• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

ONGEZENI JUHUDI KUJIFUNZA KINGEREZA ITAWASAIDIA KUFIKIA NDOTO ZENU

Imewekwa: January 12th, 2024


Afisa Elimu awali na Msingi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mwalimu ferd Y Mhanze ameawata wanafunzi wa sekondari wilaya ya Chunya kuongeza juhudi za kujifunza Lugha ya kingereza kwani itawarahishia kujibu mitihani yao ya kidato cha pili inayowakabili lakini pia itawapa uwezo wa kujieleza katika ulimwengu huu wa maendeleo ya Sayansi na Teknolojia

Ametoa kauli hiyo mapema leo wakati alipopata nafasi ya kuongea na wanafunzi wa kidato cha pili shule ya sekondari Bitimanyanga iliyoko kata ya Mafyeko wakati wa ziara ya kamati ya Fedha Uchumi na Mipango ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya ikikagua  miradi mbalimbali inayotekelezwa katika Halmashauri ya wilaya ya Chunya

“Ongezeni juhudi sana katika kujifunza Lugha ya kingereza maana ndiyo Lugha inayotumiwa kuwatahini na hata katika mawasiliano mbalimbali ya kimataifa hutumika Lugha ya Kingereza na msipofanya hivyo maana yake mmeamua kufeli maana masomo yote isipokuwa somo la Kiswahili pekee ndilo mnajifunza kwa Kiswahili na mtatahiniwa kwa Lugha ya Kiswahili”

Aidha Mwalim Mhanze amewataka wanafunzi hao kutumia vizuri fursa waliyoipata ya kusoma katika kipindi ambacho serikali imeboresha mazingira ya kusomea bila kujali jiografia  ikiwa ni pamoja na uwepo wa Maabara za fizikia. Kemia na baiolojia kwenye shule za sasa ni tofauti na ilivyokuwa miaka ya zamani.

“Ninyi mna bahati sana ila mnashindwa kuitumia, serikali inaleta fedha nyingi na nyinyi ni mashahidi, leo maktaba, maabara zinajengwa hivyo mnasoma hata kwa vitendo moja kwa moja, sisi wenzenu tulipokuwa tnasoma tulisoma “Luminous frame” lakini hatukuona hiyo “luminous frame” kwa macho maana “Bansen Barner” Hazikuwepo lakini ninyi mnasoma Darasani na baadaye mnaenda maabara kuona kile alichofundishwa mwalimu, Hiyo ni fursa itumieni” Amesema Mwalimu Mhanze

Naye afisa Elimu wa sekondari wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mwalimu Hamis Mapoto alipata nafasi ya kuungana na Mwalimu Mhanze Darasani baada ya kukamilisha ukaguzi wa mradi wa  matundu sita ya vyoo na ukarabati wa madarasa mawili ambapo amewambia wanafunzi hao kwamba wao wamepata bahati ya kutembelewa na viongozi wakubwa hivyo iwe chachu kwao katika masomo yao

Wakizungumza kwa niaba ya wanafunzi wenzao wa kidato cha pili wa  Elika Samson Briyton, Maimuna John Kawila na Clever Yonifat Mbuza wamesema sababu kubwa inayopelekea wanafunzi wengine kufeli ni uvivu wa kusoma hivyo wao wamewaahidi viongozi waliowatembelea kusoma kwa bidii na kujituma ili kumtendea haki Mhe Rais anayepeleke fedha za kujenga na kuendelea kuboresha miundombinu ya shule hiyo

Shule ya sekondari Bitimanyanga imepewa fedha shilingi milioni 31 ili kukamilisha madarasa mawili ambayo yalikuwa maboma na kujenga matundu sita ya vyoo ikiwa ni juhudi za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuboresha sekta ya elimu nchini.

Mwalimu Mhanze akiwa anaeleza jambo wakati alipokuwa anazungumza na wanafunzi wa kidato cha Pili Shule ya Sekondari BitiManyanga

Mwalimu Mhanze akiwa darasani na katika picha ishara hiyo alikuwa anasisitiza umuhimu wa kiingereza kufikia ndoto zako za Mbeleni

Bado kwa msisitizo mkubwa Mwalimu Mhanze akionesha ishara mbalimbali huku akisisitiza umuhimu wa kusoma kwa bidii huku mkazo ukiwa kwenye Lugha ya Kiingereza

Mwanafunzi Elika Samson Brayton wa shule ya sekondari Bitimanyanga kidato cha Pili akijibu swali wakati wakipewa maelekezo na Mwalimu Mhanze

Mwanafunzi Clever Yonifat Mbuza akijibu swali aliloulizwa na Mwalimu Mhanze wakati akizungumza na wanafunzi hao kuhusu umuhimu wa kituma kujifunza Lugha ya Kiingereza

Wanafunzi wa kidato cha pili wakiwa wanasikiliza kwa umakini maelekezo na kwa Mbali mwanafunzi  Maimuna John Kawili amenyoosha mkono akionesha anataka kuuliza jambo kwa mwalimu Mhanze ili kufikia ndoto zake

Afisa elimu Sekondari wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mwalimu Hamis Mapoto   akizungumza Jambo na wanafunzi wa kidato cha pili baada ya kukamilisha zoezi la ukaguzi wa miradi chini ya kamati ya fedha, uchumi na mipango ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.