• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

ONGEZENI KUTAFUTA MAENEO ZAIDI YA KUJENGA SHULE ZA MCHEPUO WA KIINGEREZA MAANA CHUNYA INAKUA KWA KASI

Imewekwa: November 27th, 2023

Kamati ya Uendeshaji ya Halmashauri ya Wilaya Ya Chunya (CMT) imewataka idara ya Elimu awali na msingi kuendelea kutafuta maeneo zaidi yatakayotumika kujenga shule nyingine za Mchepuo wa Kiingereza maana wilaya ya Chunya inakua kwa kasi hivyo lazima na mahitaji ya shule za mchepuo wa kiingereza yataongeza

Rai hiyo imetolewa leo 27/11/2023 na CMT ikiongozwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo Ndugu Athuman Bamba akikaimu nafasi ya Mkurugenzi mtendaji baada ya kamati hiyo kutembelea shule ya Chunya Pre & Primary English Medium School inayomilikiwa na Halmashauri ya wilaya ya Chunya ilipoenda kukagua eneo ambalo yanajengwa madarasa manne ambapo chanzo cha fedha za ujenzi ikiwa ni mapato ya Ndani

“Maeneo zaidi yatafutwe kwaajili ya ujenzi wa shule nyingine za mchepuo wa Kiingereza maana wilaya ya Chunya inakua kwa kasi hivyo uhitaji wa huduma kama hii utakuwa ni mkubwa kuliko sasa hivyo afisa Elimu awali na msingi jaribu kutafuta maeneo makubwa na mazuri kwaajili ya kujenga shule za namna hii” Amesema Ndugu Bamba

Naye Kaimu Mkuu wa idara ya Mipango na uratibu ndugu Nebart Gavu ameshauri uongozi wa shule kwakushirikiana na ofisi ya Afisa Elimu awali na msingi waandae mpango unaoonesha lengo la shule hiyo ni kuhudumia wanafunzi wangapi na idadi hiyo itumike kukadiria idadi ya majengo yanayokusudiwa na baadaye eneo lote lipangwe mapema ili kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza hapo baadaye

“Naomba muandae mpango kazi kwamba shule hii inahitaji kuwa na madarasa mangapi na orodha hiyo tukiipata wahandisi waandae mpango wa matumizi ya eneo maana tukichelewa kufanya hivyo inaweza kuleta changamoto hapo baadaye na zile kauli za kwamba tungejua mapema jengo Fulani tungejenga hapa au pale” Alisema Nebert Gavu

Akifafanua baadhi ya mambo yaliyoulizwa na kamati hiyo kaimu Afisa Elimu  awali na msingi wilaya ya Chunya Mwalimu  Abdallah Mcheru amesema lengo la awali la kujenga shule hiyo ilikuwa ni kila darasa kuwa na mikondo miwili kwa kila darasa lakini amesema jambo la kuleta mapendekezo ya matumizi bora ya eneo la shule hiyo yatafanyiwa kazi kwa wakati na kuyawasilisha kwenye vikao vijavyo

“Usajili wa shule hii kwasasa ni mikondo miwili kwa kila darasa kwa maana ya wanafunzi 90 yaani arobaini na tano kwa kila mkondo lakini sasa ni kweli kuna haja ya kujadili mwendelezo wa shule hii na sisi tutayafanyia kazi mapendekezo hayo” Amesema Mwalimu Mcheru

Ziara hiyo imekuja baada ya kikao cha asubuhi ya leo Mhandisi wa Halmashauri Eng Charles Kway kupitia Afisa Elimu Msingi kuwasilisha mchoro wa ujenzi wa madarasa manne wenye mabadiriko baada ya mchoro wa awali kutokutosha kulingana na eneo hilo na ndipo mwenyekiti alishauri wajumbe kufika eneo la ujenzi na kushauri yote yanayowezekana kushauri

Kupitia mapato ya ndani Halmashauri ya wilaya ya Chunya inajenga madarasa manne kwa gharama ya shilingi milioni mia moja (100) katika shule ya Mchepuo wa Kiingereza Chunya ili kujiandaa kwa mwaka wa masomo 2024 ambapo mpaka sasa fedha hizo zimetolewa na tayari taratibu mbalimbali za ujenzi zinaendelea

Picha za Madarasa yanayojengwa shule ya Mchepua wa Kingereza Chunya, Mchoro huo umetengezwa na wataalamu (Wahandisi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

Wajumbe wa kamati ya uendeshaji ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya wakiwa eneo linalojengwa madarasa manne Shule ya awali na msingi mchepuo wa Kiingereza Chunya (Aliyenyoosha mkono mwenye suti nyeusi ni kaimu Mkurugenzi mtendaji Mwana Athuman Bamba na ndiye alikuwa mwenyekiti wa kikao kilichoamua kutembelea eneo hilo, na mwingine aliyenyoosha mkono ni Mhandisi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Eng Charlse Kway)

Wajumbe kamati ya uendeshaji ya Halmashauri ikiendelea kushauriana mambo mbalimbali kuhusu ujenzi wa madarasa katika shule ya Mchepua wa Kiingereza Chunya (Aliyeshika Karatasi Ni Mhandisi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Eng Charlse Kway, anayefuata kulia kwake na amenyoosha mkoa ni kaimu mkuu wa idara ya Mipango na Uratibu ndugu Nebart Gavu na anayefuata ni Mweka hazina wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Rajabu Lingoni

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.