo ya miradi mbalimbali inayotekelezwa katika halmashauri ya wilaya ya Chunya kwa lengo la kujiridhisha kama miradi hiyo inathamani sawa na fedha ambazo serikali imeleta kujenga mirdi hiyo.

Muonekano wa Majengo katika kituo cha Afya Sangambi

Wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi wilaya ya Chunya wakiongozwa na Katibu wa CCM wilaya ya Chunya Ndugu Charles Jokery wa pili kutoka kushoto wakisikiliza taarifa ya ujenzi wa kituo cha Afya Sangambi

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.