• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

RC HOMERA: THAMANI YA FEDHA IMEONEKANA KWENYE UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI NKUNG’UNGU.

Imewekwa: February 10th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Juma Zuberi Homera ameridhishwa na matumizi ya fedha ya ujenzi wa shule ya sekondari Nkung’ungu huku akiahidi serikali kuleta fedha ya ziada kwaajili ya kujenga mabweni ya wanafunzi wa shule hiyo.

Akizungumza leo Februari 10, 2025 Mhe. Homera amesema ameona thamani ya fedha kwenye ujenzi wa shule ya sekondari Nkung’ungu ambayo imejenga vyumba vya madarasa nane na miundombinu mingine kwenye shule hiyo.

“Shule hii italeta maendeleo hapa Nkung’ungu nawapongeza wananchi waliojitolea kujenga shule hii, na nimeambiwa hapa kuwa kuna wanafunzi thelathini na moja ambao wamechaguliwa lakini bado hawajaripoti, nataka mpaka ikifika tarehe 15 mwezi Machi, 2025 wanafunzi hawa wawe wameripoti shuleni” amesema Mhe. Homera.

Mhe. Homera amesisitiza kuwa endapo wanafunzi hao hawataripoti katika kipindi hicho hatua zaidi zitachukuliwa huku akimtaka mkuu wa shule ya sekondari Nkung’ungu kuwapokea wanafunzi hao hata kama hawana sare za shule.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, Mhe. Bosco Mwanginde amemuleza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya kuwa, ujenzi wa shule hiyo ulikuwa na changamoto kadhaa ikiwemo wananchi kutaka shule hiyo ijengwe kwenye eneo jingine tofauti na ilipoamuliwa awali(Nkung’ungu) huku akitaja kuwa hizo zilikuwa ni vuguvugu za vyama vya siasa na wanasiasa ambapo kwasasa changamoto hii imekwisha.

Awali akisoma taarifa ya maendeleo ya shule ya sekondari Nkung’ungu Afisa elimu kata Nkung’ungu Mwalimu Sophia Mgumba amesema shule hiyo imejenga madarasa nane, ofisi mbili, maabara tatu, jengo moja la tehama, mkataba moja, matundu kumi ya vyoo vya wasichana, matundu kumi ya vyoo vya wavulana pamoja na kichomea taka.

“Tulipokea fedha tarehe 26 Juni 2024 kaisi cha Tsh shilingi Milioni 583,  pesa iliyotumika mpaka sasa ni milioni 433, na bakaa ni mil 149” amesema Mwalimu Mgumba.

Mwalimu Mgumba aliongeza kuwa, malengo ya mradi wa ujenzi wa shule ya sekondari Nkung’ungu ni kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza, ambapo mpaka sasa tayari wameanza kusoma huku wanafunzi waliochaguliwa wakiwa ni 83, wasichana 34, wavulana 49. Wanafunzi walioripoti ni 48,  wasichana 25 na wavulana 23.

Malengo mengine ni kupunguza umbali na utoro. Changamoto kubwa kwenye ujenzi wa shule ya sekondari Nkung’ungu kuwa ni mfumo wa manunuzi wa (NeST) uliochelesha mradi kuanza na kukamilika kwa wakati uliopangwa amesema Mwalimu Mgumba.

Mkuu wa Mkoa Mbeya, Mhe. Juma Zuberi Homera akikagua maendeleo ya ujenzi wa wa shule ya Sekondari Nkung’ungu iliopo Wilaya ya Chunya.

Muonekano wa maendeleo ya ujenzi wa shule ya Sekondari Nkung’ungu ukiwa kwenye hatua ya mwisho ya ukamilishwaji.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya akipokelewa na viongozi pamoja na kamati ya ujenzi wa shule ya sekondari Nkung’ungu baada ya kuwasili katika shule hiyo kwaajili ya kukagua maendeleo ya ujenzi.

Baadhi ya wananchi, wanafunzi na viongozi wa shule ya Sekondari Nkung’ungu wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera alipokuwa akihutubia wananchi hao mara baada ya kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa shule ya sekondari Nkung'ungu.

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.