• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

VYAMA VYA SIASA KUHAMASIHA WANANCHI KUJITOKEZA KWENYE UBORESHAJI DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA.

Imewekwa: December 21st, 2024

Afisa Mwandikishaji Jimbo la Lupa Wilayani Chunya Wakili Athumani Bamba amefanya kikao na viongozi wa vyama vya siasa kwaajili ya kujadili mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwajulisha juu za zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la Mpiga kura kwani vyama vya siasa ni wadau wa kubwa wa zoezi hilo ili waweze kusaidia kuhamasisha jamii kujitokeza   kujiandikisha na kuboresha taarifa zao katika daftari la kudumu la Mpiga kura

 Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi za Uchaguzi  jimbo la Lupa  Wilaya ya Chunya Leo Tarehe 21/12/2024 ambapo Viongozi mbalimbali wa vyama vya Siasa Wilaya ya Chunya wameshiriki

“Zoezi la uandikishaji litaanza rasmi tarehe 27/12/2024 hivyo lengo la kikao hichi ni kuwapa taarifa ninyi kama viongozi wa vyama vya sias kwasababu tunajua mnamtaji mkubwa wa watu hivyo mtatusaidia kuhamasisha na kuwajulisha Wananchi juu Ya zoezi la kujiandikisha pamoja na kupeleka Mawakala wenu katika vituo vya kujiandikishia”

Aidha Afisa mwandikishaji jimbo la Lupa ameongeza kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ipo Wilayani Chunya kwaajili ya kuhakikisha zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la Mpiga kura linafanyika kwa ukamilifu kwani zoezi hilo limeeanza na utolewaji wa Mafunzo kwa Maafisa waandikishaji wasaidizi ngazi ya kata na mafunzo hayo yataendelea kwa wahusika wengine wa zoezi hilo pamoja na kuapishwa kwa Mawakala wa vyama vya siasa

Naye Afisa Uchaguzi Wilaya ya Chunya ndugu Ridhiwani Mshighati  amesema kuwa zoezi la uboreshaji wa daftari la Mpiga kura litahusisha watu ambao  wamehama kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine, wale waliokuwa hawajafikisha umri wa kujiandikisha na sasa wamefikisha umri wa kujiandikisha lakini pia kuondoa taarifa za watu waliofariki na sifa zingine ambazo zimeainishwa .

Katibu wa Chama cha Mapinduzi ndugu Charles Jokery, Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ndugu Yohana Mpamba na Mwenyekiti wa ACT wazalendo ndugu Timoth Mwafumu wametoa mapendekezo yao juu ya ratiba iliyotolewa ya kuwaapisha Mawakala lakini pia kupanga vituo kulingana na jographia ya Chunya jinsi ilivyo ili kuwarahisishia  na kuwapunguzia adha mbalimbali Mawakala  wa vyama  vya siasa

Kikao cha Afisa Mwandikishaji jimbo la Lupa na Viongozi wa Vyama vya siasa kimehudhuriwa na  Afisa Mwandikishaji Jimbo, Afisa Uchaguzi, Viongozi kutoka vyama  viNNE  vya siasa ambavyo ni CCM, CHADEMA , ACT wazalendo, CHAUMMA na   Balaza la Wanawake  Chadema (BAWACHA) na kujadili mambo mbalimbali kuhusu zoezi la uboreshaji daftari la kudumu la Mpiga kura ikiwa ni maandalizi kuelekea uchaguzi Mkuu Octoba 2025

Afisa Mwandikishaji jimbo la Lupa wakili Athuman Bamba  akizungumza na Viongozi wa Vyama vya Siasa  juu ya zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la Mpiga kura

Afisa Uchaguzi Wilaya ya Chunya ndugu Ridhiwani Mshigati akizungumza  sifa za watu wanaopaswa kujiandikisha na kuboresha taarifa zao katika daftari la kudumu la Mpiga kura

Katibu wa Chama cha Demokrsia na Maendeleo Chadema ndugu Yahana Mpamba  akitoa mapendekezo wakati wa kikao cha Afisa mwandikishaji Jimbo la Lupa na vyama viongozi wa vyama vya siasa .

Afisa Mwandikishaji jimbo la Lupa watatu kutoka kulia kwenye picha ya pamoja na Viongozi wa vyama vya siasa Wilaya ya Chunya baada ya kumaliza kikao

Viongozi wa vyama vya siasa Wilayani Chunya wakisikiliza lengo la kikako kutoka kwa Afisa Mwandikishaji Jimbo la Lupa  

 

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.