• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

WANAFUNZI WA SEKONDARI WAPATIWA ELIMU YA LISHE, CHUNYA

Imewekwa: October 18th, 2023

Afisa lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ndugu Simon Mayala  amewataka wanafunzi na wanachunya kwa ujumla kubadili namna ya ulaji wa vyakula ili kuepukana na changamoto mbalimbali zinazotokana na ulaji mbaya, na kushauri umuhimu wa kuzingatia lishe bora huku akisisitiza kwamba lishe bora ni kupata mlo kamili na sio kushiba kama ilivyozoeleka kwa jamii nyingi ikiwepo wanafunzi ambao baadaye ndio Taifa la Kesho.


Hayo ameyasema leo 18/10/2023  kwa nyakati tofauti  katika viwanja vya shule ya Sekondari Kiwanja  na Shule ya sekondari ya kata Itewe alipokuwa akitoa elimu ya Lishe ikiwa ni mwendelezo wa Kampeni ya lishe vijana balehe  kitaifa  yenye lengo la kutoa elimu ya lishe kwa vijana  na namna bora ya ulaji  unaozingatia afya.


‘’Lishe bora inaanza na namna ya ulaji kwani lishe bora sio kula na kushiba   hivyo vijana kama taifa la kesho tunapaswa kuzingatia namna ya ulaji bora kutokana na changamoto mbalimbali za kiafya zinazotokana na ulaji mbaya  kwani kumekuwa na wimbi kubwa la magonjwa ya moyo hii yote  ni kutokana na vyakula tunavyo vitumia’’ alisema Mayala


Mayala ameongeza  kuwa   vijana wanapaswa kula kwa kuzingatia afya jambo ambalo litasaidia kupunguza changamoto mbalimbali za kiafya kwa kutumia vyakula vinavyolinda mwili na kuwataka kuacha mara moja kula vyakula ambavyo vitawasababishia madhara ya kiafya kwa  baadaye.


Naye Mkuu wa shule ya Sekodari Kiwanja Jackson   Mnyalape amesema kuwa  elimu ya lishe wanoyoipata wanafunzi  ni muhimu kwa maisha yao ya sasa na hata maisha yao ya baadaye kwani itawasaidia hata kwa baadae watakapokuwa watu wazima na familia zao  hivyo elimu hiyo ni muhimu sana kwao  lakini pia watakuwa mabalozi wazuri hata watakapo rudi majumbani mwao.


Dorah Daniel, Isack Sajire kutoka shule ya sekondari kiwanja  na Norberth Mawazo pamoja na Anastazia Ndede wa shule ya sekondari ya kata Itewe  wamesema kuwa elimu ya lishe walioipata itawasaidia kupunguza au kuacha kula vyakula ambavyo vitawasababishia changomoto za kiafya kwa baadaye lakini pia  upimaji wa hali ya lishe umewasaidia kujua hali zao za lishe  na kujua wanatakiwa kufanya nini ili kuboresha zaidi hali zao za  lishe.


Kampeni ya lishe vijana balehe yenye kauli mbiu ’Lishe kwa Vijana Balehe , Chachu ya Mafanikio yao”imehitimishwa rasmi leo tarehe 18/10/2023 katika halmashauri ya wilaya ya Chunya, na  ilianza  tarehe 16/10/2023. Kampeni imefikia Shule za sekondari Isenyela, Kiwanja na Itewe ambapo wanafunzi 756 wamepima hali zao za Lishe wakati wa Kampeni hiyo, Kampeni hiyo imehusisha Maafisa elimu Sekondari Halmashauri ya wilaya ya Chunya, Wauuguzi kutoka hospitali ya Wilaya ,walimu pamoja na Wanafunzi

Afisa lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ndugu Simon Mayala akifafanua jambo wakati wa mafunzo ya Lishe kwa wanafunzi hasa Rika Balehe, Hapo ni shule ya Sekondari Kiwanja

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya kata Itewe wakiwa katika utulivu wakati wakipatiwa elimu ya Lishe na Maafisa toka ofisi za elimu, na wataalamu wa lishe

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kiwanja wakipata elimu ya Lishe kutoka kwa wataalamu wa Lishe

Wataalamu wa Lishe kutoka Halmashauri ya wilaya Chunya wakishirikiana na wanafunzi kupima urefu wao na uzito ili kutathimini hali ya lishe

Kazi ikiendelea ya upimaji wa urefu sambamba na uzito ili kutathimini hali ya lishe kwa mlengwa

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.