• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

RC HOMERA "CHUNYA ITAKUWA NI WILAYA YA UCHUMI MKUBWA MKOANI MBEYA"

Imewekwa: March 12th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Zuberi Homera amesema wilaya ya Chunya itabadilika sana katika Nyanja mbalimbali ikiwepo miundombinu ya barabara kutokana na miradi inayotarajiwa kutekelezwa wilayani humo kwani wawekezaji mbalimbali wako tayari kuwekeza katika wilaya hiyo jambo ambalo litaongeza mzunguko wa fedha na kuketa maendeleo

Mhe. Homera ameyasema hayo wakati akizungumza katika kikao cha baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya chunya cha kujadili na kupitia hoja za Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali CAG

Mhe Homera amewataka viongozi wilayani Chunya kuendelea kuwa  na umoja na mshikamano katika utekelezaji wa Majuku yao kwani palipo na migogoro hapawezi kupata maendeleo, Migogoro sio sehemu ya serikali ya awamu ya sita na haileti maendeleo kwa Taifa

“Tunakwenda kuanza utekelezaji wa ile fursa ya uwekezaji katika kata za  Nkung’ungu na Lupa,ule uwekezaji ni Mkubwa Kampuni ziko tayari kufanya uwekezaji hivyo barabara zitatengenezwa, Chunya itakuwa ni wilaya ya Uchumi Mkubwa mkoani Mbeya, Hivyo endeleeni kuwa wamoja kwani Migogoro haina nafasi”

Awali Katibu Tawala wa Mkoa wa Mbeya Ndugu Rodrick Mpogole akizungumza katika kikao hicho, amewataka watumishi kuhakikisha wanazuia hoja za ukaguzi na pale inapojitokeza hoja ya mkaguzi ni lazima ijibiwe kwa ufasaha, aidha tufanya kazi kwa ufasaha na ufanisi ikiwa ni njia bora na sahihi ya kuzuia hoja za mdhibiti na mkaguzi wa hesabu za serikali

“Kwaniaba ya watumishi naomba niseme mambo matatu kwanza vikao hivi si vizuri sana na vinapotokea ni kwamba sisi watumishi tunashida hivyo tutengeneze mkakati wa kuzuia hoja za ukaguzi na pale ambapo hoja za ukaguzi zimejitokeza ni lazima zijibiwe kwa wakati na jambo la tatu naomba tufanye kazi kwa umakini na ufanisi kama njia ya kuzuia hoja za ukaguzi” amesema Mpogole

Nae mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka Simaon Mayeka akitoa salamu za serikali wilayani Chunya, amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Mbeya kwa kikao hicho na amesema maelekezo yote kwa mujibu wa kikao yatatekelezwa kwa ufanisi mkubwa, aidha amesisitiza watumishi kuandaa taarifa sahihi na kwa umakini mzuri ili kuepuka kupoteza muda bila sababu

“Naomba nitoe ushauri kidogo, watumishi mnapoandika taarifa ziandikwe kwa umakini ili kuepuka usumbufu na kupoteza muda bila sababu Mfano kama Kituo cha Afya mtande hoja inaeleza kutokuwepo kwa Mbao wakati Mbao zililetwa na zimetumika kujenga na tayari kituo kinafanya kazi kwahiyo niwaombe mjitahidi kuweka vizuri taarifa zenu ili kuepuka kupoteza muda”

Naye Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Tamimu Kambona amesema Mpaka sasa halmashauri ya wilaya ya Chunya ina asilimia tisini (90%) ya ukusanyaji wa mapato na bila shaka wanaongoza katika Mkoa na lengo sio kuongoza kwenye mapato peke yake bali na maeneo mengine mengi na sababu ya kuongoza kwao ni ushirikiano mzuri kati ya ofisi ya Mkuu wa wilaya na ofisi ya Mkurugenzi lakini pia usimizi mzuri wanaoupata kutoka kwa baraza la madiwani likiongozwa na Mwenyekiti wake makini Mhe Bosco Mwanginde ambaye ni  Diwani wa kata ya Mbugani

Kwa Upande wa Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mhe Bosco Mwanginde wakati akihitimisha kikao hicho amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Kwa busara, hekima na utulivu  wakati wa kikao hicho muhimu cha kujadili hoja za mkaguzi wa Hesabu za Serikali  katika halmashauri ya wilaya ya Chunya

Aidha Mweshimiwa Mwanginde amemuhakikishia Mkuu wa Mkoa kwamba baraza la madiwani wilayani Chunya wataendelea kusimamia utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chunya itaendelea kuongoza katika Nyanja zote katika mkoa wa Mbeya na hatimaye Taifa kwa ujumla

Baraza hilo la Madiwa liliketi tarehe 10/03/2023 katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya wilaya ya Chunya (Sapanjo) Lengo likiwa kujadili hoja mbalimbali kutoka Ofisi ya  Mkaguzi wa Hesabu za serikali zilizotokana na ukaguzi maalumu ulifanyika hivi karibuni na kufanyia kazi mapendekezo ya Ofisi ya CAG

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mhe. Bosco Mwanginde akizungumza katika kikao cha Baraza Maalumu la Madiwani lililoketi Machi 10 kujadili  hoja za Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.