• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

WANAUME JITOKEZENI MNAPOFANYIWA UKATILI

Imewekwa: July 27th, 2023

Afisa ustawi wa Jamii wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Nashi Mwalende amewataka wanaume wilayani Chunya kuacha kasumba na kuogopa bali wajitokeze katika ofisi za Ustawi wa Jamii  ili kupata msaada pale wanapofanyiwa ukatili wa namna yoyote ile kuliko kujichukulia maamuzi ambayo baadaye yanakuja kuwa ni kinyume na sheria jambo ambalo linagharimu maisha yao na  familia kwa ujumla


Akizungumza tarehe 25/7/2025 ndani ya studio za Redio Baraka ambapo Maafisa kutokaofisi za ustawi wa Jamii na Idara ya Maendeleo ya Jamii wilaya ya Chunya   waliungana kutoa elimu ya ukatili ambapo Ndugu Mwalende, amesema ofisi za ustawi wa jamii wilaya ya Chunya ziko tayari kupokea wanaume wote na kuwahudumia huku akisema wapo maafisa wanaume ambao wanaweza kuwahudumia watu  wanaotaka kuhudumiwa na afisa wa kiume


“Wanaume tunawaomba sana wajitokeze madawati yetu yako huru  waondoe ile dhana kwamba wanawake wakienda ustawi wa jamii wanapendelewa kuliko wanaume sisi tutawahudumia wote kwa usawa kabisa, Tumekuwa tunapita maeneo mbalimbali kwenye vijiji wanaume wenyewe wameshuhudia kwamba nao wanafanyiwa ukatili jambo muhimu wajitokeze katika ofisi za ustawi wa jamii na kama wanaona shida kufika wanaweza kutupigia  simu na kama bado wanaweza kuona shaka kwetu waende polisi dawati la jinsia”


Naye Afisa Mendeleo ya Jamii Nasra Hassan Mkupete ametaja aina mbalimbali za ukatili ikiwa ni pamoja na ukatili wa kiuchumi  ambao unawakumba jinsi zote  huku akisema wanaume wamekuwa wagumu sana kujitokeza kueleza na kutafuta msaada pindi wanapofanyiwa ukatili jambo linalopelekea wanaume wengi kuwa na msongo wa mawazo na wakati mwingine kutenda mambo ambayo kama wangejitokeza kutafuta msaada wasingefanya maamuzi ya namna hiyo


“Aina ya kwanza ni ukatili wa kimwili ambao husababisha madhara kwa mwili, ukatili wa kingono ambao mara nyingi hutokea kwa watoto wa kike, ukatili wa kisaikolojia ambao huathiri moyo, hisia na aina nyingine ya ukatili ni ukatili wa kiuchumi ambao hufanyiwa wanaume na wanawake lakini wanaume wengi huwa hawatoi taarifa kamili wanapofanyiwa ukatili”


Naye Groria Amandi Kavishe kutoka ofisi ya Maendeleo ya jamii wilaya ya Chunya amesema jamii inaweza kupata madhara mbalimbali kutokana na ukatili wa kijinsia hivyo jamii haina budi kupambana na ukatili wa aina yoyote ile ili kuhakikisha jamii inakuwa salama kwa manufaa ya jamii yenyewe na Taifa kwa ujumla.


“Pia kuna madhara yanaweza kutokea kutokana na ukatili mfano mtu anaweza kufa , umaskini ambao unaweza kutokea kutokana na mtu kuzuiwa kufanya kazi na mumewe jambo linaloweza kupelekea umaskini, msongo wa mawazo na madhara mengine mengi”


Maafisa hao wamefika Redio Baraka ili kutoa Elimu  ya ukatili wa kijinsia kwa wananchi ikiwa ni mwendelezo wa juhudi za kuhakikisha Jamii inaepukana na ukatili wa namna mbalimbali nakuwa na  jamii  salama huku shughuli za kujipatia kipato zikiendelea jambo ambalo litapelekea jamii kujikomboa kiuchumi

Nashi Mwalende afisa ustawi wa jamii akifafanua jambo walipokuwa Mubashara Redio Braka kutoa elimu ya Ukatili

Nasra Hassan Mkupete akieleza Jambo pindi Maafisa Maendeleo ya Jamii na Maafisa ustawi wa Jamii wilaya ya Chunya walipokuwa Mbashara Redio Baraka Kutoa elimu ya ukatili

Groaria Amandi Kavishe akiwa Mubashara Redio Baraka Maafisa toka wilaya ya Chunya walipofika kutoa elimu ya Ukatili

Maafisa  kutoka wilaya ya Chunya katika Picha ya Pamoja ndani ya Studio za kurusha Matangazo za Redio Baraka baada ya kutamatisha Zoezi la uelimishaji Jamii kuhusu Ukatili kupitia Redio Baraka. Aliyekaa ni Frank Philip Mwandishi na Mtangazaji wa kipindi, aliyesimama kuanzia Kulia ni Nashi Mwalende kutoka ustawi wa Jamii, katikati ni Groria Kavishe na anayemalizia ni Nasra Hassan kutoka Idara ya Maendeleo ya Jamii

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.