• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

FURSA ZA UWEKEZAJI CHUNYA

Start Date: 2017-03-28
End Date: 2017-03-30

 

UTANGULIZI:
Wilaya ya Chunya inafursa mbalimbali za uwekezaji katika sekta za madini, kilimo, mazao ya misitu na nyuki, Utalii na Mali Asili, Pia bidhaa mbali mbali kutoka kwa wajasiriamali ambazo ni pamoja ni Asali ya nyuki wakubiwa na wadogo, mafuta ya Alizeti, bidhaa mbalimbali za mbao(Samani) , watu wote mnakaribishwa kuchangamkia fursa hizi za uwekezaji.

UCHIMBAJI WA MADINI:
Wilaya ya Chunya inautajiri mkubwa wa dhahabu na shughuli za uchimbaji na uwekezaji zilianza zamani kabla hata ya uhuru wa Tanganyika, wawekezaji wakubwa na wadogo wanaendelea na shughuli za uwekezaji katika maeneo mbalimbali ya wilaya na hivyo kuchangia katika kutoa ajira na mapato kwa serikali na Halmashauri..

   Yapo maeneo maalum yaliyotengwa kwaajili ya wachimbaji wakubwa, kati na wadogo hivyo wawekezaji wa ngazi zote mnakaribishwa kuja kuwekeza


     KILIMO        

Asilimia 87 ya wakazi wa wilaya ya Chunya wanategemea kilimo na kilimo ndiyo huchangia kwa kiwango kikubwa sana uchumi wa Wilaya

 Wilaya inakadiriwa kuwa na jumla ya eneo lenye ukubwa wa hekta 1,315,000 ambapo eneo linalofaa kwa kilimo linakadiriwa kuwa ni hekta 1,035,400 na jumla ya hekta 79,072 ndizo zilizotumika kwa kilimo cha mazao ya chakula, biashara na bustani (mboga na matunda)..

 Wilaya ina wastani wa joto kati ya nyuzi za sentigredi 21 na 23. Wilaya hii hupata aina moja ya mvua (Unimodal rainfall pattern) yenye wastani kati ya milimita 500 na 1000 kwa mwaka. Msimu wa mvua huanzia mwishoni mwa mwezi Oktoba hadi Aprili na kipindi chenye mvua nyingi ni kati ya mwezi Januari na Machi.. Yapo pia maeneo yanayofaa kwa kilimo cha umwagiliaji hivyo wawekezaji wanakaribishwa sana.

.Mazao mbali mbali ya chakula na bishara yanastawi vizuri ndani ya wilaya ambayo ni pamoja na Mahindi, Maharage, Mtama, Karanga, Viazi vitamu, Ulezi, Mihogo, Alizeti, Tumbaku,  Kunde, Choroko, Mihogo, Viazi vitamu na ulezi.

MALIASILI NA UTALII
Wilaya ya chunya ni moja kati ya maeneo yaliyosheheni Rasilimali maalum na  muhimu  kwa utalii . Maliasili zilizosheheni mtawanyiko wa mimea , Msitu na Wanyamapori mbalimbali zikiwemo sehemu zenye mambo ya kale, kihistoria, Chemichemi za maji moto na maumbile ya kuvutia ya Milima na miinuko yenye uoto wa asili.

FURSA ZA UTALII
Biashara ya uwindishaji kitalii inafanyika Chunya kama njia ya uvunaji endelevu wa wanyamapori, kuna uwepo wa wanyama pori karibia wote wa BIG 5 isipouwa kifaru, kuna TWIGA MWEUPE kama mnyama wa kipekee ktk ikolojia ya hifadhi ya majini ya Chunya-Rungwa na hifadhi ya Taifa ya Ruaha.

 kuna uoto Pekee uliosheheni misitu ya miombo na mininga , milima ya kihistoria  na matambiko  mf. Ml. Mwene).
   
 Chunya inapitiwa na barabara ya kihistoria ya kutoka kaskazini mwa Afrika mji wa Cairo hadi kusini mji wa Cape Town, Afrika kusini.(The Great North Road). Chunya imeunganishwa na barabara ya lami kwenda uwanja wa kisasa wa Songwe International Airport. .
                               

UFUGAJI WA NYUKI

Wilaya ya Chunya ni mojawapo ya Wilaya zinazozalisha Asali na Nta kwa wingi Tanzania. Uoto wa asili wa miti aina ya Miombo ambayo ni malisho ya Nyuki na hali ya hewa inachangia sana katika shughuli za uzalishaji. Uwepo wa aina mbalimbali wa miti ya miombo inayochanua kwa misimu tofauti husaidia upatikanaji wa chakula cha nyuki kwa mwaka mzima. Wilaya ya Chunya inazalisha sana Asali ya Nyuki Wakubwa na Wadogo pamoja na Nta. Wastani wa uzalishaji wa asali kwa mwaka ni tani 408.54 na Nta ni tani 25.2. Kuna fursa nyingi za uwekezaji katika sekta ya Nyuki Wilayani Chunya kama Kuanzisha manzuki (Appiary), kuuza vifaa vya U nyuki kama vile Mizinga ya Kisasa, vifaa vya kuchakatia, mavazi ya kinga na Kuanzisha viwanda vya kuchakatia mazao ya nyuki.


 FURSA ZAIDI ZA UWEKEZAJI

Maeneo ya uwekezaji yaliyopo katika wilaya ya chunya ni saba (7) yenye jumla ya ekari 2758.86, Tunakaribisha wawekezaji wazawa na wa kigeni ili kuwekeza katika wilaya yetu. Maeneo hayo yapo kiwanja, itewe, makongolosi, kibaoni, mbugani, sinjilili, na lupa ambayo yanapatikana katika tarafa zote mbili za kiwanja na kipembawe

Fursa za uwekezaji zilizopo katika wilaya ya chunya ni kwenye viwanda na biashara. Viwanda vifuatavyo vinaweza kuwekezwa.

  • Kiwanda cha kukamulia Alizeti
  • Kiwanda cha kuchakata Mazao ya Nyuki
  • Kiwanda cha kutengeneza Samani mbalimbali.
  • Kuwekeza kwenye Utalii; Uwindaji wa kitalii, Utalii wa kiutamaduni mf. Mlima Mwene n.k
  • Maeneo ya Malisho ya mifugo na kuchakata Nyama.
  • Kuanzisha Mashamba makubwa ya Matunda mf. Maembe na viwanda vya usindikaji
  • Kuanzisha kituo cha mafunzo ya Ujasiriamali wadogo katika sekta ya madini na kujenga viwada vya kuchakata madini



Matangazo

  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, HALMASHAURI YA CHUNYA December 14, 2022
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • RC HOMERA AIPONGEZA WILAYA YA CHUNYA KUFANYA VIZURI KATIKA SEKTA YA MADINI

    March 18, 2023
  • DKT KILUSWA “HAKUNA SABABU YA KUTOROSHA MADINI”

    March 15, 2023
  • RC HOMERA "CHUNYA ITAKUWA NI WILAYA YA UCHUMI MKUBWA MKOANI MBEYA"

    March 12, 2023
  • DC MAYEKA “POLENI WAKULIMA WA TUMBAKU, …SASA TUKATE BIMA”

    March 10, 2023
  • Zaidi

Video

NAIBU WAZIRI WA MADINI DKT KILUSWA AFUNGUA MAONESHO YA KWANZA YA TEKNOLOJIA YA MADINI CHUNYA.
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.