• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

BI. MWAKISOLE " TUSIWABAGUE WATOTO KATIKA MALEZI"

Imewekwa: March 9th, 2023

Mwenyekiti wa umoja wa wanawake kupitia chama Cha Mapinduzi wilaya ya Chunya Bi .Ezelina Anyosisye Mwakasole amewataka wanawake wilayani Chunya kutowatenga watoto wakati wanapowalea kwani kufanya hivyo kunasababisha uonezi, ukandamizwaji kwa Watoto

Ameyasema hayo Jana tarehe 8 Machi 2023 katika maadhimisho ya siku ya wanawake wilayani Chunya

"Mnapowapangia kazi watoto muwapangie kwa usawa ikiwa ni kuchota maji mtoto wa kike na Wa kiume wote wakachote maji, ikiwa ni majukumu yanayohusu kupika Kuosha vyombo wote wafanye shughuli hizo kwanza kuwafundisha kazi wote bila kujali jinsia

Aidha Bi Mwakisole amewataka wanawake kuongeza juhudi katika mapambano dhidi ya virusi vya UKIMWI kwani wameweza katika mapambano mengine mengi na wamefanikiwa katika mapambano hayo hivyo wakiamua wanaweza kutokomeza janga la UKIMWI

“Hebu tupige vita Sasa ukimwi usiendelee kututesatesa, Kama tumeweza kupambana kwenye Mambo mengine ikiwepo usawa katika Elimu, ajira na mambo mengine hivyo hata kwenye mapambano ya maambukizi tupambane ili tuepukane na maambukizi ya UKIMWI”

Katika hafla hiyo Mgeni Rasmi ametunuku vyeti vya pongezi kwa vikundi mbalimbali vya wajasiliamali wilayani Chunya ambavyo vimeweza kurejesha mikopo waliyokopeshwa na Halmashauri hiyo kwa uaminifu huku wanachama wa vikundi hivyo wakikiri wazi kwamba mikopo hiyo imewasaidia  kujikwamua kiuchumi. Vikundi vilivyotunukiwa vyeti ni pamoja na Kikundi cha Utulivu, Kikundi cha Wanawake katikati ya mji, Kikundi cha Umoja, Kikundi cha Star women na vingine.

Kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi afisa maendeleo ya Jamii wilaya ya Chunya ndugu Vincent Msolaa akimuwakilisha Mkurugenzi mtendaji  Halmashauri ya wilaya ya Chunya ndugu Tamimu Kambona amesema halmashauri ya wilaya ya Chunya Itaendelea kutoa mikopo kwa mujibu wa miongozo ya serikali kwa vikundi mbalimbali vya wanawake ili kuinua uchumi wao huku akisema zaidi ya shilingi milioni mia moja na arobaini (140) zimetolewa kwa vikundi vya wanawake wilayani Chunya

Msolla amewataka wanawake wilayani Chunya Kuchukua tahadhari ya vitendo vya Ushoga vinavyotokana na mmomonyoko wa maadili huku akiwakumbusha kuhakikisha wanawadhibiti watoto kutoangalia katika mitandao mbalimbali ya kijamii na televisheni mbalimbali mambo ambayo sio mweleko wa maadili yetu Tanzania.

Oliver Mtandi ambaye ni mkaguzi msaidizi Jeshi la Polisi wilayani Chunya amewata wanawake kuwa imara katika kuhakikisha maadili yanalindwa kwani Mama anayo nafasi kubwa sana katika malezi na makuzi ya Mtoto kwani mmonyoko wa maadili unaonekana sasa inasabibishwa na wanawake kutokusimamia vizuri nafasi zao. Kwa upande wa jeshi la polisi amesema wamejipanga kushirikiana na wananchi hivyo amewataka kutoa taarifa pale wanapoona uvunjifu wa amani unajitokeza


“mwanamke ni mjenzi wa kwanza wa familia yake, ndiye mlinzi wa kwanza wa familia yake, sisi wanawake tunaweza kujenga nyumba zetu na tunaweza kubomoa nyumba zetu kwani maandiko yamezungumza wazi. Jeshi la polisi tuko tayari kushirikiana na wananchi hivyo toeni taarifa pale unapoona ukatili unafanyika

Awali akisoma Risala mbele ya Mgeni rasmi, Mwenyekiti wa Kampeni ya kupinga ukatili  inayojulikana kama Shujaa wa maendeleo na ustawi wa Jamii Tanzania (SMAUJATA) Bi Tunsume Kibweja amesema wilayani Chunya wanawake bado wanapambana na ukatili mkubwa katika maeneo mbalimbali ikiwepo ukatili wa kiuchumi

“Katika wilaya yetu wanwake wengi wanakosa fursa za kushirki katika biashara jambo linalosababisha baba peke yake kutegemewa kwa kila kitu, lakini wanawake wanayimwa haki ya kupata elimu na hata kumiliki maliza”

Bi Kibweja amesema pia maambukizi ya UKIMWI wilayani Chunya ni makubwa kwa wanawake ukilinganisha na wanaume na hii ni kutokana na wanawake kukosa nguvu ya kuamua ni muda gani hata kuingia katika mahusiano au kutokuingia katika mahusiano lakini pia maambukizi mengine husababishwa na ukatili wa kingono ambao unafanywa kwa wanawake

Diwani wa kata ya Matundasi ilyoko Mamlaka ya mji mdogo wa Makongolosi wilayani Chunya Mhe Kimo Choga amewashukuru watu wote waliohudhuria katika maadhimisho hayo huku akisema wanawake ni msingi wa maendeleo kwenye kata ya matundasi hivyo amewataka wanaume kuwaunga mkono wake zao katika kuhakikisha maendeleo katika ngazi ya familia, jamii na hatimaye TAIFA kwa ujumla

"Nawaomba wanaume wenzangu tuunge mkono jitihada za wake zetu (Wanawake) ili kuhakikisha tunapata maendeleo kwenye familia zetu na Mimi nitahakikisha nahimiza wanaume kuendelea kupinga ukatili kwa wanawake na ikiwezekana tuachane na Nyumba zetu za kando" amesema Mhe Choga

Maadhimisho ya siku ya mwanamke duniani katika wilaya ya Chunya yamefanyika katika kata ya Matundasi ambapo kauli mbiu ya maadhimisho hayo ikiwa ni “Ubunifu na Mabadiliko ya kiteknolojia: Chachu katika kuleta usawa wa kijinsia” yamehudhuliwa na viongozi mbalimba wa serikali na taasisi binafsi ili kupaza sauti pamoja na Mwanamke ili hatimaye nia ya serikali ya awamu ya sita ya kumkomboa mwananchi wake katika Nyanja mbalimbali inatimia

Afisa Maendeleo ya Jamii wilaya ya Chunya Ndugu Vincent Msolla akizungumza mbele wa watu katika Madhimisho ya siku ya Mwanamke

Meza kuu wakifuatilia burudani mbalimbali zilizokuwa zikitumbuiza

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.