• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

Amy Holdings Kunufaisha wakulima wa tumbaku Lupa

Imewekwa: June 30th, 2022

Mkurugenzi wa kampuni ya tumbaku ya Amy Holdings, Ahmed Mansoor Huwel ambaye pia ni mnunuzi wa tumbaku kupitia kampuni yake tanzu ya Mkwawa Leaf ameahidi kuboresha maslahi ya wakulima wa zao hilo.

Huwel ameyasema hayo jana Wilayani Chunya wakati wa utambulisho wa kampuni yake ya Amy Holdings kwa wananchi wa kata ya Lupa, utambulisho uliofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mh Juma Homera.

“Tumekuja hapa kwa nia njema hatujaja hapa kunyang’anya tumbaku ya mtu, kwa msiojua Philip ni rafiki yangu na tunajuana nae sana tumemsaidia Philip toka mwanzo alivyofungua kampuni ya Premium,” alisema Huwel.

Huwel aliongeza kwa kusema wao kama Amy Holdings wamekuja na sera tofauti na sera mpya kwani hawajaja Lupa kunyang’anya ama kuiba tumbaku wa mtu.

Vilevile Huwel aliongeza kwa kusema anaamini kuwa na ushindani ni afya, kwani kunapokuwa na ushindani kunakuwa na afya kwa wakulima wengi.

Aidha, alisema kuwa lengo la kuinunua kampuni hiyo ni kuwasaidia watanzania ili kuwanyanyua kiuchumi.

“Shida kubwa waliyopitia wakulima wa Tanzania ndio hasa iliyonisukuma mimi kuweza kununua hii kampuni ya TLTC ili niweze kuwasaidia na kuwakomboa wakulima wenzetu wa nyumbani.” Amesema Huwel

“Niwahakikishie wakulima wote wa Tanzania wakiwepo wa hapa Lupa nimekuja kuwasaidia sijaja kuwanyang’anya wala sijaja kuwaibia nia yetu ni njema sana.” Aliongeza Huwel.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh. Juma Homera amesema wao kama mkoa wanahitaji kuwe na Ushindani, kusuwepo na mtu mmoja ambaye atatawala soko.

“Tukasema kwamba hebu tulete ushindani, tuwe na kampuni zaidi ya moja, tunashukuru Waziri wa Kilimo, tunanshukuru sana ametuletea kampuni mpya ya Amy Holdings ambayo inanunua Tabora na maeneo mengine.” Alisema Homera.

Pia homera amewataka wakulima kuhakikisha wanatoa ushirikiano kwa wanunuzi wote, aliyopo kwa sasa Premium na mnunuzi mpya ambaye ni Amy Holdings

“Mimi hapa nimekuja kutambulisha makubaliano ni ya kwenu wenyewe mnataka mumuuzie, mnataka kufanya nini ni nyinyi wenyewe.” Alisema Homera

Vilevile amewaasa wakulima ambao tayari wameshaingia mikataba na Kampuni ya Premium kutovunja mikataba hiyo bali washirikiane nao kwani wamekuwa nao kwenye shida na raha.

“Kama kuna tumbaku imezidi na una uwezo wa kuuza kwa kampuni nyingine nenda kauze, maana mkataba si tani elfu nne na zipo tani elfu nne mia tano, mia tano hizo si gombania goli kila mmoja anaweza kuzichukua?

“Lakini msivunje mikataba mkalaza madeni mkamkimbia Premium mkaenda kwa kampuni nyingine, nendeni kwa step (hatua) kama mzigo upo wa kutosha unaweza kufanya option (chaguo) ya kwenda kwa mwingine lakini kama mzigo upo limit (idadi maalum) usihame kubalianeni na mkataba wenu malizaneni naye.

“Najua kwa changamoto hii huku kuna Premium huku kuna Amy Holdings bei lazima itachangamka sisi tutakuwa tunashangilia tu, nawajua Premium wananunua Mpanda, nimekaa nao hii Mbeya nimekaa nao na nipo nao lakini lazima tulete kampuni nyingi zaidi ili bei iwe nzuri kwa wananchi.” Alisema Homera

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh Juma Homera akizungumza na Wananchi wa Kata ya Lupa wakati wa Kutambulisha Kampuni Mpaya ya Ununuzi wa Tumbaku wilayani Chunya.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Amy Holdings Campany Limited Ndg. Ahmed Huwel Akiwa kwenye Mkutano wa kutambulishwa kwa kampuni yake ya Ununuzi wa Tumbaku kwa Wananchi wa Kata ya Lupa

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.