• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

WANAKIJIJI WAJITOLEA ZAIDI YA MILIONI 16 ILI KUJENGA ZAHANATI

Imewekwa: January 15th, 2024

Makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mhe Ramadhan Shumbi amewata wananchi wa kijiji cha Lola kuendelea kuvumilia mpaka pale mifumo ya kifedha itakapokuwa sawa Milioni 50 iliyotolewa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuja kujenga zahanati ya Lola italetwa maana tayari ilishaingia Halmashauri lakini kinachokwamisha kwasasa ni mifumo ya kifedha

Makamu mwenyekiti ametoa kauli hiyo mwishoni mwa juma alipoiongoza kamati ya fedha. Uchumi na Mipango kukagua ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Lola ambayo mpaka sasa kupitia michango ya wadau wakishirikiana na wananchi imefikia kiwango cha kuezekwa, kupigwa ripu, kufungwa dari na sasa wanaendelea kupanga mawe tayari kukamilisha sakafu kwa gharama ya Millioni 16

“Ndugu viongozi na wananchi wa Lola fedha yenu kwaajili ya ujenzi wa zahanati hii ilishafika Chunya changamoto ilipo mpaka sasa ni mifumo ya kifedha hivyo ninyi vumilieni tu fedha hizo zitatolewa na zitawafika, epukeni wapotoshaji wanaotoa maneno mbalimbali ili kuwafini na serikali ya Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan

Aidha kamati hiyo kupitia makamu mwenyekiti wake imewataka wananchi na viongozi kutohujumu miundombinu mbalimbali ya serikali inayojengwa katika maeneo yao na amesema kamati haitakubali miradi mbalimbali kuhujumiwa na mtu yeyeto bila kujali nafasi yake ama uwezo wake kifedha kwani lengo la serikali ni kuwarahisishia wananchi wake upatikanaji wa huduma mbalimbali katika maeneo wanayoishi

“Hatutamwacha salama mtu yeyote atakaye hujumu miradi ya maendeleo na nawaomba msijitokeza kuwasaidia watu wa namna hiyo wakibainika kuhujumu miundombinu yetu, achene tu sheria ichukue mkondo wake ili wajifunze na wapate adabu” Alisema Mhe Shumbi

Naye Nebart Gavu kwa niaba ya afisa mipango na uratibu wa wilaya ya Chunya amewahakikishia wananchi wa lola kwamba Changamoto iliyopo sio kwa fedha za zahanati ya Lola tu bali ni Halmashauri zote huku akitaja miradi mbalimbali yenye thamani ya Zaidi ya Bilioni Mbili pia pesa zimekwama kutokana na mifumo ya kifedha hivyo mifumo ikiwa sawa fedha hizo zitafika na kuendelea kumalizia mradi huo kama ilivyokusudiwa

Katibu tawala wa wilaya ya Chunya Ndugu Anakleth Michombero amewataka viongozi na wananchi wa kijiji hicho kuendela kushirkiana katika utekelezaji wa miradi ya Maendeleo kama walivyofanya katika ujenzi wa Zahanati hiyo kwakufanya hivyo hata miradi mingine itakayoletwa katika kijiji itafanikiwa pia

Kamati hiyo pia imeshauri uongozi wa kijiji hicho kuendelea kupanda miti kuzunguka eneo hilo la Zahanati huku wakichukua tahadhari ya umbali kutoka eneo jengo lilipojengwa ili kuepusha miti hiyo kuanguakia jengo hilo hapo mbeleni jambo linaloweza kuleta hasara isiyo ya lazima na kuisababishia hasara serikali na hata wananchi wa kijiji hicho pia

Zahanati ya kijiji cha Lola mpaka hatua ilipofika imegharimu Zaidi milioni 16 ambapo Nguvu za wananchi ni milioni 12,200,000/=, Wadau wa maendeleo wamechangia shilingi milioni mbili (2,000,000/=) huku serikali imetoa milioni Hamsini (50,000,000/=) kwaajili ya kukamilisha ujenzi huo.


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.