• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

WANANCHI WANA MATUMAINI MAKUBWA SANA NA NINYI.

Imewekwa: December 9th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe. Mbaraka Alhaji Batenga amesema kuwa Wananchi wana matumaini makubwa sana na Wenyeviti wa vijiji,Vitongoji na Wajumbe wa serikali za vijiji ambao wamewachagua wao wenyewe kwa kuwapigia kura katika uchaguzi wa serikali za mitaa Novemba 27/2024.

 Kauli hiyo ameitoa leo Disemba 9/2024 wakati wa Mafunzo kwa wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji na Wajumbe wa serikali za vijiji yaliyofanyika katika Ukumbi wa  mikutano wa Sapanjo Halmashauri ya Wilaya ya Chunya.

“Wananchi wana matumaini makubwa sana na ninyi  ,wamewaamini  ,wakaja kwenye kampeni wakawapigia  kura kuwachagua , msiende kuweka mikono mbele baada ya wananchi kuwapa dhamana  hii, kwasababu ridhaa ya kuongoza kwenu kumetokana na wananchi na hao ndio waajiri wenu, mkawaheshimu” amesema Mhe.Batenga

Mhe Batemga ameongeza kuwa mafunzo kwa wenyeviti wa Vijiji , Vitongoji na Wajumbe wa serikali z a Vijiji yamelenga kuwapa nyenzo na kuwajengea uwezo ili  waweze kujua majukum  yao na namna ya  kwenda kuyatekeleza kwani  kwa kufanya hivyo itawasaidia kujenga Imani kwa Wananchi waliowaamini na kuwachagua

Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ndugu Charles Jokery ametoa  rai kwa viongozi hao wa Vijiji,Vitongoji na Wajumbe wa serikali za Vijiji kwenda kuwatumukia wananchi badala ya kuwa kero kwa wananchi kwani chama hakitasita kuwachukulia hatua wale wote watakao kuwa kero kwa Wananchi

“ Viongozi wa Vijiji  na Vitongoji mmechaguliwa kwenda kuwatumikia wananchi na sio kwenda kuwalarua wananchi ,nendeni mkatatue kero za wananchi na sio kuongeza kero kwa wananchi ,  kumekuwa na tabia ya watu  baada ya kuchaguliwa  manakuwa kero na tishio kwa wananchi hiyo siyo dhamira ya chama cha Mapinduzi “ amesema Jokery

  Naye katibu wa chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema  ndugu Yohana Mpamba amewaasa viongozi wa Vijiji, Vitongoji na wajumbe wa serikali za Vijiji kufanya  kazi kwa uadilifu kwa kuzingatia misingi yote ya haki, sheria na taratibu za nchi zinavyosema kwani  wao ndio waliobeba dhamana ya kuwatumikia wananchi katika maeneo yao .

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chuya ndugu Cuthberth  Mwinuka  amewataka Viongozi wa vijiji kwenda  kuhimiza wananchi kulima vizuri na kuyatunza mazao hayo  kwani wakilima vizuri kijiji kitaepuka na  janga la njaa  lakini pia wataweza kuuza ziada ya mazao  yao  kwaajili ya  kujipatia mahitaji mengine .

“Himizeni wananchi walime kwasababu ukijenga uchumi wa kijiji ndio maendeleo ya Kijiji, mimi sitarajii kuja kumuomba Mhe. Mkuu wa Wilaya aniletee mahindi kwaajili ya kusambaza kwa wananchi kwaajili ya njaa, chakula tunacholima ni chakutosha , tuhifadhi na ziada tuuze pasipo kusababisha njaa ndani ya familia. “ amesema Mwinuka

Wakizungumza kwa niaba ya viongozi wengine walipaota mafunzo  wakati wa semina kwa  Vijiji , Vitongoji na wajumbe wa serikali za vijiji   Bi Rukia Mwakyusa ,Titho Kitema  wamesema kuwa mafunzo waliyoyapata yana umuhimu mkubwa sana kwao kwani yamewasaidia kujua mipaka yao  pamoja na majukumu yao na mambo mbalimbali ya kwenda kuwaelimisha wananchi katika maeneo yao

Mafunzo kwa wenyeviti wa Vijiji , Vitongoji na wajumbe wa serikali za vijiji yamefanyika  kwa makundi mawili  kundi la kwanza ilikuwa tarafa ya Kipembawe  Tarehe 8/12/2024 na kundi la pili Tarafa ya Kiwanja  Tarehe 9/12/2024 yameenda sambamba na kuadhimisha  miaka 63 ya Uhuru wa Tanganyika

Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe. Mbaraka Alhaj Batenga akiongea juu ya matumaini waliyonayo wananchi kwa Viongozi wa Vijiji, Vitongoji na wajumbe wa serikali za vijiji wakati wa Mafunzo kwa Viongozi hao yaliyoenda sambamba na kuadhimisha miaka 63 ya Uhuru wa Tanganyika.

Katibu wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Chunya ndugu Charles Jokery akitoa salam za Chama wakati wa mafunzo ya Viongozi wapya wa Vijiji,Vitongoji na wajumbe wa serikali za vijiji yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri wa Sapanjo  


Kaim Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ndugu Cuthberth Mwinuka akiwataka Viongozi wa Vijiji, Vitongoji na wajumbe wa serikali za Vijiji akiwasisitiza viongozi hao kuwahimiza wananchi waokulima vizuri ili waweze kupata mavuno mengi

Afisa Utumishi Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ndugu Moses Ngole akifundisha juu ya majukum ya wenyeviti wa Vijiji,Vitingoji na wajumbe wa serikali za Vijiji wakati wa mafunzo yaliyofanyika kwa Viongozi wa Tarafa ya Kiwanja

Viongozi wa Vijiji, Vitongoji,na wajumbe wa serikali za vijiji wakiendelea kufuatilia mafunzo juu ya mada mbalimbali zilizofundishwa kwaajili ya kuwasaidia  katika kutekeleza majukum yao






Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.