• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

TATHIMINI YA ZAO LA TUMBAKU IWE NA UHALISIA

Imewekwa: March 5th, 2024

Kaimu mwenyekiti wa Wadau wa Tumbaku Mkoa wa Kitumbaku Chunya Ndugu Lameck John Matukulu amewataka wadau na wataalamu wote wa tumbaku waliokusanyika wilayani Chunya kwa lengo la kufanya tathimini ya zao la Tumbaku kwa msimu huu wa 2023/2024 kuhakikisha wanatumia nguvu, akili na kujituma ili kuhakikisha matokeo ya zoezi la tathimini ya zao yanakuwa na uhalisia

Ametoa kauli hiyo tarehe 04/03/2024 wakati wa kikao cha kujengeana uwezo ikiwa ni maandalizi ya zoezi la kufanya tathimini ya zao la Tumbaku kwa msimu wa kilimo 2023/2024 zoezi ambalo linaanza rasmi tarehe 05/03/2024 zoezi ambalo litadumu zaidi ya siku 10 na litahusisha vyama vyote 33 vilivyopo katika Mkoa wa Kitumbaku Chunya

Awali akizungumza kuhusu tathimini ya zao hilo kwa msimu wa 2022/2023 katibu wa wadau wa Tumbaku mkoa wa kitumbaku Chunya ndugu Faustine Mtweve amewapongeza wajumbe walioshiriki zoezi la tathimini kwa msimu uliopita kwakufanya kazi kwa weledi kupelekea Mkoa wa Kitumbaku Chunya kuwa na ufanisi wa asilimia 101 jambo ambalo lilichagizwa na kujituma, uzalendo pamoja na ushirikiano uliokuwepo wakati wa zaoezi hilo hivyo amewataka wajumbe wa kikao kuhakikisha ufanisi unaongezeka Zaidi

“Mwaka jana tulifanikiwa kuwa na asilimia 101 za ufanisi hivyo lazima niwapongeze wote mlioshiriki zoezi la Tathimini msimu uliopita lakini niwaombe tushirikiane, tupendane na tushikamane ili kwa msimu huu tuwe na asilimia Zaidi ya tulizopata msimu uliopita na hilo linawezekana kama tukishirikiana bila kujali utofauti wa taasisi tunazotoka”

Naye Mjumbe mwezeshaji kutoka Bodi ya Tumbaku Mkoa wa Kitumbaku Chunya Ndugu Cleophas Nziku amewaambia wajumbe kwamba wanategemewa sana na taasisi walizotoka, serikali, wadau wa Tumbaku, Taasisi za kifedha na maeneo mengine hivyowameaasa wafanyekazi kwa weledi mkubwa ili wadau wote wanaowategemea wapate taarifa sahihi

“Takwimu hizi ni muhimu sana maana zinatumika maeneo mbalimbali ikiwemo Taasisi Binafsi na serikali wanategemea Takwimu hizi, Taasisi za kifedha na taasisi nyingine nyingi zinategemea takwimu zitakazopatikana kwenye tathimini ya zao la Tumbaku tunayotaraji kuaianza kehso hivyo nimwaombe tuwe makini sana. Sisi ni wataalamu na tunategemewa sana na tusifanye kazi kwa Mihemko, tuzingatie weledi ili tupate takwimu stahiki.

Akichangia mjadala wa utangulizi kabla ya kuanza rasmi zoezi la Tathimini Meneja Mahusiano wa Kampuni ya Kwawa Ndugu Goodluck Mwasa amewataka viongozi kuwa na uongozi mzuri na shirikishi kama walivyofanya msimu uliopita jambo lililopelekea Mkoa wa Kiumbaku Chunya kuwa na ufanisi mzuri wa asilimia 101

Naye Bwana Shamba ambaye pia ni meneja wa eneo kutoka Kampuni ya Premium Active ndugu Samwel J Philipo amewahimiza wadau wengine watakaoshirikiana kufanya tathimini ya zao la Tumbaku kwa mwaka 2024 kufanya kazi kwa bidii huku akiwakumbusha kuuliza maeneo yote korofi mapema wakati wa mafunzo hayo kwani kazi ya tathimi huwa inakuwa ngumu sana mnapoanza kufanyakazi ya kuathimini ili hali wengine bado kuna maeneo hawaelei nini cha kufanya

Zoezi la Tathimini ya zao la Tumbaku linalenga kupata makadirio ya uzalishaji wa zao husika kwa msimu wa kilimo mwaka husika ili maandalizi ya soko yaandaliwe sawa na makadirio husika, zoezi hilo linahusisha taasisi mbalimbali zikiwepo Halmashauri ya wilaya ya Chunya na Songwe, Bodi ya Tumbaku, Chama kikuu cha Ushirika wa wakulima wa Tumbaku Mkoa wa kitumbaku Chunya Mkoani Mbeya CHUTCU, Kampuni ya za unuazi wa Tumbaku ikiwa ni pamoja na Mkwawa, Premium, Magefa, Yaya, PATL Pamoja na TORITA/TARI

Wataalamu wa kilimo wakiwa katika tathimini kwa vitendo wakati wa kikao cha ufunguzi kilichoketi tarehe 4/3/2024

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.