• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

RC HOMERA, AFUNGUA RASMI MASOKO YA TUMBAKU MKOA WA KITUMBAKU CHUNYA.

Imewekwa: May 18th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mbe. Juma Zuberi Homera amesema Serikali ya awamu ya sita ina lenga kumkwamua mwananchi wa chini akiwepo mkulima wa zao la Tumbaku ndio sababu inahakikisha soko la Tumbaku linasimamiwa ipasavyo jambo ambalo limeleta faraja kwa wakulima katika msimu wa kilimo wa mwaka 2022/2023 ambapo bei ya Tumbaku katika mkoa wa Kitumbaku Chunya ni dola 2.42 huku wastani wa bei nchini ikiwa ni dola 2.0

Akizungmza katika hafla ya ufunguzi rasmi wa masoko ya Tumbaku katika mkoa wa kitumbaku Chunya katika Chama cha msingi Mtanila Mhe Homera amewapongeza wakulima wa tumbaku kwanza kwa namna wanavyoshiriki katika kilimo lakini pia amewataka viongozi kuendelea kuwasimamia wakulima katika maeneo mbalimbali ili uzalishaji wao uwe wenye tija

“Bei nilizoziona ni nzuri sana na nimpongeze sana mnuzi kwa bei hizi, lakini pia niwapongeze wanamtanila kwasababu wameandaa vizuri sana Tumbaku kasoro hizi chache zisitufanye turudi nyuma bali tuzirekebishe na tusonge mbele lakini nimeona viongozi wa chama hiki wako smati na muendelee kuwasimamia vizuri wakulima ili waendelee kuzalisha kwa tija, Msione bei inachangamka namna hii Mhe Rais ameona Zao la Tumbaku liwe zao la kumkwamua Mwananchi”

Aidha Mkuu wa Mkoa amezindua rasmi ghala la Chama cha Msingi Mtanila lenye uwezo wa kubeba mituma 2500 kwa wakati mmoja lenye thamani ya milioni 200 pia amekabidhi trekta lenye thamani ya milioni 73 kwa chama cha Msingi Mtanila na baadaye amewakabidhi pikipiki za magurudumu matatu (Guta) wakulima kumi baada ya kupata Mkopo kutoka Banki ya Azania

“Vyama vichache sana vinanunua vyombo kama hivi, wangekuwa wengine wangepiga dili, wangesema trekta hili limenunuliwa kwa milioni 100 lakini ninyi mmeenda kwenye uhalisia milioni 73 zimetumika hongereni sana, muendelee hihivi na mwakani muongeze trekta linguine, hongereni sana Mtanila”

Meneja wa Banki ya Azania Ndugu Samson Basil Mahimbi amesema wao kama wadau wa kilimo wataendelea kutoa mikopo kwa riba nafuu kwa wakulima ikiwa ni kutekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi ambayo inalenga kuwaletea wananchi wake Maendeleo

“Mtanila ni miongozi mwa vyama saba ambavyo msimu uliopita tumewakopesha zaidi ya dola milioni saba na nusu sawa na bilioni 17 na wakulima zaidi ya 3000 wamenufaika na mikopo toka Azania kwa asilimia saba na mwakani tutaendelea kufanya hivyo ili tunaposema Azania Benki ni bega kwa began a wakulima huwa tuna maanisha kweli”

Awali aikitoa taarifa kwa mgani rasmi, viongozi wa serikali, taasisi za serikali na binafsi pamoja na wananchi waliojitokeza Mhasibu Mkuu wa Chama cha Msingi cha Mtanila Ndugu SEIF MARIJANI amesema chama kimefanikiwa maeneo mbalimbali huku akitaja changamoto ya Mbolea kukwamisha maendeleo ya kilimo.

“Chama cha Msingi Mtanila kimefanikiwa kujenga ghala la kuhifadhia tumbaku lenye uwezo wa kuhifadhi mitumba 2500 kwa wakati mmoja, tumefanikiwa kunua trekta kwa gharama ya milioni 73 kupitia mapato ya ndani, chama kina mfuko wa pembejeo, kujenga ofisi ya Chama, kuandaa shamba la miti ambalo limepandwa miti laki moja mwaka 2023 lakini tunazo changamoto ya pembejeo za kilimo tofauti na misimu mingine iliyopita”

Hafla ya ufunguzi rasmi wa masoko ya Tumbaku katika Mkoa wa Kitumbaku Chunya imefanyika tarehe 17/5/2023 katika kata ya Mtanila ambapo Chama cha Msingi Mtanila kilikuwa mwenyeji kwa niaba ya vyama vingine 27 ambapo shughuli mbalimbali zilifanyikiwa ikiwepo uzinduzi wa ghala, kukabidhi trekta, pamoja na kukabidhi pikipiki za Magurudumu Matatu kwa wakulima kumi ambapo banki ya Azania imewakopesha wakulima hao.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera akizindua Ghala la kuifadhia Tumbaku chama cha Msingi Mtanila

Muonekano wa Ghala la Kuifadhia Tumbaku Chama cha Msingi Mtanila

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.