• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

RC HOMERA" NAKUAGIZA DC SIMAMIA MSITU USICHIMBWE”.

Imewekwa: November 9th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Z. Homera  amemwagiza Mkuu wa Wilaya ya Chunya kuhakikisha anasimamia suala la misitu kuto kuingiliwa na wachimbaji  na kuwataka wanaochimba maeneo ya msitu kuacha mara moja  kwani utunzaji wa mistitu ni kwaajili ya manufaa ya sasa na baadae

Maagizo hayo ameyatoa tarehe  8/11/2023 wakati wa ziara yake alipotembelea kituo cha afya cha Sangambi  pamoja na kusikiliza kero mbalimbali za wananchi wa kata hiyo kupitia mkutano wa Hadhara ulifanyika katika viwanja vya sokoni karibu na Ofisi ya Kijiji cha Sangambi .

“Mkuu wa Wilaya simamia suala la msitu ni marufuku mtu kuingia kuchimba eneo la misitu leo hii tumejenga shule na kituo cha afya kwasababu wenzetu walitunza huu msitu   kwani kwa kuchimba eneo la msitu  mtaacha mashimo na wanafunzi watakosa maeneo ya kujifunzia” alisema Mhe. Homera

Aidha  Mhe Homera  amemwagiza Meneja  wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa  wa Mbeya kuhakikisha umeme unapatikana kwenye kituo cha Afya Sangambi huku akimpa muda wa mwezi mmoja kutekeleza agizo hilo ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za Afya kwa wananchi wanaoenda kupata huduma katika kituo hicho

 ‘’Maagizo haya nampa meneja wa TANESCO Mkoa wa Mbeya wekeni mpango wa dharula hapa hakikisheni umeme unapatikana katika kituo hiki cha afya cha Sangambi ndani ya mwezi mmoja    tunajua kuna changamoto ya vifaa lakini umeme lazima upatikane “aliongeza Mhe. Homera.

Akitoa salam za Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe.Mayeka S.Mayeka  amesema kuwa Wilaya ya Chunya amesema wilaya ya Chunya inakua kwa kasi hivyo amewataka wananchi kupitia serikali za vitongoji na vijiji kuzingatia mpango mzuri wa ujenzi jambo litakalofanya mitaa na vijiji kuwa na barabara zinazopitika pamoja na mpango mzuri wa makazi pasina kusubiri serikali kuja kusimamia zoezi hilo

Awali akisoma taarifa ya kituo cha afya cha Sangambi afisa elimu kata Mwalimu Joseph Kihwele amesema katika utekelezaji wa mradi huo wa   ujenzi wa kituo cha afya  kumekuwa na changamoto mbali mbali   ikiwa ni kukosekana kwa umeme katika kituo hicho cha Afya  pamoja na mabadiliko ya gharama za vifaa vya ujenzi.

Adam Mwakalobo, Frank Mbwilo na wengine walitoa kero zao juu ya namna serikali za vijiji zinavyopendelea baadhi ya watu kugawa maeneo ya msitu kwaajili ya machimbo jambo ambalo limepelekea mkuu wa Mkoa kupiga marufuku uchimbaji ndani ya misitu hiyo, kero nyingine zilizopatiwa majibu ni pamoja na suala la maji, Barabara na nyingine nyingi

Ziara ya Mkuu wa Mkoa Wilayani Chunya  Imedumu kwa siku tatu   kuanzi tarehe 6/11/2023 na kuhitimisha   tarehe 8/11/2023  ambapo amekagua miradi mbalimbali  yya maendeleo, misitu ya Hifadhi pamoja na kusikiliza kero mbalimbali za  wananchi na kuzipatia majibu. Ziara hiyo imehusisha kamati ya ulinzi na usalama Mkoa na wilaya na, wataalamu mbalimbali kutoka Mkoani na Halmashauri ya Wilaya ya Chunya , wakuu  wa taasisi mbalimbali na Waandishi wa Habari.

Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe.Mayeka S. Mayeka akitoa salam katika kituo cha Afya cha Sangambi wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa walipotembelea na kukagua kituo hicho.

.Akisoma taarifa fupi ya mradi wa kituo cha Afya cha Sangambi wakiti wa ziara ya Mkuu wa Mkowa wa Mbeya Mhe.Juma Z.Homera

Adam Mwakalobo mkazi wa kijiji cha Sangambi akitoa kero yake mbele ya Mkuu wa Mkoa katika mkutano wa hadhara uliofanyika eneo la Sokoni kijiji cha Sangambi   







         `

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.