• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

WADAU WA MAENDELEO WAMETAKIWA KUENDELEA KUMUUNGA MKONO MHE RAIS KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO

Imewekwa: January 28th, 2024

Mwenyekiti wa Halmashaui ya wilaya ya Chunya Mhe Bosco Said Mwanginde amewataka wadau wa maendeleo na Wananchi kwa ujumla kuendelea kumuunga mkono Mhe Rais katika kujenga, kulinda na kuiendeleleza miundombinu mbalimbali ya maendeleo katika maeneo yao na kufanya hivyo itaendelea kusaidia uimarishaji wa upatikanaji wa huduma kwa wananchi katika maeneo Yao

Ametoa rai hiyo jana Jumamosi ya tarehe 27/1/2024 alipokuwa anazungumza na wananchi katika hafla ya kukabidhi Chumba kimoja cha darasa kilichojengwa na mdau wa Maendeleo ndugu Salmon J Chanzu katika Sule ya msingi ya Soweto iliyopo kata ya Kasanga Halmashauri ya wilaya ya Chunya

“Kujenga chumba cha Darasa kama alivyofanya ndugu Salmon sio kwamba anapesa nyingi sana, lakini ni uzalendo na kuipenda nchi yako hivyo wadau wengine wa maendeleo katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya tuendelee kumuunga mkono Mhe Rais katika ujenzi wa Miundombinu mbalimbali hii itaendelea kuturahisishia upatikanaji wa huduma katika maeneo yetu” alisema Mwanginde

Aidha Mhe Mwanginde pamoja na kumshukuru mdau wa maendeleo kwa kujenga darasa hilo amewaagiza watendaji wote wa Serikali kuwashirikisha wadau wa maendeleo katika maeneo yao ili washiriki ipasavyo katika ujenzi wa miundombinu ya maendeleo na inawezekana wadau wapo ntayari kushiriki katika maendeleo lakini sisi watendaji wa Serikali mnaweza kuwa kikwazo cha wadau kushiriki katika shughuli mbalimbali za maendeleo

Awali kabla ya kumkaribishwa Mwenyekiti wa Halmashauri aliyekuwa mgeni rasmi katika Hafla hiyo Diwani wa kata ya Kasanga Mhe Benson Msomba amemshukuru mdau wa maendeleo kujenga Chumba cha darasa katika Shule ya Msingi Soweto na ameendelea kuhimiza wananchi na watu wote waliopo katika kata ya Kasanga kuendelea kuishi vizuri na wadau wa maendeleo jambo linaloleta matokeo chanya kama kuongezewa nguvu katika jitihada za maendeleo

Awali akisoma Risala ya kijiji cha Soweto kwa mgeni rasmi mwalimu mkuu wa shule ya msingi Soweto mwalimu  Mtalege Mwakalobo Classford alisema bado wanaupungufu wa Chumba kimoja cha darasa ambapo mpaka sasa wanaendelea kukusanya Fursa ili taratibu za ujenzi wa Chumba hicho cha Darasa uanze mapema lakini pia alimshukuru mdau wa maendeleo kwa kujenga Chumba hicho ambacho kitasaidia wanafunzi 45 wa darasa la awali katika shule hiyo na kupunguza idadi ya wanafunzi wengi kwenye chumba kimoja

Shule ya Msingi Soweto ina jumla ya wanafunzi 350 ambapo Chumba kilichojengwa kitapunguza upungufu wa vyumba viwili uliokuwa unaikabili shule hiyo ambapo upungufu wa chumba kimoja kinachobaki kwasasa fursa zinaendelea kukusanywa ili taratibu za ujenzi zianze mara moja hatimaye kuepukana na changamoto ya upungufu wa vyumba vya madarasa kabisa katika shule hiyo.

Viongozi Mbalimbali wakimshukuru Mdau wa Maendeleo ndugu Salmon Chanzu baada ya kufungua rasmi chumba cha Darasa alichojenga kwenye Shule ya Msingi Soweto

Cheti ya pongezi kilichotolewa na uongozi wa kata ya Kasanga kwa Mdau wa Maendeleo ndugu Salmon Chanzu ikiwa ni ishara ya kutambua na kuthamini mchango wa mdau huo katika maendeleo ya kata hiyo

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.