• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

CCM WILAYA YAPONGEZA UJENZI WA VYUMBA YA MADARASA, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA

Imewekwa: December 22nd, 2021

Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Chunya ikiongozwa na Katibu wa Wilaya Ndg. Charles J. Seleman, imefanya ziara ya kukagua Miradi ya Ujenzi wa vyumba ya Madarasa unaotekelezwa chini ya Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO-19.

Katika ziara hiyo kamati imetembelea miradi 10 ya ujenzi wa vyumba ya madarasa katika shule za sekondari na vituo shikizi, miongoni mwa shule za sekondari zilizotembelewa ni pamoja na shule ya Sekondari Sangambi inayojengwa vyumba vya madarasa 11, Shule ya Sekondari Chokaa inayojengwa vyumba 2, Shule ya Sekondari Itewe yenye ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa, Ujenzi wa vyumba 2 Shule ya Sekondari Makalla, Ujenzi wa vyumba 7 katika Shule ya Sekondari Kipoka na Maradi wa vyumba 3 katika sekondari ya Makongolosi.

Aidha kamati imetembelea Ujenzi wa Vyumba vya Madarasa katika vituo shikizi, miongoni mwa vituo vilivyotembelewa ni Kituo Shikizi cha Mpaliji chenye ujenzi wa vyumba 2, kituo shikizi cha Mererani chenye ujenzi wa vyumba 4, Kituo shikizi cha Kalungu chenye ujenzi wa vyumba 3, pamoja na Kituo shikizi cha Machinjioni chenye ujenzi wa vyumba 5 vya madarasa.

Akizungumza kwa niaba ya Mweyekiti wa CCM Wilaya, Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya Ndg. Charles Seleman, ameupongeza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kwa usimamizi mzuri wa miradi ya ujenzi wa vyumba ya madarasa unaotekelezwa chini ya Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO-19.

Baadhi ya wajumbe wa kamati ya siasa wilaya walisema utekelezaji wa ujenzi wa vyumba vya madarasa unakwenda vizuri na kuutaka uongozi wa Halmashauri kuongeza kasi zaidi ili kukamilisha ujenzi wa vyumba kwa madarasa yaliyobaki.

Naye Mbunge wa Jimbo la Lupa - Chunya, Mh.Masache Njelu Kasaka ameupongeza uongozi wa Halmashauri kwa usimamizi mzuri wa fedha pamoja na kazi nzuri ya ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa fedha za UVIKO-19.

“Sisi leo tumekuja kama Kamati ya Siasa ya Chama CCM Wilaya tumeridhika na utekelezaji wa miradi hii ya ujenzi wa vyumba vya madarasa kwani majengo haya yanaakisi fedha zilizotolewa, sisi kama wilaya tumeridhika na tulichokiona”.

Wajumbe wa Kamati ya Siasa Chama Cha Mpinduzi [CCM] wilaya ya Chunya Wakikagua Mradi wa Ujenzi wa vyumba vya Madarasa Shule ya Sekondari Kipoka

Wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi CCM pamoja na Wataalamu wa Halmashauri ya wilaya ya Mbeya wakiendelea na Ukaguzi wa Miradi ya Ujenzi wa vyumba ya Madarasa unaotekelezwa chini ya Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO-19.

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.