• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

Imewekwa: March 21st, 2025

Wenyeviti na wajumbe wa Halmashauri ya vijiji vya Mwiji na Lualaje, tarafa ya Kipembawe wamejengewa uwezo kwenye mafunzo ya siku moja ya utawala bora, uongozi na manajimenti ya rasilimali fedha ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na kuthibiti matumizi mabaya ya rasilimali fedha.

Afisa Tarafa ya Kipembawe, Kasim Salimu Kilondomara ametoa mafunzo hayo Machi 21, 2025 kwenye ukumbi wa mikutano wa shule ya sekondari Lualaje uliopo, tarafa ya kipembawe Wilayani Chunya, ikiwa ni muendelezo wa jitihada za kuboresha utendaji kazi na utawala bora kwa watumishi wa umma wa tarafa ya Kipembawe.

“Nimefanya tafiti nimegundua kuwa, vijiji vingi havikusanyi mapato mengi ilihali fursa ya kukusanya ipo, miradi mingi iliyopo katika ngazi ya kijiji haisimamiwi ipasavyo na wananchi wamekuwa na kero za muda mrefu ambazo hazipatiwi ufumbuzi ndio maana nimeamua kutoa mafunzo haya ili kuwajengea uwezo wenyeviti wa vijiji na wajumbe ya Halmashauri ya vijiji kujidhatiti kutoa huduma bora kwa wananchi” amesema Kilondomara.

Aidha, Kilondomara amebainisha kuwa, wenyeviti wa vijiji, wajumbe wa Halmashauri ya vijiji walipatikana baada ya uchaguzi wa serikali za mitaa kumalizika mwezi Novemba, 2024 hivyo baadhi yao hawana uzoefu kufanya kazi, semina hiyo imelenga kuwafahamisha majukumu yao, muundo wa kijiji, mipaka ya kiutawala, kutatua kero za wananchi, kusimamia miradi ya maendeleo kwa ufanisi na kuongeza tija ya kukusanya mapato.

“Nimeshatoa mafunzo haya ya elimu ya utawala bora, uongozi na menejimenti ya fedha  kwa vijiji 23 vya Tarafa ya Kipembawe bado kijiji kimoja tu, nikihitimisha mafunzo nitafanya tathimini kubaini mabadiliko ya utendaji kazi kwa kila kijiji na kuchukua hatua stahiki kwa kijiji kitakacho kiuka miongozo na taratibu za kisheria kutoa huduma kwa wananchi” amesema Kilondomara.

Kilondomara amewasisitiza wenyeviti wa vijiji, wajumbe wa Halmashauri ya vijiji kuwahimiza wananchi kushiriki kwenye mikutano ya hadhara na kuchangia fursa mbalimbali kwenye miradi ya maendeleo inayoletwa na serikali kuu vilevile kuibua na kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya vijiji vyao. 

“Viongozi wa vijiji munapaswa kufanya mikutano ya hadhara na kutoa taarifa ya mapato na matumizi ya vijiji kuonesha uwazi na matumizi bora ya rasilimali fedha ambazo ni msingi wa maendeleo ya vijiji vyetu” amesema Kilondomara.

Naye, mjumbe wa kamati ya mipango, Uchumi na Fedha wa kijiji cha Mwiji, Joseph Mathias, amesema semina walioipata inawapa nguvu kubwa ya utendaji kwenye masuala mbalimbali ikiwemo manunuzi, upangaji wa bajeti, matumizi bora ya fedha na uwajibikiaji wa kiongozi kwa ngazi ya Halmashauri ya Kijiji.

“Mafunzo tuliyopata hapa tunaenda kuyaishi kwa kufanya kazi hususani kamati ya fedha kwa kuwa tuikuwa tunafanya kazi kwa kutumia busara sasa tumejengewa uwezo na tumepata miongozo wa kufanya kazi kwa weledi” amesema Mathias.

Atupokile Japheti Mwakibata, Mjumbe wa Halmashauri ya kijiji cha Lualaje, Kamati ya Mipango,  Fedha na Uchumi, amemshukuru Afisa Tarafa ya Kipembawe kwa semina hiyo ambayo imemuongezea uelewa namna ya kuwatumikia wananchi na kuongeza mapato ya kijiji kwa kuibua vyanzo mbalimbali vya mapato kwa kushirikiana na wajumbe wenzake na wananchi.

Mafunzo ya siku moja ya elimu ya utawala bora, uongozi na menejimenti ya fedha yametolewa na Afisa Tarafa ya Kipembawe, Kasim Salimu Kilondomara na kuhudhuriwa na Watendaji, Wenyeviti na Wajumbe wa Halmashauri ya kijiji cha Mwiji na Lualaje ili kuonengeza ufanisi wa utendaji kazi na kuhakikisha maendeleo ya vijiji yanawanufaisha wananchi.

Wenyeviti wa Kijiji na Wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji wakifuatilia kwa makini mafunzo ya Utawala bora, Uongozi na Menejimenti ya fedha iliyotolewa katika ukumbi wa shule ya Sekondari Lualaje.

Afisa Tarafa ya Kipembawe, Kasim Salimu Kilondomara akitoa mafunzo ya Utawala bora, Uongozi na Menejimenti ya fedha kwa Wenyeviti wa Kijiji na Wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji katika ukumbi wa shule ya Sekondari Lualaje.

Wenyeviti wa Kijiji na Wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji wakiwa katika picha ya pamoja na Afisa Tarafa ya Kipembawe baada ya kutamatika kwa semina ya siku moja ya Utawala bora, Uongozi na Menejimenti ya fedha iliyofanyika katika ukumbi wa shule ya Sekondari Lualaje.

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.