• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

ZIARA YA MHE. MKUU WA WILAYA YA CHUNYA REHEMA MADUSA KATIKA KATA YA MATUNDASI KUKAGUA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI YA MATUNDASI.

Imewekwa: January 17th, 2018

Katika ziara hiyo Mh.Mkuu wa Wilaya aliambatana na Mkurugenzi Mtendaji wilaya ya chunya Bi. Sophia Kumbuli, Kamati yake ya ulinzi na Usalama, , Afisa madini (W)Mhandisi  (W) pamoja na Afisa Elimu Sekondari (W).

Lengo hasa la ziara ya Mheshimiwa mkuu wa Wilaya ni:

1.    Kufanya kikao kifupi na uongozi wa Sunshine Mining juu ya ujenzi wa maabara katika shule ya sekondari Matundasi

2.    Kufika katika shule ya sekondari Matundasi kuona ilipofikia katika ujenzi wa maabara,madarasa na nyumba ya walimu.

3.    Kufanya kikao na wananchi wa Kata ya Matundasi


Mh.Mkuu wa wilaya alianza kwa kuonana na uongozi wa mgodi wa Sunshine ambao ndio wanaojenga maabara katika shule hiyo ya Matundasi kama sehemu ya kurejesha sehemu ya faida kwa jamii. Katika kikao kifupi cha ndani na uongozi wa Sunshine mining, Mh.Madusa aliomba uongozi wa mgodi huo kufanya haraka kukamilisha ujenzi wa maabara mbili ambazo wameshapauwa na aliwaambia ni vizuri ikiwa tayari ndani ya miezi miwili kuanzia leo tarehe 11/01/2018 pamoja na changamoto mbalimbali walizoeleza. Uongozi wa Sunshine Mining waliahidi kufanya kama ilivyoombwa na Mh.Mkuu wa wilaya.

                                                                          
Mh. Rehema Madusa (wa pili kutoka kulia) na Mkurugenzi Mtendaji Bi. Sophia Kumbuli (Wa kwanza kushoto) wakiwa ndani ya moja ya maabara katika shule ya Sekondari Matundasi pamoja na uongozi wa Sunshine Mining.


Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya alimalizia ziara yake kwa kufanya Mkutano na wanachi wa Kata ya Matundasi .Katika Mkutano huo Mheshimiwa Diwani(Kimo J.Choga) alimpongeza Mkuu wa wilaya na Mkurugenzi mtendaji kwa uchapaji kazi wao mzuri, Pia Mh.Diwani alisema wana miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo inaendelea, iliyokamilika na mengine ipo kwenye mipango ikiwa ni pamoja na ujenzi wa Zahati Itumbi ambayo Sunshine wataijenga na kupauwa lakini umaliziaji mwingine utafanywa na wananchi.

                                                                           

                                                                                      Mkuu wa Wilaya akizungumza na wanachi.

                                                                           

Mh.Rehema Madusa(mwenye miwani), Mkurugenzi Mtendaji kushoto kwake Bi. Sophia Kumbuli wakisikiliza kero za wananchi.  
Kulia kwa Mkuu wa wilaya ni Mh.Diwani kata ya Matundasi na Mwenyekiti  wa mtaa  “A”

Mkurugenzi Mtendaji alipata pia nafasi ya kuongea na wananchi ambapo aliwaeleza vigezo vya shule kusajiliwa na kuruhusiwa kuchukua wanafunzi . Vigezo hivyo ni

  • Lazima iwe na maabara tatu zilizokamilika za masomo ya fizikia,Bayolojia na Kemia
  • Maktaba
  • Ukumbi wa mikutano.
  • Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya aliendesha harambee ya papo kwa hapo kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa shule ya sekondari  Matundasi. Katika harambee hiyo fedha taslimu Tsh.169,000 na ahadi jumla ya Tsh. 6,151,000 zilitolewa, Pia Mh.Mkuu wa Wilaya aliahidi vifaa vya Ujenzi: Bati 300, na saruji mifuko 173.

                                                                        

                                                                            Baadhi ya wananchi wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya

                                                                          

                                                                          Ulipofikia ujenzi Jengo la Utawala Shule ya sekondari Matundasi

                                                                          

                                                                              Ulipofikia Ujenzi wa Majengo ya Maabara katika Shule ya Sekondari Matundasi           

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.