• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

TUILINDE AMANI YETU

Imewekwa: July 25th, 2023

Katibu tawala wa wilaya ya Chunya ndugu Anakleth Michombero akimwakilisha mkuu wa wilaya katika maadhimisho ya siku ya kumbukizi ya mMashujaa amewaasa wananchi wa wilaya ya Chunya kuilinda Amani tuliyonayo kwani Amani hainunuliwi kama bidhaaa nyingine tukiipoteza Amani kuirejesha ni kazi kubwa hivyo twendelee kuilinda na kuidumisha Amani ya nchi yetu


Hayo ameyazugumza wakati wa maadhimisho ya siku ya kumbukizi ya mashujaa waliopigania taifa letu ambayo huadhimishwa julai 25 kila mwaka ambapo kwa halmashauri ya wilaya ya Chunya Maadhimisho hayo yamefanyika leo 24/07/2023 katika soko la Uhindilini lililopo kijiji cha Kibaoni kata ya Chokaa.


“Tunapaswa kuwaenzi mashujaa wetu kwa vitendo kwa kuilinda Amani tuliyonayo jukumu la kuilinda Amani ni suala la kila mmoja wetu si suala la viongozi au chama fulani tukumbuke kwamba  Amani ikitoweka haitaangalia kiongozi au kada wa chama fulani kwahiyo tuilinde sana Amani yetu tuliyonayo” amesema Michombero


Akisoma taarifa ya siku ya mashujaa ndugu Anakleth Michombero amesema kuwa tuna adhimisha siku hii kwa kuwakumbuka mashujaa waliojitoa uhai wao kupigania taifa letu kwa Uzalendo Kama Halmashauri ya wilaya ya Chunya tunaungana na Taifa kuwakumbuka na kuwaombea mashujaa wetu walipoteza maisha yao wakati wakuipigania nchi yetu kwa kuidumisha na kuiendeleza misingi ya Amani waliyotuachia.


“Misingi mizuri na amani iliyojengwa na waasisi wa Nchi yetu hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na hayati Abeid Amani Karume imetufanya wananchi wa Chunya kuishi kwa Amani na utulivu huku tukifanya shughuli zetu za kila siku za maendeleo bila kubuguziwa na kuingiliwa na mtu yeyote hali ambayo imesababisha wilaya yetu ya Chunya kuwa kivutio kizuri cha uwekezaji katika shughuli mbalimbali za uchimbaji wa madini, kilimo cha mazao mbalimbali na Ufugaji”


Akitoa salamu katika maadhimisho hayo Katibu wa chama cha Mapinduzi wilaya ya Chunya ndugu Charles Jokery Amesema kuwa Nchi hii imepiganiwa na watu wengi kutoka sehemu tofauti tofauti za nchi yetu Akiwemo hayati mwalim Julius Kambarage Nyerere ,Hayati Abeid Amani Karume ,  na wengine wengi ambao leo hii wametufanya tunaishi kwa Amani na utulivu.


Awali akifungua maadhimisho hayo mwenyekiti wa kjiji cha kibaoni Ndugu Joshua Mambalala ameendelea kuwakumbusha wananchi kuhusu suala la usafi kuwa ni sehemu ya maisha yetu ya kila siku hivyo wananchi wanapaswa kuhakkikisha mazingira yanakuwa safi muda wote bila kusubiri msukumo kutoka kwa viongozi kila mtu anajukumu la kufanya usafi mazingira yanayomzunguka na kuhakiksha yanakuwa safi na salama muda wote kwaajili ya usalama wa afya zetu.


‘’Ndugu zangu niwaombe suala la usafi tusisubiri msukumo kutoka kwa viongozi wetu wa serikali usafi uwe sehemu ya maisha yetu ya kila siku tuhakikishe mazingira yetu yote yanakuwa safi na salama muda wote na kuifanya Tanzania yetu kuwa na mazingira safi na salama kwa afya zetu’’


Maadhimisho hayo  ya kumbukizi ya siku ya mashujaa yameadhimishwa wilayani Chunya kwa kufanya usafi maeneo mbalimmali ya soko la uhindini, ikitanguliwa na dua ya kuwaombea mashujaa wetu iliyoongozwa na viongozi wa dini. Viongozi mbalimbali wa Chama na serikali wilaya ya Chunya wamehudhuria,viongoziwa ulinzi na usalama, wafanyakazi halmashauri ya wilaya ya Chunya, wafanya biashara na wananchi wengine

Watumishi wa halmashauri ya wilaya ya Chunya wakifanya usafi wa mazingira katika Soko la Uhindini siku ya maadhimisho ya kumbukizi ya mashujaa

  Maafisa waJeshi la polisi wakifanya usafi wa mazingira siku ya kumbukizi  ya Mashujaa  katika Soko la Uhindini Wanafunzi wa shule ya msingi kibaoni wakifanya usafi wa mazingira  katika Soko la Uhindini siku ya maadhimisho ya kumbukizi ya Mashujaa

Maafisa waJeshi la polisi  pamoja na wananchi wakimsikiliza mgeni rasmi  baada ya zoezi la usafi kukamilika

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.