• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

ZIARA YA MHE. WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII WILAYA YA CHUNYA.

Imewekwa: July 3rd, 2018

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Hamis Kigwangala akiongozana na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Amos Makalla amefanya ziara ya kikazi katika wilaya ya Chunya ambapo aliwasili

Makao Makuu ya wilaya na kupokewa na Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe. Rehema Madusa, kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya,

viongozi wa Chama Tawala, Mwenyekiti wa Halmashauri, Mkurugenzi wa Halmashauri, pamoja na wakuu wa idara mbalimbali za

serikali kuu na Halmashauri. Punde baada ya kuwasili Mkuu wa wilaya ya Chunya alimkaribisha na kisha kumsomea taarifa fupi

ya wilaya ambapo  kubwa zaidi aligusia juu uvamizi wa wanachi katika maeneo ya hifadhi na kugusia kuwa operesheni zilianza

tangu zamani akitolea mfano mwaka 2013 na 2015 zilifanyika operesheni za kuwaondoa wavamizi hao, lakini maeneo hayo bado

yanaendelea kuvamiwa akitolea mfano msitu wa hifadhi wa TFS wa kipembawe wenye hekta takribani 6000.Pia juhudi zimeendelea

kufanyika na Serikali ya Wilaya ya sasa kwani  nayo imeendesha Operesheni ya kuwaondoa wavamizi na kufanikiwa kwa kiasi

kikubwa.  akigusia pia vitalu viwili chini ya wilaya vya Piti East na Chunya west amabavyo navyo vimevamiwa, Pia

aliendelea kusema kuwa wakati wa operesheni za kuawaondoa wavamizi mali nyingi ziliweza kukamatwa ikiwemo na magogo

yaliyokutwa ndani ya msitu wa hifadhi kinyume cha sheria na taratibu.

 alipopewa nafasi ya kuongea Mhe. Waziri alianza kwa kumshukuru Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh. Amos Makalla kwa kumpokea vizuri

tangu alipoingia katika mkoa wake na kusema lengo la ziara hii ni kufuatilia na kusimamia utekelezaji wa sera mbalimbali

za Maliasili, akaendela kuleza kuwa Maliasili ni za nchi nasiyo za wizara ya Maliasili na wao kama wizara ni waangalizi tuu.

aliendelea kueleza kuwa Serikali ya wilaya inamamlaka ya kusimamia utekelezaji wa sheria katika eneo husika. akigusia

suala la uhifadhi wa msitu wa Patamela Mhe. waziri alisema wao kama wizara wamepewa msitu bila kujali umepitia kwenye

wilaya gani na akamshukuru Mhe. Mkuu wa Mkoa kwa kuweza kushughulikia mgogoro uliojitokeza na kuumaliza. aliendelea

kugusia kuwa majangili wanaishi na wananchi hususani kwenye vijiji vinavyozunguka mapori ya akiba hivyo kuiomba serikali ya wilaya kuongeza juhudi.

Katika ziara hiyo Mhe. Waziri alipata pia fursa ya kukagua uvamizi uliofanyika katika Msitu wa hifadhi wa serikali kuu wa
Itengu kata ya kibaoni, ambapo aliweza kubaini uharibifu wa mazingira, uchimbaji wa madini kinyume na taratibu pamoja
makazi yalijengwa kiholela.
  Ziara hiyo ilihitimishwa kwa kufanya mkutano wa hadhara katika kata ya mwaoga ambapo Mhe. Waziri alianza kwa kusikiliza
kero za wananchi ambazo nyingi ya kero zilikuwa ni juu wawekezaji kujitwalia maeneo makubwa na wananchi kukosa sehemu za
uchimbaji, pamoja na mkanganyiko unaotokea wananchi wanapokamatwa ndani ya msitu wa hifadhi na kwenda kufunguliwa mashtaka
wilaya jirani ya Songwe. kero ambazo hazikuwa chini ya wizara ya Maliasili moja kwa moja na kumpa nafasi Mhe. Mkuu wa Mkoa
kuzitolea maelezo, Mbali na kujizotela maelezo kero hizo aliahidi kuwa atamleta waziri wa Madini ili nae aje atoe majibu na
dukuduku la wananchi.
  Akiwahutubia wananchi katika kata ya Mwaoga Mhe. Waziri alianza kwa kusema jukumu alilopewa la uwaziri ni gumu na kamwe
hakulifurahia pindi alipoteuliwa bali alimshukuru Mungu kwani Maliasili ni uhai wa nchi, na kutokana na utunzaji wa
maliasili unapata maji, chakula, umeme n.k. aliendelea kusisitiza na ninanukuu "Misitu ya hifadhi ni hifadhi, Wizara ya
Maliasili inatetea Misitu na Wanyamapori na ukikamatwa ndani ya hifadhi utachukuliwa hatua kali kama jangili mwingine tu"
mwisho wa kunukuu. Pia Mhe. waziri alimpa nafasi Mkurugenzi wa Huduma za Misitu (TFS) ili atoe taratibu za wananchi
kuchimba ndani ya hifadhi ambaye alisistiza kuwa ili uweze kuchimba ndani ya hifadhi mwananchi ahakikishe anapata leseni
kutoka wizara ya Madini, na kwamba lazima kwanza tathmini ya uharibifu wa mazingira ifanyike ili kubaini athari na
kutafuta njia ya kudhibiti. aliongeza ukikutwa unachimba bila vibali mali zako zitataifishwa na kufikishwa kwenye vyombo
vya Dola.


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.