• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

Watendaji wa kata Chunya wapatiwa mafunzo ya TEHAMA, utawala na usimamizi wa rasilimali

Imewekwa: May 20th, 2022

WATENDAJI wa Kata za Halmashauri ya Wilaya ya Chunya wamepatiwa mafunzo na Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kupitia mradi wa PS3+ uliofadhiliwa na watu wa Marekani.

Mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo watendaji hao katika nyanja za tenkolojia ya mawasiliano (TEHAMA), usimamizi wa rasilimali, utawala bora pamoja na ushirikishwaji wa wananchi.

Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo, David Olelaput ambaye ni mratibu wa PS3+ Nyanda za juu Kusini alisema, mradi wa PS3+ umelenga kusaidia katika maeneo hayo ili kuleta tija katika jamii.

"Kwa kifupi leo hii tupo hapa kusapoti kwenye eneo la ushirikishwaji wa wananchi na utawala bora." Alisema Olelaput.

Naye Mataalam wa kamati ya Mkoa Mamlaka ya Serikali za Mitaa Bw. Nazar Sola amesema, mradi wa PS3+ unashirikiana na Serikali kuimarisha Mfumo wa Utawala bora kwenye Halmashauri.

"Lakini baada ya kufanya kazi hii kwa miaka kadha tumeona mambo hayatendeki kama tulivyotarajia, tumekuwa na majadiliano na TAMISEMI kwamba ni kwanini masuala ya Utawala bora hasa masuala ya ushirikishwaji wa wananchi hayafanyiki, mbao za matangazo na masanduku ya maoni hayafanyi kazi, mkutano watu hawahudhurii na bado taarifa toka kwenye vijiji zinaandikwa na kupelekwa Halmashauri.

"Wewe kama Mkurugenzi wa kata kazi yako ni kuratibu shughuli zinazofanyika kwenye kata yako, lengo la haya mafunzo ni kukumbushana juu ya uimarishaji wa mifumo ya utawala bora na ushirikishwaji wa wananchi." Alisema Sola.

Akifunga mafunzo hayo, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya Bw. Alex Batwel amewataka watendaji wa kata kuhakikisha yale yote waliyojifunza kwa siku mbili wanakwenda kuyafanyia kazi na kuleta tija na manufaa kwenye maeneo yao ya kazi na Halmashauri kwa ujulma.

"Utawala bora ni mpana sana, mmejifunza namna ya kuzingatia ufuataji wa taratibu na sheria zinazowaongoza kwenye ngazi zenu za kata, pia mmejifunza juu ya majukumu yenu, mipaka yenu na mahusiano kwenye taasisi zinazopatikana kwenye kata zenu.

“Nina imani haya mafunzo mliyoyapata yataenda kuboresha kile mlichokuwa mnakifanya aidha kwa mazoea au kwa kufuata utaratibu, mkaenda kufanya kikawa kizuri zaidi.” Alisema Batwel.

"Mkawasimamie watendaji wa vijiji, wenyeviti wa vitongoji kuhakikisha wanasoma taarifa za mapato na matumizi, waitishe mikutano mikuu kwa mujibu wa sheria.

“Mkienda kusimamia hayo ndio mwisho wa siku tunasema utawala bora na ushirikishwaji wa wananchi unazingatiwa." Alisisitiza Batwel.

Katika mafunzo hayo watendaji wa kata wamejengewa uwezo dhidi ya utawala bora ikilenga namna ya uendeshaji wa vikao, uandishi wa muhtasari wa vikao, ushirikishwaji wa wananchi katika kuandaa bajeti, kusomewa mapato na matumizi, matumizi ya mbao za matangazo pamoja na tovuti ya halmashauri ikiwa ni jukwaa la kutolea taarifa za maendeleo katika maeneo yao.

Mtaalamu wa Kamati ya Mkoa Mamlaka ya Serikali za Mitaa Bw. Nazar Sola akifafanua malengo ya Mradi wa PS3+ kwa washiriki walio Udhuria Mafunzo ya Utawala bora na Usimamizi wa Rasilimali

Mratibu wa PS3+ Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndg. Simon Mbella akiwasilisha mada ya Utawala bora na Ushirikishwaji wa wananchi kwa Watendaji wa kata 

Watendaji wa kata Wakiwa kwenye Mafunzo ya Utawala Utawala Bora na Ushirikishwaji wa Wananchi yaliyo tolewa na PS3+ kwa kushirikiana na Serikali katika Ukumbi wa mikutano wa halmashauri

Afisa Tehama Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndg Happygod Mollel akiwasilisha mada inayohusu Tovuti ya Halmashauri kwa Washiriki wa Mafunzo ya PS3+ katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri

Afisa Mipango Wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndg Nerbart Gavu akiwasilisha mada ya O & OD iliyoboreshwa kwa Watendaji wa kata walioshiriki mafunzo ya Utawala bora yaliyotolewa na PS3+ kwa kushirikiana na Serikali

Watendaji wa kata wakiwa kwenye mafunzo kwa vitendo wakijifunza Mfumo wa MUKI 

Mtaalamu wa Kamati ya Mkoa Mamlaka ya Serikali za Mitaa Bw. Nazar Sola akimwelekeza Mtendaji wa kata ya Makongolosi jinsi ya Kutumia Mfumo wa MUKI

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.