• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

UPANDAJI WA MITI NI TAKWA LA KISHERIA KATIKA KILIMO CHA TUMBAKU

Imewekwa: March 9th, 2024

Timu ya Tathimini ya zao la Tumbaku katika mkoa wa kitumbaku Chunya kupitia wataalamu Mbalimbali imewataka Vyama vya msingi vya Ushirika kuhakikisha wanaendelea kuhimiza na kuwasimamia wakulima katika upandaji na uhifadhi wa miti kwani ukaguzi wa miti iliyopandwa kwa mwaka jana na mwaka huo utafanyika mapema kabla ya ufunguzi wa masoko

Wakizungumza kwa Nyakati tofauti katika vyama vya Nkung’ungu na Ifuma wawakilishi kutoka bodi ya Tumbaku, Chama kikuu cha ushirika Chunya CHUTCU pamoja na wadau wanaounda timu ya tathimini ya zao kwa mwaka 2024 wamesema kabla ya masoko kufunguliwa rasmi mapema mwezi Aprili ukaguzi wa miti iliyopandwa mwaka jana na mwaka huu utafanyika hivyo wamewataka viongozi wa bodi kuhakikisha wanachama wao wanatimiza takwa la kisheria kuhusu kilimo cha zao la Tumbaku.

“Kabla masoko hayajafunguliwa rasmi mwezi wa nne, kutakuwa na zoezi la ukaguzi wa miti iliyopandwa mwaka jana na mwaka huu, hivyo hakikisheni miti imepandwa na imetunzwa kwa mujibu wa taratibu zetu za kilimo cha Tumbaku..., Zingatieni taratibu, kanuni na miongozo ya Kilimo cha Tumbaku…, Tumbaku tuliyoiona endeleeni kuitunza ili tukaione pia kwenye Masoko hapo baadaye hivyo wasimamieni wakulima ili wafikie malengo”. Alisema Cleopa Nziku, Loysujaki Kimiri na Ahazi Itika

Aidha Cleopa Nziku kutoka Bodi ya Tumbaku mkoa wa Kitumbaku Chunya amewashauri wakulima kuzingatia ushauri na maoni yanayotolewa na timu ya Tathimini ikiwa ni pamoja na kuendelea kuwahimiza wakulima kutunza tumbaku ili kupata Tumbaku yenye ubora kwakuwa zoezi la Tathimini huwa lina uhalisia sana hivyo wakizingatia ushauri wa timu nzima itawasaidia kufika malengo waliyojiwekea wao kama chama

"Zoezi hili huwa halidanganyi hivyo zingatieni ili kuhakikisha wanayafanyia kazi hayo mapendekezo ya Wajumbe wa watathimini na Msipofuata taratibu za kilimo cha Tumbaku tutawatoeni hivyo hakikisheni mnazingatia kutowashirikisha watoto kwenye kazi za kilimo cha Tumaku, Zingatieni kupanda miti na kuzingatia usalama kwa watu wanaofanyakazi Maeneo yenu” Aliongeza Bwana Nziku

Naye Ahazi Itika kutoka kampuni ya Kwawa Leaf Tobacco amewashauri viongozi wa vyama vya Msingi na bodi kwa ujumla kuhakikisha wanawasimamia wananchi kuchuma Tumbaku kwa wakati ili kuepuka upotevu ambao unaweza kuepukika maana kiwango tunachokiona ni kizuri na kitanatakiwa kusimamiwa ili masoko yatakapoanza tushuhudie hali nzuri tuliishuhudia tukiwa kwenye tathimini

Adili Juma, Ndakson msole na Chrispin Mpasula kwa niaba ya viongozi wengine wa bodi ya Chama cha Ushirika Nkung’ungu wanawashukuru timu nzima ya tathimini iliyofika kwenye chama hicho na kusema wamepokea maelekezo, ushauri na mapendekezo na kuahidi kuyafanyia kazi ili kufikia makisiso ya kuzalisha kwa chama chao

Zoezi ya tathimini ya zao la Tumbaku linaendelea katika mkoa wa kitumbaku Chunya ikiwa ni siku yake ya nne ambapo timu zote mbili zikiendelea kufika katika mashamba ya wakulima kwakushirikiana na wajumbe wa bodi za vyama husika na kuona hali ilivyo na kutoa ushauri mbalimbali huku zoezi hilo likitegemewa kutoa makisio ya uzalishaji kwa msimu wa 2023/2024 tayari kuelekea ufunguzi wa masoko mapema mwezi wa nne

Mjumbe wa Chama Cha ushirika cha Nkung'ungu akichangia jambo mbele ya timu ya Tathimini ya zao la Tumbaku ilipopita kwenye Chama hicho na kufanya tathimini ya zao hilo

Timu ya Tathimini ya zao la Tumbaku ikifanya Majumuisho kwenye moja ya mashamba yaliyopitiwa wakati wa tathimini baada ya kumalizia kutembelea shamba hilo na kujionea hali ya uzalishaji

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.