• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

WAKUU WA SHULE ZA SEKONDARI NA MAAFISA ELIMU KATA WAJENGEWA UWEZO UTEKELEZAJI MTAALA ULIOBORESHWA.

Imewekwa: January 24th, 2025

Mthibiti ubora wa shule wilaya ya Chunya mwalimu Arton Joseph Kayombo awajengea uwezo walimu wakuu wa shule za sekondari na maafisa elimu kata juu ya utekelezaji wa mtaala ulioboreshwa ukihusisha mafunzo ya amali na mafunzo jumuishi.

Mafunzo hayo yametolewa leo, Januari 24, 2025 katika ukumbi mdogo wa mikutano wa shule ya sekondari Kiwanja yakiwa na lengo la kuwaandaa walimu wanaofundisha shule za sekondari juu ya utekelezaji wa mtaala ulioboreshwa.

“Utekelezaji wa mtaala ulioboreshwa utaleta mabadiliko makubwa sana kwa jamii kwasababu malengo yake ni kuaandaa wanafunzi wenye uwezo wa kujitegemea kwakuwa elimu ya mafunzo ya amali inatolewa kwa vitendo na itapelekea kupunguza tatizo la upatikanaji ajira nchini” amesema Kayombo.

Aidha Mwalimu Kayombo amewahimiza walimu wakuu wa shule za sekondari kuendelea kutoa mafunzo endelevu shuleni(MEWAKA)ili kuwajengea uwezo walimu walio chini yao kuweza kutoa mafunzo yenye tija kwa kufuata mtaala wa mafunzo.

Awali akifungua mafunzo hayo, mwenyekiti wa wakuu wa shule za sekondari Wilaya ya Chunya Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Isangawana mwalimu Sikitu Wakson Shurra amesema ni wakati muwafaka sasa kwa walimu wakuu na maafisa elimu kata kuwasimamia walimu wanaofundisha kwenye shule zao za sekondari kuhakikisha maandalio ya somo na ufundishaji unaokidhi viwango na vigezo vilivyopo kwenye mtaala mpya ulioboreshwa unazingatiwa ili uleta tija.

Mwalimu Shurra amesema, walimu wakuu wanapaswa kukagua ufundishaji wa walimu ikiwemo ukaguzi wa andalio la somo, mpango na zana za kufundishia kama vinakidhi mahitaji ya somo husika.

Naye mwalimu mkuu wa shule ya sekondari Mayeka, mwalimu Flora Mwanchuli amesema Mabadiliko ya mtaala mpya ulioboreshwa utamfanya mwanafunzi atayehitimu mafunzo kwa ngazi ya sekondari kuwa na ujuzi utakaomsaidia kwenye maisha kwakuwa mafunzo ya amali yatatolewa kuanzia kidato cha kwanza mpaka kidato cha nne.

Kwa upande wake Afisa elimu kata ya Chalagwa, Fatuma Mahenge amesema, mtaala mpya ulioboreshwa una stadi nyingi za vitendo zinazompa chaguzi mbalimbali mwanafunzi kujifunza kitu anachokipenda na baada ya kuhitimu mafunzo mwanafunzi ataweza kumudu kufanya shughuli mbalimbali za uzalishaji mali kwakuwa alijifunza akiwa shuleni kupitia mafunzo ya amali na jumuishi.

Mafunzo ya mtaala mpya ulioboresha unahusisha mafunzo jumuisha na mafunzo ya amali ambapo utekelezaji wake umeshaanza kwa baadhi ya shule za sekondari nchini huku ukitajwa kuwa na tija kubwa katika maendeleo ya sekta ya elimu.

Mwenyekiti wa wakuu wa shule za sekondari Wilaya ya Chunya Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Isangawana mwalimu Sikitu Wakson Shurra akifungua mafunzo ya utekelezaji wa mtaala mpya ulioboreshwa kwa walimu wakuu na maafisa elimu katika ukumbi mdogo wa mikutano wa shule ya sekondari Kiwanja.

Mthibiti ubora wa shule Wilaya ya Chunya mwalimu Arton Joseph Kayombo akitoa mafunzo ya utekelezaji wa mtaala mpya ulioboreshwa kwa walimu wakuu na maafisa elimu katika ukumbi mdogo wa mikutano wa shule ya sekondari Kiwanja.

Walimu wakuu na maafisa elimu wakimpongeza mtoa mada wa mtaala mpya ulioboreshwa, Mthibiti Ubora shule Wilaya ya Chunya Arton Joseph Kayombo katika ukumbi mdogo wa mikutano wa shule ya sekondari Kiwanja, Januari 24, 2025.

Walimu wakuu na maafisa elimu wakifutia kwa makini mada mbalimbali za utekelezaji wa mtaala mpya ulioboreshwa katika ukumbi mdogo wa mikutano wa shule ya sekondari Kiwanja, Januari 24, 2025.


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.