• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

VIJANA CHUNYA KUNUFAIKA NA MRADI WA AFYA NA MAENDELEO YA VIJANA (REST).

Imewekwa: December 5th, 2024

Mradi wa Afya na maendeleo ya vijana (REST) unaotekelezwa na shirika la DSW Tanzania katika Hammashauri ya Wilaya ya Chunya  unalenga kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili vijana ikiwa ni pamoja na Afya ya Uzazi, ukatili wa kijinsia  na changamoto pamoja na kuwawezesha vijana kiuchumi ili kuweza kujitambua , kulinda Afya zao na kujitegemea kiuchumi.

Hayo yamezungumzwa   na Mkurugenzi wa Shirika la DSW-Tanzania, ndugu Peter Owaga  Desemba 5, 2024 wakati wa mafunzo kwa vijana  vinara ili waweze kuwajengea uwezo vijana wenzao pamoja na kushiriki katika shughuli za maendeleo katika maeneo yao kwa kushirikiana na serikali.

Awali akifungua mafunzo hayo Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Chunya Mwl. Costansia Komba amesema kuwa Halmashauri wako tayari kuyafanyia kazi yale yote yatakayohitaji kufanyiwa kazi huku akiwataka vijana washiriki wa mafunzo hayo kwenda kuyafanyia kazi mafunzo hayo katika maeneo yao ili kutimiza adhima ya mradi wa REST ya kuwasaidia vijana katika afya ya uzazi, ukatili wa kijinsia,pamoja na kujikwamua kiuchumi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la DSW Tanzania ndugu Peter Owaga amesema kuwa shirika linatekeleza miradi mbalimbali ya afua za afya na maendeleo kwa vijani ili kuona kijana ni mtu mwenye manufaa katika jamii ikiwa ni pamoja na kuwasaidia vijana kijitambua kwenye masuala ya afya ya uzazi, ukatili wa kijinsia , stadi za maisha  na uongozi pamoja na kuwahimiza kushiriki kwenye miradi ya maendeleo.

“ Kwenye huu mradi wa REST kazi yetu kubwa itakuwa ni kuimarisha uwezo wa Vijana Vinara ambao wametambuliwa na serikali kwaajili  kuwajengea uwezo kwaajili ya kuwafikia vijana wengine ikiwa ni pamoja kuhimiza ushiriki wao katika  shughuli za maendeleo, kuimarisha stadi za maisha na uongozi” alisema Owaga.

Aidha  Owaga ameongeza kuwa,   mradi wa REST  unalenga kuimarisha mifumo iliyopo, kujenga uwezo wa wataalam waliopo ili kutokomeza ukatili wa kijinsia, kuimarisha upatikanaji wa huduma rafiki kwa vijana pamoja na kuhakikisha sauti za vijana zinakuwa mstari wa mbele kuibua changamoto za vijana na kuzitafutia ufumbuzi .

Afisa Maendeleo vijana Wilaya ya Chunya  ndugu James Sunge amesema kuwa vijana wengi wamekuwa na changamoto nyingi  kama vile mimba za utotoni , uonjwa wa UKIMWI  , ukatili wa kijinsia na changomoto zingine zinazochagizwa na  shughuli mbalimbali za kiuchumi ikiwa ni pamoja na uchimbaji wa madini  hivyo ujio wa mradi wa REST kutoka shirika la DSW utasaidia kuzitatua na kuzipunguza changamoto hizo.

Akiongea kwa niaba ya wawezeshashi mwezeshaji wa Kitaifa  Huduma rafiki kwa Vijana bi Mariam Mhanjim amesema, shirika la DSW wanawawezesha vijana  vinara ili kuwasaidia vijana wengine  kutokana na changamoto mbalimbali zinazowakabili vijana ikiwa ni pamoja na  ukosefu wa elimu  juu ya changamoto mbalimbali  za Afya  hivyo vijana kinara watawasaidia viajana wengine waweze kufika kwanye vituo vya Afya kwaajili ya kupata huduma au kuwapa huduma wanapofika katika vituo vya Afya ili kuwawezesha vijana kuvuka wakiwa salama.

Wakiwawakilisha  vijana wengine waliopata mafunzo REST, ndugu  Samuel Macha Mtoa huduma za afya na ndugu Ngugu Joseph Kasota, Mtoa huduma za Afya ngazi ya jamii wamesema kuwa mafunzo waliyoyapata yatawasaidia kuwaelimisha vijana   na kuwasaidia katika kukabiliana na changamoto mbalimbali za kiafya  na changamoto zingine ili kijana aweze kujua njia sahihi na salama za kujikinga na kuvuka ujana akiwa salama lakini pia kujitambua kama kijana ni nguvu kazi ya taifa.

Mradi wa REST unaotekelezwa na shirika la DSW-Tanzania unatekelezwa katika kata 6 ambazo ni kata ya Mafyeko,Lupa, Makongolosi, Matundasi,Chokaa na Sangambi  za Halmashauri ya Wilaya ya Chunya  katika tarafa ya Kiwanja na Kipembawe yamehudhuriwa na Watoa huduma za Afya kutoka katika vituo vya kutolea huduma za Afya, Watoa Huduma za Afya ngazi ya jamii, Afisa  Maendeleo vijana , Afisa  Maendeleo wa Wilaya ya Chunya na Walimu kutoka shule za msingi na sekondari katika Wilaya ya Chunya.

.



Kaimu Mkurugenzi  Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, Mwl. Costansia Komba akifungua mafunzo yanayotaolewa na Shirika DSW- Tanzania kupitia mradi wa REST unaotekelezwa kwenye kata sita katika Halmashauri ya Wilaya ya Chunya.

Mkurugenzi waShirika la DSW -Tanzania akizungumza na Vijana vinara kutoka kata 6 za mradi wakati wa mafunzo yaliyotolewa Ukumbi wa Omary City katika Halmashauri ya Wilaya ya Chunya

w

Wallimu wa shule za msingi na Shile za Sekondari wakiwa kwenye picha ya pamoja na Wafanyakazi wa Shirika la DSW-Tanzania  katika Ukumbi wa Mikutano wa Omary City katika Hamlmashauri ya Wilaya ya Chunya

Watoa huduma za Afya wakiwa kwenye picha na wafanyakazi wa shirika la DSW-Tanzania   baada ya kutoka kwenye mafunzo  Ukumbi wa Omary City




Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.