• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

WADAU WA AFYA NA MAENDELEO YA VIJANA WAKUMBUSHWA MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA UTELKELEZAJI.

Imewekwa: January 22nd, 2025

Mkuu wa divisheni ya maendeleo ya jamii Bi Marietha Mlozi  amewataka  wadau wa mashirika yasiyokuwa ya kiserikali kuzingatia mambo muhimu yatakayowasaidia katika utekelezaji wa shughuli zao ikiwa ni pamoja na  kuwasilisha taarifa za robo za utekelezaji wa shughuli zao  katika idara husika, ushiriki wa wadau hao  katika vikao mbalimbali, kulipa ada za kila mwaka na mambo mengine mengi.

Kikao hicho cha wadau  kimeketi  leo Tarehe 22/01/2025 katika Ukumbi wa mikutano wa Omary City  Wilayani Chunya na kuhusisha wadau mbalimbali  wanaotekeleza miradi ya afya na maendeleo kwa vijana kimeandaliwa na shirika la DSW linalotekeleza mradi wa afya na maendeleo kwa vijana(REST)  kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Chunya.

Wadau  hao wa mashirika yasiyokuwa ya kiserkali wanaotekeleza miradi ya afya na maendeleo ya  vijana wamekutana na kujadili mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na uwasilishwaji wa shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na mashirika hayo kwa lengo la kufahamiana , pamoja na kubadilishana uzoefu katika utekelezaji wa majukum yao.

Naye Mkurugezi wa Shirika la DSW ndugu Peter Owaga mbali na kuelezea shirika hilo, ameeleza pia shughuli mbalimbali zinazotekelezwa katika maradi wa afya na maendeleo ya vijana (REST) huku akiwataka wadau wanaotekeleza miradi ya afya na maendeleo kwa vijna kuendelea kushirikiana  ili kumuwezesha na kumsaidia kijana  kubaki salama  ikiwa ni pamoja na kujitambua katika masuala mazima ya afya ya uzazi, pamoja na kujikwamua kiuchumi.

“Ndugu wadau leo tumefahamiana na kujua kila mmoja wetu kazi anazofanya na maeneo anayofanya kazi, hivyo sisi kama wadau tunaweza kuona namna gani tunaweza kushirikiana katika utekelezaji wa shughuli zetu kwa maeneo yale ambayo tunatekeleza mradi , sambamba na hilo tunaweza kushirikiana hata katika  maandiko mbalimbali kwasababu kazi yetu kubwa kama wadau ni kutatua changamoto zilizopo kwenye jamii.”amesema Owaga.

Aidha, wadau hao wamewasilisha shughuli mbalimbali wanazofanya ikiwa ni pamoja na mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia ,uwezeshaji wa vijana kiuchumi , elimu ya afya ya uzazi kwa vijana  ikiwa ni pamoja na mapambano dhidi ya magonjwa ya ngono na mambo mengine mengi yanayolenga kutatua changamoto katika jamii hususani kwa vijana ambao ni taifa la leo na kesho.

Kikao kazi cha wadau wanaotekeleza miradi ya  afya na maendeleo ya Vijana kimewahusiaha wadau wa mashirika mbalimbali yanayotekeleza miradi yake katika halmashauri ya Wilaya ya Chunya, mashirika hayo ni pamoja na shirika la DSW,HJMFRI,TDFT,PASADA,PHEDEA, Tasnema, Prospering for mind and window for Justice kwa lengo la kufahamiana na kuweka mipangokazi itakayo endelea kuwakutanisha  wadau hao pamoja.

Mkurugenzi wa shirika la DSW Ndugu Peter Owaga  akizungumza na wadau wanaotekeleza miradi ya afya na maendeeo ya Vijana namna ya kuendeleza ushirikiano wao katika kutatua changamoto mbalimali za vijana katika jamii wakati wa kikao kazi na wadau hao kilichoketi ukumbi wa mikutano wa Omary City Wilayani Chunya.

Mratibu wa mradi wa Afya na maendeleo ya vijana (REST) Bi celina Protas akielezea shughuli  zilizotekelezwa kupitia mradi huo wakati wa kikao kazi na wadau wa mashirika yasiyo ya kiserikali katika Ukumbi wa mikutano wa Omary City Wilayani Chunya.

Afisa Maendeleo ya jamii Vijana  Halmashauri ya Wilaya ya Chunya Ndugu James Sunge  akiwakumbusha wadau juu ya usajili na wa mashirika yasiyokuwa ya kiserikali wakati wa kikao kazi cha wadau wa afya na maendeleo ya vijana kilichefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Omary City Wilayani Chunya.


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.